Yeremia 14:1-22

  • Ukame, njaa kali, na upanga (1-12)

  • Manabii wa uwongo washutumiwa (13-18)

  • Yeremia akiri dhambi za watu (19-22)

14  Hili ndilo neno la Yehova lililomjia Yeremia kuhusu ukame:+   Yuda inaomboleza,+ na malango yake yamefifia. Yamehuzunika na kuzama ardhini,Na kilio kinapanda juu kutoka Yerusalemu.   Na mabwana wao wanawatuma watumishi wao* walete maji. Wanaenda kwenye visima* lakini hawapati maji. Wanarudi vyombo vyao vikiwa vitupu. Wameaibika na kukata tamaa,Nao wanavifunika vichwa vyao.   Kwa sababu udongo umepasuka,Kwa maana hakuna mvua nchini,+Wakulima wametamauka na kuvifunika vichwa vyao.   Hata paa jike aliye porini anamwacha mtoto wake mchangaKwa sababu hakuna nyasi.   Punda wa mwituni wanasimama kwenye vilima vitupu. Wanahemahema kama mbwamwitu;Macho yao yanadhoofika kwa sababu hakuna majani.+   Ingawa makosa yetu yanatushtaki,Ee Yehova, tenda kwa ajili ya jina lako.+ Kwa maana matendo yetu ya ukosefu wa uaminifu ni mengi,+Nasi tumekutendea dhambi.   Ee tumaini la Israeli, Mwokozi wake+ wakati wa taabu,Kwa nini wewe ni kama mgeni nchini,Kama msafiri alalaye usiku mmoja tu?   Kwa nini wewe ni kama mtu anayeshangaa,Kama mwanamume mwenye nguvu asiyeweza kuokoa? Kwa maana uko miongoni mwetu, Ee Yehova,+Nasi tumeitwa kwa jina lako.+ Usituache. 10  Yehova anasema hivi kuhusu watu hawa: “Wanapenda kutangatanga;+ hawajaizuia miguu yao.+ Basi Yehova hafurahishwi nao.+ Sasa atalikumbuka kosa lao, naye atawaadhibu* kwa sababu ya dhambi zao.”+ 11  Kisha Yehova akaniambia: “Usisali kwamba watu hawa wapate mema.+ 12  Wanapofunga, sisikilizi sihi zao,+ na wanapotoa dhabihu nzima za kuteketezwa na matoleo ya nafaka, siyafurahii,+ kwa maana nitawaangamiza kwa upanga, kwa njaa kali, na kwa ugonjwa hatari.”+ 13  Ndipo nikasema: “Ole wangu, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova! Tazama, manabii wanawaambia, ‘Hamtaona upanga, wala hamtakumbwa na njaa kali, bali nitawapa amani ya kweli mahali hapa.’”+ 14  Kisha Yehova akaniambia: “Manabii wanatabiri uwongo katika jina langu.+ Sikuwatuma wala kuwaamuru wala kuzungumza nao.+ Wanawatabiria ninyi maono ya uwongo na uaguzi* usiofaa kitu na udanganyifu wa moyo wao wenyewe.+ 15  Kwa hiyo mimi Yehova ninasema hivi kuhusu manabii wanaotabiri katika jina langu ingawa sikuwatuma, na wanaosema hakuna upanga wala njaa kali itakayokuja katika nchi hii: ‘Manabii hao wataangamia kwa upanga na kwa njaa kali.+ 16  Na watu wanaotabiriwa mambo hayo watatupwa katika barabara za Yerusalemu kwa sababu ya njaa kali na upanga, na hakuna yeyote atakayewazika+—wao, wake zao, wana wao, au mabinti wao—kwa maana nitawamwagia msiba wanaostahili.’+ 17  “Unapaswa kuwaambia neno hili,‘Macho yangu na yabubujike machozi usiku na mchana, yasiishe,+Kwa maana bikira, binti ya watu wangu amepondwa kabisa na kuvunjwa,+Kwa jeraha baya sana. 18  Nikienda shambani na kutazama,Ninawaona wale waliouawa kwa upanga!+ Na nikiingia jijini,Ninayaona magonjwa yaliyoletwa na njaa kali!+ Kwa maana nabii na kuhani wamezunguka katika nchi wasiyoijua.’”+ 19  Je, umeikataa Yuda kabisa, au, je, umelichukia* Sayuni kabisa?+ Kwa nini umetupiga, hivi kwamba hatuwezi kupona?+ Tulitumaini kupata amani, lakini hakuna jambo lolote jema lililokuja,Wakati wa kuponywa, lakini kuna hofu!+ 20  Tunatambua uovu wetu, Ee Yehova,Na kosa la mababu zetu,Kwa maana tumekutendea dhambi.+ 21  Kwa ajili ya jina lako, usitukatae;+Usikidharau kiti chako cha ufalme chenye utukufu. Kumbuka, nawe usivunje agano lako pamoja nasi.+ 22  Je, kuna sanamu yoyote kati ya sanamu za ubatili za mataifa inayoweza kuleta mvua,Au, je, hata mbingu zinaweza kuleta mvua zenyewe? Je, si Wewe peke yako, Ee Yehova Mungu wetu?+ Nasi tunakutumaini,Kwa maana wewe peke yako ndiye uliyefanya mambo hayo yote.

Maelezo ya Chini

Au “walio wadogo nchini.”
Au “mitaro; matangi.”
Au “atawafanya wawajibike.”
Au “ubashiri.”
Au “nafsi yako imelichukia.”