Yeremia 12:1-17

  • Yeremia alalamika (1-4)

  • Jibu la Yehova (5-17)

12  Wewe ni mwadilifu, Ee Yehova,+ ninapokuletea malalamishi yangu,Ninapozungumza nawe kuhusu mambo ya haki. Lakini kwa nini njia ya waovu imefanikiwa,+Na kwa nini watu wenye hila hawana wasiwasi?   Uliwapanda, nao wametia mizizi. Wamekua na kuzaa matunda. Wewe uko kwenye midomo yao, lakini uko mbali na mawazo yao ya ndani kabisa.*+   Lakini unanijua vema, Ee Yehova,+ unaniona;Umeuchunguza moyo wangu na kuupata ukiwa katika muungano nawe.+ Waweke kando kama kondoo wa kuchinjwa,Na uwatenge kwa ajili ya siku ya kuuawa.   Nchi itaendelea kunyauka mpaka liniNa majani ya kila uwanja kukauka?+ Kwa sababu ya uovu wa wale wanaokaa ndani yake,Wanyama na ndege wamefagiliwa mbali. Kwa maana wamesema: “Haoni kitakachotupata.”   Ikiwa unachoka unapokimbia pamoja na watu waendao kwa miguu,Unawezaje kushindana mbio na farasi?+ Hata kama una uhakika katika nchi ya amani,Itakuwaje kwako kati ya vichaka vikubwa kando ya Yordani?   Kwa maana hata ndugu zako mwenyewe, nyumba ya baba yako mwenyewe,Wamekutendea kwa hila.+ Wamelia kwa sauti kubwa dhidi yako. Usiwe na imani nao,Hata wakikuambia mambo mema.   “Nimeiacha nyumba yangu;+ nimeuacha urithi wangu.+ Mpendwa wangu nimpendaye sana* nimemtia mikononi mwa maadui wake.+   Urithi wangu umekuwa kwangu kama simba msituni. Amenguruma dhidi yangu. Kwa hiyo nimemchukia.   Urithi wangu ni kama ndege anayewinda mwenye rangi nyingi;*Ndege wengine wanaowinda wanamzunguka na kumshambulia.+ Njooni, kusanyikeni pamoja, ninyi nyote wanyama wa mwituni,Njooni mle.+ 10  Wachungaji wengi wameliharibu shamba langu la mizabibu;+Wamelikanyaga-kanyaga shamba langu.+ Wameligeuza shamba langu linalotamanika kuwa nyika yenye ukiwa. 11  Limekuwa ukiwa;Limenyauka;*Limekuwa mahame mbele zangu.+ Nchi yote imefanywa kuwa mahame,Lakini hakuna mtu anayelitia jambo hilo moyoni.+ 12  Waangamizaji wamekuja kwenye vijia vyote vya nyikani vilivyokanyagwa sana,Kwa maana upanga wa Yehova unanyafua kuanzia mwisho mmoja wa nchi mpaka mwisho wa pili.+ Hakuna amani kwa yeyote.* 13  Wamepanda ngano, lakini wamevuna miiba.+ Wamejichosha wenyewe, lakini hawajapata faida yoyote. Wataona aibu kwa sababu ya mazao yaoKwa sababu ya hasira ya Yehova inayowaka.” 14  Yehova anasema hivi dhidi ya majirani wangu wote waovu, wanaogusa urithi niliowamilikisha watu wangu Waisraeli:+ “Tazama, ninawang’oa kutoka kwenye nchi yao,+ nami nitawang’oa watu wa nyumba ya Yuda kutoka kati yao. 15  Lakini baada ya kuwang’oa, nitawaonyesha tena rehema na kumrudisha kila mmoja wao kwenye urithi wake na kwenye ardhi yake.” 16  “Na wakihakikisha kwamba wanajifunza njia za watu wangu na kuapa kwa jina langu, ‘Kwa hakika kama Yehova anavyoishi!’ kama walivyowafundisha watu wangu kuapa kwa jina la Baali, ndipo watakapojengwa miongoni mwa watu wangu. 17  Lakini wakikataa kutii, mimi pia nitaling’oa taifa hilo, nitaling’oa na kuliangamiza,” asema Yehova.+

Maelezo ya Chini

Au “hisia zao za ndani kabisa.” Tnn., “figo zao.”
Au “Mpendwa wa nafsi yangu.”
Au “mwenye madoadoa.”
Au labda, “Linaomboleza.”
Tnn., “wote wenye mwili.”