Yeremia 17:1-27

  • Dhambi ya Yuda imetia mizizi (1-4)

  • Baraka za kumtumaini Yehova (5-8)

  • Moyo wenye hila (9-11)

  • Yehova, tumaini la Israeli (12, 13)

  • Sala ya Yeremia (14-18)

  • Kuishika Sabato ikiwa siku takatifu (19-27)

17  “Dhambi ya Yuda imeandikwa kwa kalamu ya chuma. Imechongwa kwa ncha ya almasi juu ya bamba la moyo waoNa juu ya pembe za madhabahu zao,   Huku wana wao wakikumbuka madhabahu zao na miti yao mitakatifu*+Kando ya mti wenye majani mengi, juu ya vilima virefu,+   Juu ya milima katika maeneo yaliyo wazi ya mashambani. Mali zako, hazina zako zote, nitazitoa ili ziporwe+—Naam, mahali pako pa juu kwa sababu ya dhambi katika maeneo yako yote.+   Utauacha kwa kupenda urithi wako niliokupa.+ Nami nitakufanya uwatumikie maadui wako katika nchi usiyoijua,+Kwa maana umeiwasha hasira yangu kama moto.*+ Itaendelea kuwaka daima.”   Yehova anasema hivi: “Amelaaniwa mtu* anayewatumaini wanadamu,+Anayetegemea nguvu za wanadamu,*+Na ambaye moyo wake unamwacha Yehova.   Atakuwa kama mti ulio peke yake jangwani. Hataona mema yatakapokuja,Lakini atakaa mahali pakavu nyikani,Katika nchi yenye chumvi ambayo hakuna mtu anayeweza kuishi ndani yake.   Amebarikiwa mtu* anayemtumaini Yehova,Ambaye uhakika wake uko katika Yehova.+   Atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji,Unaopeleka mizizi yake kwenye kijito. Hatatambua joto linapokuja,Bali majani yake yatasitawi sikuzote.+ Naye hatakuwa na mahangaiko katika mwaka wa ukame,Wala hataacha kuzaa matunda.   Moyo ni wenye hila* kuliko kitu kingine chochote nao ni hatari.*+ Ni nani anayeweza kuujua? 10  Mimi, Yehova, ninauchunguza moyo,+Ninakagua mawazo ya ndani kabisa,*Ili kumpa kila mmoja kulingana na njia zake,Kulingana na matunda ya matendo yake.+ 11  Kama kwale anayekusanya kile ambacho hakutaga,Ndivyo alivyo mtu anayekusanya utajiri kwa udanganyifu.*+ Atauacha katikati ya maisha yake,Na mwishowe ataonekana hana akili.” 12  Kiti cha ufalme chenye utukufu, kilichokwezwa tangu mwanzo,Ndicho mahali petu patakatifu.+ 13  Ee Yehova, tumaini la Israeli,Wote wanaokuacha wataaibishwa. Wale wanaokuasi* wataandikwa mavumbini,+Kwa sababu wamemwacha Yehova, chanzo cha maji yaliyo hai.+ 14  Niponye, Ee Yehova, nami nitapona. Niokoe, nami nitaokoka,+Kwa maana ninakusifu wewe. 15  Tazama! Kuna wale wanaoniambia: “Neno la Yehova liko wapi?+ Na lije, tafadhali!” 16  Lakini mimi, sikukimbia na kuacha kukufuata ukiwa mchungaji,Wala sikutamani siku ya msiba. Unajua vema mambo yote ambayo midomo yangu imesema;Yote yalitendeka mbele za uso wako! 17  Usiwe tisho kwangu. Wewe ni kimbilio langu katika siku ya msiba. 18  Wale wanaonitesa na waaibishwe,+Lakini usiruhusu niaibishwe. Waache washikwe na hofu,Lakini usiruhusu nishikwe na hofu. Ilete siku ya msiba juu yao,+Nawe uwaponde na kuwaangamiza kabisa.* 19  Yehova aliniambia hivi: “Nenda usimame katika lango la wana wa watu ambalo wafalme wa Yuda huingilia na kutokea, na katika malango yote ya Yerusalemu.+ 20  Nawe unapaswa kuwaambia hivi: ‘Sikieni neno la Yehova, ninyi wafalme wa Yuda, watu wote wa Yuda, na wakaaji wote wa Yerusalemu, mnaoingia kupitia malango haya. 21  Yehova anasema hivi: “Jihadharini, nanyi msibebe mzigo wowote siku ya Sabato wala kuuingiza kupitia malango ya Yerusalemu.+ 22  Hampaswi kutoa mzigo wowote katika nyumba zenu siku ya Sabato; nanyi hampaswi kufanya kazi yoyote.+ Endeleeni kuishika siku ya Sabato ikiwa siku takatifu, kama nilivyowaamuru mababu zenu.+ 23  Lakini hawakusikiliza wala kutega sikio lao, nao wakakataa kwa ukaidi* kutii au kukubali nidhamu.”’+ 24  “‘“Hata hivyo, mkinitii kabisa,” asema Yehova, “nanyi msiingize mzigo wowote kupitia malango ya jiji hili siku ya Sabato, nanyi mwendelee kuishika siku ya Sabato ikiwa siku takatifu kwa kutofanya kazi yoyote siku hiyo,+ 25  ndipo wafalme na wakuu wanaoketi kwenye kiti cha ufalme cha Daudi+ wataingia pia kupitia malango ya jiji hili, wakipanda gari na farasi, wao pamoja na wakuu wao, watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalemu;+ na jiji hili litaendelea kuwa na watu daima. 26  Na watu watakuja kutoka katika majiji ya Yuda, kutoka maeneo yanayozunguka Yerusalemu, kutoka nchi ya Benjamini,+ maeneo ya chini,+ kutoka eneo lenye milima, na kutoka Negebu;* wataleta dhabihu nzima za kuteketezwa,+ dhabihu nyingine,+ matoleo ya nafaka,+ ubani, na dhabihu za shukrani ndani ya nyumba ya Yehova.+ 27  “‘“Lakini msiponitii kwa kutoshika siku ya Sabato ikiwa siku takatifu na mkibeba mizigo na kuileta kupitia malango ya Yerusalemu katika siku ya Sabato, nitayawasha moto malango yake, nao hakika utaiteketeza minara yenye ngome ya Yerusalemu+ nao hautazimwa.”’”+

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Au labda, “Kwa hasira yangu umewashwa kama moto.”
Au “mtu mwenye nguvu.”
Tnn., “Anayefanya mwili wa nyama kuwa mkono wake.”
Au “mtu mwenye nguvu.”
Au “ ni mdanganyifu.”
Au labda, “hauwezi kuponywa.”
Au “hisia za ndani kabisa.” Tnn., “figo.”
Au “lakini si kwa haki.”
Tnn., “wanaoniasi,” inaelekea wanamwasi Yehova.
Au “uwaangamize mara mbili zaidi.”
Tnn., “wakazifanya shingo zao kuwa ngumu.”
Au “kusini.”