Yeremia 10:1-25

  • Mungu aliye hai atofautishwa na miungu ya mataifa (1-16)

  • Uharibifu na uhamisho unaokuja (17, 18)

  • Yeremia aomboleza (19-22)

  • Sala ya nabii (23-25)

    • Mwanadamu hawezi kuongoza hatua yake mwenyewe (23)

10  Sikieni neno ambalo Yehova amesema dhidi yenu, enyi watu wa nyumba ya Israeli.  Yehova anasema hivi: “Msijifunze njia ya mataifa,+Wala msihofu ishara za mbinguniKwa sababu mataifa yanazihofu.+   Kwa maana desturi za mataifa ni udanganyifu.* Ni mti tu wa msituni uliokatwa,Uliochongwa kwa mikono ya fundi kwa kifaa chake.*+   Wanaupamba kwa fedha na dhahabu+Wanaupigilia misumari kwa nyundo ili usianguke.+   Kama sanamu ya kufukuza ndege katika shamba la matango, haziwezi kuzungumza;+Lazima zibebwe, kwa maana haziwezi kutembea.+ Msiziogope kwa maana haziwezi kuwadhuru,Wala haziwezi kufanya jambo lolote jema.”+   Hakuna yeyote aliye kama wewe, Ee Yehova.+ Wewe ni mkuu, na jina lako ni kuu na lenye nguvu.   Ni nani asiyepaswa kukuogopa, Ee Mfalme wa mataifa,+ kwa maana ni jambo linalofaa;Kwa sababu kati ya watu wote wenye hekima wa mataifa na kati ya falme zao zote,Hakuna yeyote yule aliye kama wewe.+   Wote hawatumii akili nao ni wajinga.+ Mafundisho kutoka kwa mti ni udanganyifu* mtupu.+   Mabamba ya fedha huletwa kutoka Tarshishi+ na dhahabu kutoka Ufazi,Kazi ya fundi, ya mikono ya mhunzi. Mavazi yao ni nyuzi za bluu na sufu ya zambarau. Vyote hutengenezwa na wafanyakazi stadi. 10  Lakini kwa kweli Yehova ni Mungu. Yeye ndiye Mungu aliye hai+ na Mfalme wa milele.+ Kwa sababu ya ghadhabu yake dunia itatetemeka,+Na hakuna taifa litakalostahimili shutuma yake. 11  * Waambieni hivi: “Miungu ambayo haikuumba mbingu na duniaItaangamia kutoka duniani na kutoka chini ya hizi mbingu.”+ 12  Yeye ndiye Muumba wa dunia kwa nguvu zake,Yule aliyeiimarisha ardhi inayozaa kwa hekima yake+Na aliyezitandaza mbingu kwa uelewaji wake.+ 13  Anapofanya sauti yake isikike,Maji yaliyo mbinguni husukasuka,+Naye huyafanya mawingu yapande* kutoka kwenye miisho ya dunia.+ Hutengeneza radi* kwa ajili ya mvua,Naye huutoa upepo katika maghala yake.+ 14  Kila mtu anatenda bila kutumia akili na bila ujuzi. Kila fundi wa chuma ataaibishwa kwa sababu ya sanamu ya kuchongwa;+Kwa maana sanamu yake ya chuma* ni uwongo,Nazo hazina roho* ndani yake.+ 15  Sanamu hizo ni udanganyifu,* kazi ya mzaha.+ Siku yao ya hukumu itakapofika, zitaangamia. 16  Fungu la Yakobo si kama vitu hivyo,Kwa maana Yeye ndiye aliyeumba kila kitu,Na Israeli ndiyo fimbo ya urithi wake.+ Yehova wa majeshi ndilo jina lake.+ 17  Kusanya mzigo wako kutoka ardhini,Ewe mwanamke uliyezingirwa. 18  Kwa maana Yehova anasema hivi: “Tazama, ninawatupa* nje wakaaji wa dunia wakati huu,+Nami nitawafanya wataabike.” 19  Ole wangu kwa sababu ya jeraha langu!*+ Kidonda changu hakiwezi kupona. Nami nilisema: “Kwa hakika huu ni ugonjwa wangu, na lazima niuvumilie. 20  Hema langu limeharibiwa, na kamba zangu zote za mahema zimekatwa.+ Wanangu wameniacha na hawapo tena.+ Hakuna yeyote aliyebaki wa kulitandaza hema langu au kuviinua vitambaa vyangu vya mahema. 21  Kwa maana wachungaji wametenda kwa upumbavu,+Wala hawajatafuta ushauri kutoka kwa Yehova.+ Ndiyo sababu hawajatenda kwa ufahamu,Na kondoo wao wote wametawanyika.”+ 22  Sikiliza! Habari! Inakuja! Kishindo kikubwa kutoka nchi ya kaskazini,+Ili kuyafanya majiji ya Yuda yawe ukiwa, mapango ya mbwamwitu.+ 23  Ninajua vema, Ee Yehova, kwamba njia ya mwanadamu haimo katika uwezo wake. Mwanadamu anayetembea hana uwezo wa kuongoza hatua yake.+ 24  Nirekebishe, Ee Yehova, kulingana na hukumu,Lakini si katika hasira yako,+ usije ukanimaliza.+ 25  Yamwagie ghadhabu yako mataifa yanayokupuuza+Na familia ambazo haziliitii jina lako. Kwa maana wamemnyafua Yakobo,+Naam, wamemnyafua na kumwangamiza kabisa,+ Nao wameifanya nchi yake ukiwa.+

Maelezo ya Chini

Au “ubatili.”
Au “tezo yake.”
Au “ubatili.”
Mwanzoni, mstari wa 11 uliandikwa katika Kiaramu.
Au labda, “malango.”
Au “Huufanya mvuke upande.”
Au “sanamu ya kuyeyushwa.”
Au “pumzi.”
Au “ubatili.”
Au “ninawarusha.”
Au “jeraha langu la kuvunjika.”