Yeremia 18:1-23

  • Udongo mikononi mwa mfinyanzi (1-12)

  • Yehova awageuzia Israeli mgongo (13-17)

  • Njama dhidi ya Yeremia; ombi lake (18-23)

18  Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Yehova:  “Inuka na ushuke mpaka kwenye nyumba ya mfinyanzi,+ na huko nitakuambia maneno yangu.”  Basi nikashuka mpaka kwenye nyumba ya mfinyanzi, naye alikuwa akifanya kazi kwenye magurudumu ya mfinyanzi.  Lakini chombo alichokuwa akitengeneza kikaharibika mikononi mwake. Basi mfinyanzi akakitengeneza upya kuwa chombo kingine, kama alivyopenda.*  Kisha neno la Yehova likanijia likisema:  “‘Je, siwezi kuwatendea kama mfinyanzi huyu alivyotenda, enyi watu wa nyumba ya Israeli?’ asema Yehova. ‘Tazama! Kama udongo mikononi mwa mfinyanzi, ndivyo mlivyo mikononi mwangu, enyi watu wa nyumba ya Israeli.+  Wakati wowote nitakaposema kuhusu kung’oa na kubomoa na kuharibu taifa au ufalme,+  na taifa hilo liache uovu wake niliotangaza dhidi yake, mimi pia nitabadili nia yangu* kuhusu msiba niliokusudia kuuleta dhidi yake.+  Lakini wakati wowote ninaposema kuhusu kujenga na kupanda taifa au ufalme, 10  na taifa hilo litende maovu machoni pangu na kukosa kuitii sauti yangu, mimi pia nitabadili nia yangu* kuhusu mema niliyokusudia kulitendea.’ 11  “Sasa, tafadhali, waambie watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalemu, ‘Yehova anasema hivi: “Ninatayarisha* msiba na kupanga njama dhidi yenu. Geukeni, tafadhali, kutoka kwenye njia zenu mbaya, na mrekebishe njia zenu na matendo yenu.”’”+ 12  Lakini wakasema: “Hakuna tumaini lolote!+ Kwa maana tutafuata mawazo yetu wenyewe, na kila mmoja wetu atatenda kulingana na ukaidi wa moyo wake mwovu.”+ 13  Kwa hiyo Yehova anasema hivi: “Ulizeni wenyewe, tafadhali, kati ya mataifa. Ni nani amesikia jambo kama hili? Bikira wa Israeli ametenda jambo linalochukiza sana.+ 14  Je, theluji ya Lebanoni inatoweka kwenye miamba iliyo kwenye miteremko yake? Au, je, maji baridi yanayotiririka kutoka mbali yatakauka? 15  Lakini watu wangu wamenisahau.+ Kwa maana wanakitolea dhabihu* kitu cha ubatili,+Nao wanawafanya watu wajikwae katika njia zao, vijia vya kale,+Ili wapite kwenye barabara za vichochoroni ambazo hazijasawazishwa na ambazo si tambarare,* 16  Ili kuifanya nchi yao kuwa kitu cha kutisha+Na kitu cha kupigiwa mluzi milele.+ Kila mtu atakayepita kando yake atatazama kwa mshtuko na kutikisa kichwa chake.+ 17  Kama upepo wa mashariki, nitawatawanya mbele ya adui. Nitawaonyesha mgongo, si uso wangu, siku ya msiba wao.”+ 18  Nao wakasema: “Njooni, tupange njama dhidi ya Yeremia,+ kwa maana sheria haitatoweka* kutoka kwa makuhani wetu au shauri kutoka kwa watu wenye hekima au neno kutoka kwa manabii. Njooni tumshambulie kwa maneno,* nasi tusisikilize anachosema.” 19  Nitegee sikio, Ee Yehova,Nawe usikilize wanachosema wapinzani wangu. 20  Je, wema unapaswa kulipwa kwa uovu? Kwa maana wameuchimbia shimo uhai wangu.*+ Kumbuka jinsi nilivyosimama mbele zako ili kusema mema kuwahusu,Ili kuwaondolea ghadhabu yako. 21  Basi waache wana wao wapatwe na njaa kali,Na uwatie mikononi mwa nguvu za upanga.+ Wake zao na wafiwe na watoto na kuwa wajane.+ Wanaume wao na wauawe kwa ugonjwa unaoua,Vijana wao wauawe kwa upanga vitani.+ 22  Kilio na kisikiwe kutoka katika nyumba zaoUtakapowaletea wavamizi kwa ghafla. Kwa maana wamechimba shimo ili kunikamataNao wametega mitego ya kuinasa miguu yangu.+ 23  Lakini wewe, Ee Yehova,Unajua vema njama zao zote za kuniua.+ Usilifunike kosa lao,Wala usiifute dhambi yao kutoka mbele zako. Na wakwazike mbele zako+Utakapowachukulia hatua kwa hasira yako.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “kama ilivyokuwa sawa machoni pa mfinyanzi kukitengeneza.”
Au “nitaghairi.”
Au “nitaghairi.”
Tnn., “ninatengeneza.”
Au “ambazo hazijatengenezwa.”
Au “moshi wa dhabihu.”
Tnn., “tumpige kwa ulimi.”
Au “mafundisho hayatatoweka.”
Au “wameichimbia shimo nafsi yangu.”