Yeremia 11:1-23

  • Yuda avunja agano lake pamoja na Mungu (1-17)

    • Miungu mingi kama majiji (13)

  • Yeremia afananishwa na mwanakondoo anayepelekwa machinjioni (18-20)

  • Yeremia apingwa na watu wa mji wa nyumbani kwao (21-23)

11  Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Yehova, likisema:  “Enyi watu, sikieni maneno ya agano hili! “Watangazie* maneno haya watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalemu,  nawe uwaambie, ‘Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: “Amelaaniwa mtu asiyetii maneno ya agano hili,+  niliyowaamuru mababu zenu siku niliyowatoa nchini Misri,+ kutoka katika tanuru la kuyeyushia chuma,+ nikisema, ‘Tiini sauti yangu, nanyi mfanye mambo yote ninayowaamuru; nanyi mtakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wenu,+  ili nitimize kiapo nilichowaapia mababu zenu, kwamba nitawapa nchi inayotiririka maziwa na asali,+ kama ilivyo leo hii.’”’” Nami nikajibu: “Amina,* Ee Yehova.”  Kisha Yehova akaniambia: “Tangaza maneno haya yote katika majiji ya Yuda na kwenye barabara za Yerusalemu: ‘Sikieni maneno ya agano hili, na myatekeleze.  Kwa maana niliwaonya vikali mababu zenu siku niliyowatoa nchini Misri na mpaka leo hii, niliwaonya tena na tena:* “Tiini sauti yangu.”+  Lakini hawakusikiliza wala kutega sikio lao; badala yake, kila mmoja wao aliendelea kuufuata kwa ukaidi moyo wake mwovu.+ Basi nikawaadhibu kulingana na maneno yote ya agano hili niliyowaamuru wafuate, lakini walikataa kuyatekeleza.’”  Kisha Yehova akaniambia: “Kuna njama kati ya watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalemu. 10  Wameyarudia makosa ya mababu zao wa zamani, waliokataa kutii maneno yangu.+ Wao pia wameifuata miungu mingine na kuiabudu.+ Watu wa nyumba ya Israeli na wa nyumba ya Yuda wamevunja agano langu nililofanya pamoja na mababu zao.+ 11  Kwa hiyo Yehova anasema hivi: ‘Ninawaletea msiba+ ambao hawataweza kuuepuka. Watakaponiomba msaada, sitawasikiliza.+ 12  Kisha majiji ya Yuda na wakaaji wa Yerusalemu wataenda kwa miungu wanayoitolea dhabihu* na kuomba msaada,+ lakini kwa vyovyote vile haitawaokoa watakapopatwa na msiba. 13  Kwa maana miungu yenu imekuwa mingi kama majiji yenu, enyi watu wa Yuda, nanyi mmekitengenezea kitu cha aibu* madhabahu nyingi kama barabara zilizo Yerusalemu, madhabahu za kumtolea dhabihu Baali.’+ 14  “Lakini wewe,* usisali kwa ajili ya watu hawa. Usipaze kilio au kusali kwa ajili yao,+ kwa maana sitasikiliza watakaponililia kwa sababu ya msiba wao. 15  Mpendwa wangu ana haki gani ya kuwa katika nyumba yanguWakati watu wengi wametekeleza njama nyingi za uovu? Je, kwa nyama takatifu* watauzuia msiba utakapokujia? Je, utafurahi wakati huo? 16  Wakati fulani Yehova alikuita mzeituni unaositawi,Maridadi na wenye matunda mazuri. Kwa sauti yenye mngurumo mkubwa, ameuwasha moto mzeituni huo,Nao wamevunja matawi yake. 17  “Yehova wa majeshi, Aliyekupanda,+ ametangaza kwamba msiba utakujia wewe kwa sababu ya uovu uliotendwa na watu wa nyumba ya Israeli na wa nyumba ya Yuda, ambao wamenikasirisha kwa kumtolea dhabihu Baali.”+ 18  Yehova alinijulisha ili nijue;Wakati huo ulinionyesha mambo waliyokuwa wakitenda. 19  Nilikuwa kama mwanakondoo mtulivu anayepelekwa machinjioni. Sikujua kwamba walikuwa wakipanga njama dhidi yangu:+ “Na tuuangamize ule mti na matunda yake,Na tumkate kabisa kutoka kwenye nchi ya walio hai,Ili jina lake lisikumbukwe kamwe.” 20  Lakini Yehova wa majeshi huhukumu kwa uadilifu;Huchunguza mawazo ya ndani kabisa* na pia moyo.+ Acha nione ukiwalipiza kisasi,Kwa maana nimeileta kesi yangu kwako. 21  Kwa hiyo Yehova anasema hivi dhidi ya watu wa Anathothi+ wanaotaka kukuua* na wanaosema: “Usitabiri katika jina la Yehova,+ la sivyo tutakuua kwa mikono yetu”; 22  kwa hiyo Yehova wa majeshi anasema hivi: “Tazama, nitawaadhibu.* Vijana watakufa kwa upanga,+ na wana wao na mabinti wao watakufa kwa njaa kali.+ 23  Hakuna yeyote atakayebaki kati yao, kwa maana nitawaletea msiba watu wa Anathothi+ katika mwaka wao wa kuadhibiwa.”*

Maelezo ya Chini

Inaonekana Yeremia ndiye anayeambiwa.
Au “Na iwe hivyo!”
Tnn., “nilikuwa nikiamka mapema na kuwaonya.”
Au “moshi wa dhabihu.”
Au “mungu wa aibu.”
Yaani, Yeremia.
Yaani, dhabihu zilizotolewa hekaluni.
Au “hisia za ndani kabisa.” Tnn., “figo.”
Au “wanaoitafuta nafsi yako.”
Au “nitawafanya wawajibike.”
Au “kuwajibishwa.”