Yeremia 1:1-19

  • Yeremia awekwa kuwa nabii (1-10)

  • Maono ya mti wa mlozi (11, 12)

  • Maono ya chungu cha kupikia (13-16)

  • Yeremia atiwa nguvu kwa ajili ya utume wake (17-19)

1  Haya ndiyo maneno ya Yeremia* mwana wa Hilkia, mmoja wa makuhani wa Anathothi+ katika nchi ya Benjamini.  Neno la Yehova lilimjia katika siku za Yosia+ mwana wa Amoni,+ mfalme wa Yuda, katika mwaka wa 13 wa utawala wake.  Pia lilikuja katika siku za Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, hadi mwishoni mwa mwaka wa 11 wa utawala wa Sedekia+ mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, mpaka Yerusalemu lilipoenda uhamishoni katika mwezi wa tano.+  Neno la Yehova lilinijia, likisema:   “Kabla sijakuumba tumboni nilikujua,*+Na kabla hujazaliwa* nilikutakasa.*+ Nilikufanya uwe nabii kwa mataifa.”   Lakini nikasema: “Ole wangu, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova! Mimi sijui kuzungumza,+ kwa maana mimi ni mvulana* tu.”+   Kisha Yehova akaniambia: “Usiseme, ‘Mimi ni mvulana tu.’ Kwa maana ni lazima uende kwa wote nitakaokutuma kwao,Nawe unapaswa kusema kila jambo nitakalokuamuru.+   Usiogope kwa sababu ya jinsi wanavyoonekana,+Kwa maana ‘mimi niko pamoja nawe ili nikuokoe,’+ asema Yehova.”  Kisha Yehova akaunyoosha mkono wake na kugusa kinywa changu.+ Na Yehova akaniambia: “Nimeyatia maneno yangu kinywani mwako.+ 10  Tazama, nimekutuma leo hii ili uwe juu ya mataifa na juu ya falme, ili kung’oa na kubomoa, ili kuangamiza na kuangusha, ili kujenga na kupanda.”+ 11  Neno la Yehova likanijia tena, likisema: “Unaona nini, Yeremia?” Basi nikasema: “Ninaona tawi la mti wa mlozi.”* 12  Yehova akaniambia: “Uko sahihi, kwa maana niko macho kabisa kuhusu neno langu ili kulitimiza.” 13  Neno la Yehova likanijia mara ya pili, likisema: “Unaona nini?” Basi nikasema: “Ninaona chungu* kinachochemka,* na mdomo wake umeinama kutoka kaskazini.” 14  Kisha Yehova akaniambia: “Msiba utafunguliwa kutoka kaskaziniDhidi ya wakaaji wote wa nchi.+ 15  Kwa maana ‘ninaziita familia zote za falme za kaskazini,’ asema Yehova,+‘Nao watakuja; kila mmoja ataweka kiti chake cha ufalmeKwenye malango ya Yerusalemu,+Dhidi ya kuta zake pande zoteNa dhidi ya majiji yote ya Yuda.+ 16  Nami nitatangaza hukumu zangu dhidi yao kwa sababu ya uovu wao wote,Kwa sababu wameniacha,+Nao wanaifukizia miungu mingine moshi wa dhabihu+Na kuziinamia kazi za mikono yao wenyewe.’+ 17  Lakini unapaswa kuwa tayari kuchukua hatua,*Nawe unapaswa kusimama na kuwaambia kila jambo ninalokuamuru. Usiwaogope,+Ili nisikuogopeshe mbele yao. 18  Kwa maana leo nimekufanya uwe jiji lenye ngome,Nguzo ya chuma, na kuta za shaba dhidi ya nchi yote,+Kuelekea wafalme wa Yuda na wakuu wake,Kuelekea makuhani wake na watu wa nchi.+ 19  Nao hakika watapigana nawe,Lakini hawatakushinda,Kwa maana ‘Mimi niko pamoja nawe,’+ asema Yehova, ‘ili nikuokoe.’”

Maelezo ya Chini

Huenda jina hili linamaanisha “Yehova Huinua.”
Au “nilikuchagua.”
Tnn., “kabla hujatoka tumboni.”
Au “nilikuweka kando.”
Au “kijana.”
Tnn., “yule anayeamka.”
Au “chungu cha kupikia chenye mdomo mpana.”
Tnn., “kinachopuliziwa,” kuonyesha moto unaochochewa chini yake.
Tnn., “kujifunga kiuno.”