Yeremia 15:1-21

  • Yehova hatabadili hukumu yake (1-9)

  • Yeremia alalamika (10)

  • Jibu la Yehova (11-14)

  • Sala ya Yeremia (15-18)

    • Apata furaha kwa kula maneno ya Mungu (16)

  • Yehova amtia nguvu Yeremia (19-21)

15  Kisha Yehova akaniambia: “Hata kama Musa na Samweli wangekuwa wamesimama mbele zangu,+ singewaonyesha kibali* watu hawa. Wafukuze kutoka mbele zangu. Waache waende.  Nao wakikuuliza, ‘Twende wapi?’ unapaswa kuwaambia, ‘Yehova anasema hivi: “Yeyote aliyekusudiwa kufa kwa ugonjwa unaoua, na afe kwa ugonjwa unaoua! Yeyote aliyekusudiwa kufa kwa upanga, na afe kwa upanga!+ Yeyote aliyekusudiwa kufa kwa njaa kali, na afe kwa njaa kali! Na yeyote aliyekusudiwa kwenda utekwani, na aende utekwani!”’+  “‘Nami nitawaletea misiba minne,’*+ asema Yehova, ‘upanga ili kuua, mbwa ili kukokota, na ndege wa angani na wanyama wa duniani ili kula na kuharibu.+  Nami nitawafanya wawe kitu cha kutisha kwa falme zote za dunia+ kwa sababu ya Manase mwana wa Hezekia, mfalme wa Yuda, kwa sababu ya mambo aliyofanya Yerusalemu.+   Ni nani atakayekuhurumia, Ee Yerusalemu,Ni nani atakayekusikitikia,Na ni nani atakayesimama ili kuuliza kuhusu hali yako?’   ‘Umeniacha mimi,’ asema Yehova.+ ‘Unaendelea kunigeuzia mgongo.*+ Basi nitaunyoosha mkono wangu dhidi yako na kukuangamiza.+ Nimechoka kukuhurumia.*   Nami nitawapepeta kwa uma kwenye malango ya nchi. Nitawaua watoto wao.+ Nitawaangamiza watu wangu,Kwa sababu wanakataa kuziacha njia zao.+   Wajane wao watakuwa wengi mbele zangu kuliko mchanga wa bahari. Nitaleta mwangamizaji dhidi yao wakati wa adhuhuri, dhidi ya akina mama na vijana. Nitawaletea wasiwasi na hofu kwa ghafla.   Mwanamke aliyezaa watoto saba amedhoofika;Anapumua* kwa shida. Jua lake limetua wakati bado ni mchana,Na kusababisha aibu na fedheha.’* ‘Na wachache waliobaki kati yaoNitawaacha waangamizwe kwa upanga na maadui wao,’ asema Yehova.”+ 10  Ole wangu, ewe mama yangu, kwa sababu ulinizaa,+Mtu anayegombana na kuzozana daima na nchi yote. Sijamkopesha mtu wala kukopeshwa;Lakini wote wananilaani. 11  Yehova alisema: “Kwa hakika nitakuhudumia ili upate mema;Kwa hakika nitakusaidia wakati wa msiba,Wakati wa taabu dhidi ya adui. 12  Je, kuna yeyote anayeweza kuvunja chuma vipandevipande,Chuma kutoka kaskazini, na shaba? 13  Nitatoa mali zako na hazina zako ili ziporwe,+Bila malipo, kwa sababu ya dhambi zako zote katika maeneo yako yote. 14  Nitawapatia maadui wenuWazipeleke katika nchi msiyoijua.+ Kwa maana moto umewashwa kwa hasira yangu. Nao unawaka dhidi yenu.”+ 15  Wewe unajua, Ee Yehova,Nikumbuke na unikazie fikira. Nilipizie kisasi wanaonitesa.+ Usiache niangamie* kwa sababu wewe hukasiriki upesi. Ujue kwamba ninabeba shutuma hii kwa sababu yako.+ 16  Maneno yako yalipatikana, nami nikayala;+Na neno lako likawa furaha na shangwe ya moyo wangu,Kwa maana nimeitwa kwa jina lako, Ee Yehova Mungu wa majeshi. 17  Siketi pamoja na watu wanaopenda raha na kushangilia.+ Kwa sababu mkono wako uko juu yangu, ninaketi peke yangu,Kwa maana umenijaza ghadhabu.*+ 18  Kwa nini maumivu yangu ni ya kudumu na jeraha langu haliponi? Linakataa kupona. Je, utakuwa kwangu kama chanzo cha maji cha udanganyifu,Ambacho hakiwezi kutegemeka? 19  Kwa hiyo Yehova anasema hivi: “Ukirudi, basi nitakurudisha,Nawe utasimama mbele zangu. Ikiwa utatenganisha kilicho na thamani kutoka kwa kisicho na thamani,Utakuwa kama kinywa changu mwenyewe.* Watalazimika kuja kwako,Lakini wewe hutaenda kwao.” 20  “Ninakufanya kuwa ukuta wa shaba wenye ngome kwa watu hawa.+ Kwa hakika watapigana nawe,Lakini hawatakushinda,+Kwa maana mimi niko pamoja nawe, ili nikuokoe na kukukomboa,” asema Yehova. 21  “Nami nitakuokoa kutoka mikononi mwa watu waovuNa kukukomboa kutoka mikononi mwa watu wakatili.”

Maelezo ya Chini

Au “nafsi yangu haingewaelekea.”
Au labda, “aina nne za hukumu.” Tnn., “familia nne.”
Au labda, “Unatembea ukirudi nyuma.”
Au “kughairi.”
Au labda, “Limeaibishwa na kufedheheshwa.”
Au “Nafsi yake inapumua.”
Tnn., “Usiniondolee mbali.”
Au “ujumbe wa shutuma.”
Au “utakuwa msemaji wangu.”