Yeremia 13:1-27

  • Mshipi wa kitani ulioharibika (1-11)

  • Mitungi ya divai itavunjwavunjwa (12-14)

  • Watu wa Yuda wasioweza kubadilika watapelekwa uhamishoni (15-27)

    • “Je, Mkushi anaweza kuibadili ngozi yake?” (23)

13  Yehova aliniambia hivi: “Nenda ukajinunulie mshipi wa kitani ujifunge kiunoni, lakini usiutie ndani ya maji.”  Basi nikanunua mshipi kulingana na neno la Yehova nikajifunga kiunoni.  Na neno la Yehova likanijia mara ya pili likisema:  “Uchukue mshipi ulionunua ambao umejifunga, nawe uinuke na kwenda kwenye Mto Efrati, uufiche huko katika mpasuko wa jabali.”  Basi nikaenda, nikauficha kando ya Mto Efrati, kama Yehova alivyoniamuru.  Lakini baada ya siku nyingi Yehova akaniambia: “Inuka, nenda kwenye Mto Efrati, uchukue kutoka huko ule mshipi niliokuamuru uufiche huko.”  Basi nikaenda kwenye Mto Efrati, nikachimba na kuuchukua ule mshipi kutoka mahali nilipouficha, nami nikaona kwamba mshipi huo ulikuwa umeharibika; haukufaa kabisa.  Kisha neno la Yehova likanijia likisema:  “Yehova anasema hivi, ‘Hivyo ndivyo nitakavyokiharibu kiburi cha Yuda na kiburi kingi cha Yerusalemu.+ 10  Watu hawa waovu wanaokataa kutii maneno yangu,+ wanaofuata kwa ukaidi moyo wao wenyewe,+ na wanaofuata miungu mingine, wakiiabudu na kuiinamia, watakuwa kama mshipi huu usiofaa kabisa.’ 11  ‘Kwa maana kama vile mshipi unavyoshikamana na kiuno cha mtu, ndivyo nilivyowafanya watu wote wa nyumba ya Israeli na watu wote wa nyumba ya Yuda washikamane nami,’ asema Yehova, ‘ili wawe watu wangu,+ jina,+ sifa, na kitu maridadi kwangu. Lakini hawakutii.’+ 12  “Nawe unapaswa pia kuwapa ujumbe huu: ‘Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: “Kila mtungi mkubwa unapaswa kujazwa divai.”’ Nao watakujibu, ‘Je, tayari hatujui kwamba kila mtungi mkubwa unapaswa kujazwa divai?’ 13  Kisha uwaambie, ‘Yehova anasema hivi: “Tazama, ninawajaza ulevi wakaaji wote wa nchi hii,+ wafalme wanaoketi kwenye kiti cha ufalme cha Daudi, makuhani na manabii, na wakaaji wote wa Yerusalemu. 14  Nami nitawaponda kwa kuwagonganisha mtu na mwenzake, baba na wana pia,” asema Yehova.+ “Sitawahurumia wala kuwasikitikia kamwe wala kuwaonyesha rehema yoyote; hakuna kitakachonizuia nisiwaangamize.”’+ 15  Sikieni na mtege sikio. Msiwe na kiburi, kwa maana Yehova amesema. 16  Mtukuzeni Yehova Mungu wenuKabla hajaleta gizaNa kabla miguu yenu haijajikwaa kwenye milima jioni. Mtatumaini kupata nuru,Lakini ataleta kivuli kizito;Ataigeuza nuru iwe giza zito.+ 17  Nanyi mkikataa kusikiliza,Nitalia* kisiri kwa sababu ya kiburi chenu. Nitatoa machozi mengi, na macho yangu yatabubujika machozi,+Kwa sababu kondoo wa Yehova+ wamechukuliwa mateka. 18  Mwambie mfalme na mama malkia,+ ‘Ketini mahali pa chini,Kwa maana taji lenu maridadi litaanguka kutoka kwenye vichwa vyenu.’ 19  Majiji ya kusini yamefungwa,* na hakuna mtu wa kuyafungua. Watu wote wa Yuda wamepelekwa uhamishoni, wamepelekwa kabisa uhamishoni.+ 20  Inua macho yako uwaone wale wanaokuja kutoka kaskazini.+ Liko wapi kundi ulilopewa, kondoo wako maridadi?+ 21  Utasema nini adhabu yako itakapofikaKutoka kwa marafiki wako wa karibu uliowafundisha tangu mwanzo?+ Je, hutashikwa na uchungu wa kuzaa, kama wa mwanamke anayezaa?+ 22  Nawe ukijiuliza moyoni mwako, ‘Kwa nini nimepatwa na mambo haya?’+ Umevuliwa nguo yako kwa sababu ya kosa lako kubwa+Na visigino vyako vimetendewa kikatili. 23  Je, Mkushi* anaweza kuibadili ngozi yake, au chui madoa yake?+ Kama inawezekana, basi mnaweza kutenda mema,Ninyi mliozoezwa kutenda uovu. 24  Basi nitawatawanya kama nyasi kavu zinazopeperushwa na upepo wa jangwani.+ 25  Hii ndiyo kura yako, fungu nililokupimia,” asema Yehova,“Kwa sababu umenisahau+ nawe unautumaini uwongo.+ 26  Kwa hiyo, nitainua nguo yako juu ya uso wako,Na aibu yako itaonekana,+ 27  Matendo yako ya uzinzi+ na kilio chako cha uchu,Ukahaba wako uliopotoka.* Juu ya vilima, katika mashamba,Nimeyaona matendo yako yanayochukiza.+ Ole wako, Ee Yerusalemu! Utaendelea kuwa mchafu mpaka lini?”+

Maelezo ya Chini

Au “Nafsi yangu italia.”
Au “yamezingirwa.”
Au “Mwethiopia.”
Au “wa aibu.”