Yeremia 16:1-21

  • Yeremia hapaswi kuoa, kuomboleza, wala kusherehekea (1-9)

  • Adhabu, kisha kurudishwa (10-21)

16  Na neno la Yehova likanijia tena, likisema:  “Usioe mke, wala usiwe na wana na mabinti mahali hapa.  Kwa maana Yehova anasema hivi kuhusu wana na mabinti wanaozaliwa hapa na kuhusu mama zao wanaowazaa na kuhusu baba zao wanaowazaa katika nchi hii:  ‘Watakufa kwa magonjwa hatari,+ lakini hakuna atakayewaombolezea wala kuwazika; watakuwa kama mbolea kwenye ardhi.+ Wataangamia kwa upanga na kwa njaa kali,+ na maiti zao zitakuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa duniani.’   “Kwa maana Yehova anasema hivi: ‘Usiingie katika nyumba ambamo waombolezaji wanafanya karamu,Wala usiende kuomboleza au kuwapa pole,’+ ‘Kwa maana nimewaondolea watu hawa amani yangu,’ asema Yehova,‘Pamoja na upendo wangu mshikamanifu na rehema.+   Wakubwa kwa wadogo watakufa katika nchi hii. Hawatazikwa,Hakuna mtu atakayewaombolezea,Wala hakuna mtu atakayejikatakata wala kujitia upara kwa ajili yao.*   Na hakuna mtu atakayewapa chakula wale wanaoomboleza,Ili kuwafariji baada ya kufiwa;Wala hakuna yeyote atakayewapa kikombe cha farajaIli wanywe kwa sababu ya kumpoteza baba yao au mama yao.   Nawe usiingie katika nyumba ya karamuKuketi pamoja nao ili kula na kunywa.’  “Kwa maana Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Mahali hapa, katika siku zenu na mbele ya macho yenu wenyewe, nitazikomesha sauti za furaha na shangwe, sauti ya bwana harusi na sauti ya bibi harusi.’+ 10  “Utakapowaambia watu hawa maneno haya yote, watakuuliza, ‘Kwa nini Yehova amesema kwamba tutapatwa na msiba wote huu mkubwa? Tumemtendea Yehova Mungu wetu kosa gani na dhambi gani?’+ 11  Utawajibu, ‘“Kwa sababu mababu zenu waliniacha,”+ asema Yehova, “nao waliendelea kuifuata miungu mingine na kuiabudu na kuiinamia.+ Lakini waliniacha mimi, nao hawakuishika sheria yangu.+ 12  Nanyi mmetenda mambo mabaya zaidi kuliko mababu zenu,+ na kila mmoja wenu anaufuata ukaidi wa moyo wake mwovu badala ya kunitii.+ 13  Basi nitawatupa nje ya nchi hii mpaka kwenye nchi ambayo wala ninyi wala mababu zenu hawakuijua,+ na huko mtalazimika kuiabudu miungu mingine mchana na usiku,+ kwa sababu sitawaonyesha kibali.”’ 14  “‘Hata hivyo, siku zinakuja,’ asema Yehova, ‘wakati ambapo hawatasema tena: “Kwa hakika kama Yehova anavyoishi, aliyewatoa watu wa Israeli nchini Misri!”+ 15  badala yake watasema: “Kwa hakika kama Yehova anavyoishi, aliyewatoa watu wa Israeli katika nchi ya kaskazini na katika nchi zote ambako alikuwa amewatawanya!” nami nitawarudisha katika nchi yao, niliyowapa mababu zao.’+ 16  ‘Tazama, ninawaita wavuvi wengi,’ asema Yehova,‘Nao watawavua. Na baada ya hapo nitawaita wawindaji wengi,Nao watawawinda kwenye kila mlima na kila kilimaNa kutoka kwenye mipasuko ya majabali. 17  Kwa maana macho yangu yanaona kila kitu wanachofanya.* Hawajafichwa kutoka mbele zangu,Wala kosa lao halijafichwa kutoka mbele ya macho yangu. 18  Kwanza, nitalipa kiwango kamili kinachostahili kosa lao na dhambi yao,+ Kwa maana wameitia unajisi nchi yangu kwa mifano isiyo hai ya* sanamu zao zinazochukizaNao wameujaza urithi wangu mambo yao yanayochukiza.’”+ 19  Ee Yehova, nguvu zangu na ngome yangu,Kimbilio langu katika siku ya taabu,+Mataifa yatakuja kwako kutoka kwenye miisho ya dunia,Nayo yatasema: “Mababu zetu walirithi uwongo mtupu,Ubatili na vitu visivyofaa kitu ambavyo havina faida yoyote.”+ 20  Je, mwanadamu anaweza kujitengenezea miunguWakati kwa kweli hiyo si miungu?+ 21  “Basi nitawafanya wajue,Wakati huu nitawafanya wajue nguvu zangu na uwezo wangu,Nao watalazimika kujua kwamba jina langu ni Yehova.”

Maelezo ya Chini

Desturi za kipagani za kuomboleza ambazo inaelekea zilifanywa katika nchi ya Israeli iliyoasi imani.
Au “yanatazama njia zao zote.”
Tnn., “maiti za.”