Yeremia 2:1-37

  • Waisraeli wamwacha Yehova na kuanza kuabudu miungu mingine (1-37)

    • Israeli ni kama mzabibu wa kigeni (21)

    • Pindo za nguo zake zina madoa ya damu (34)

2  Neno la Yehova likanijia, likisema:  “Nenda ukatangaze masikioni mwa watu wa Yerusalemu, ‘Yehova anasema hivi: “Ninakumbuka vema bidii yako* ulipokuwa kijana,+Upendo ulioonyesha ulipochumbiwa ili kuolewa,+Jinsi ulivyonifuata nyikani,Katika nchi ambayo haipandwi mbegu.+   Israeli alikuwa mtakatifu kwa Yehova,+ mavuno ya kwanza ya mazao yake.”’ ‘Yeyote aliyemrarua alikuwa na hatia. Msiba ulimpata,’ asema Yehova.”+   Sikieni neno la Yehova, enyi watu wa nyumba ya Yakobo,Nanyi familia zote za nyumba ya Israeli.   Yehova anasema hivi: “Mababu zenu waliona kosa gani kwangu,+Hivi kwamba wakatangatanga mbali sana nami,Wakazifuata sanamu za ubatili,+ nao wenyewe wakawa ubatili?+   Hawakuuliza, ‘Yehova yuko wapi,Yule aliyetutoa nchini Misri,+Aliyetuongoza kupitia nyikani,Kupitia nchi yenye majangwa+ na mashimo,Kupitia nchi yenye ukame+ na kivuli kizito,Kupitia nchi ambayo hakuna mtu anayesafiri humoNa ambamo hakuna mwanadamu anayeishi?’   Kisha nikawaleta ninyi katika nchi yenye mashamba ya matunda,Ili mle matunda yake na vitu vyake vyema.+ Lakini mliingia humo na kuitia unajisi nchi yangu;Mkaufanya urithi wangu kuwa kitu kinachochukiza.+   Makuhani hawakuuliza, ‘Yehova yuko wapi?’+ Wale wanaoshughulika na Sheria hawakunijua,Wachungaji waliniasi,+Manabii walitabiri kupitia Baali,+Nao wakawafuata wale ambao hawangewafaidi hata kidogo.   ‘Basi nitapambana zaidi nanyi,’+ asema Yehova,‘Nami nitapambana na wana wa wana wenu.’ 10  ‘Lakini vukeni mpaka nchi za pwani za* Kitimu+ mwone. Naam, tumeni watu Kedari+ nanyi mfikirie kwa uangalifu;Mwone ikiwa jambo kama hili limewahi kutendeka. 11  Je, taifa limewahi kubadili miungu yake kwa ajili ya miungu ambayo si miungu? Lakini watu wangu mwenyewe wamebadili utukufu wangu kwa ajili ya kitu kisicho na maana.+ 12  Tazameni jambo hili kwa mshangao, enyi mbingu;Tetemekeni kwa hofu kubwa,’ asema Yehova, 13  ‘Kwa sababu watu wangu wamefanya mambo mawili mabaya: Wameniacha mimi, chemchemi ya maji yaliyo hai,+Na kujichimbia* matangi ya maji,Matangi yaliyovunjika, ambayo hayawezi kuhifadhi maji.’ 14  ‘Je, Israeli ni mtumishi, au ni mtumwa aliyezaliwa nyumbani? Basi kwa nini amekuwa kitu cha kuporwa? 15  Wanasimba* wananguruma dhidi yake;+Wameinua sauti zao. Waliifanya nchi yake kuwa kitu cha kutisha. Majiji yake yameteketezwa, hivi kwamba hakuna mkaaji. 16  Watu wa Nofu*+ na Tahpanesi+ wanakula utosi wa kichwa chako. 17  Je, hukujiletea jambo hiloKwa kumwacha Yehova Mungu wako+Alipokuwa akikuongoza njiani? 18  Sasa kwa nini unatamani njia ya kwenda Misri+Ili kunywa maji ya Shihori?* Kwa nini unatamani njia ya kwenda Ashuru+Ili kunywa maji ya ule Mto?* 19  Uovu wako unapaswa kukurekebisha,Na ukosefu wako wa uaminifu unapaswa kukukaripia. Jua na utambue ubaya na uchungu+ waKumwacha Yehova Mungu wako;Hujaniogopa,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi. 20  ‘Kwa maana zamani niliivunja nira yako+Na kuzikata pingu zako. Lakini ulisema: “Mimi sitatumikia,” Kwa maana juu ya kila kilima kirefu na chini ya kila mti wenye majani mengi+Ulilala ukiwa umejinyoosha, ukifanya ukahaba.+ 21  Nilikupanda kama mzabibu bora mwekundu,+ wote ukiwa mbegu safi;Basi umebadilikaje na kuwa machipukizi yaliyoharibika ya mzabibu wa kigeni mbele zangu?’+ 22  ‘Hata ukioga kwa magadi na kutumia sabuni nyingi,Bado hatia yako itakuwa doa mbele zangu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. 23  Unawezaje kusema, ‘Sijajichafua. Sijafuata Mabaali? Angalia njia yako bondeni. Fikiria ulichofanya. Wewe ni kama ngamia jike mchanga anayekimbia kasi,Anayekimbia huku na huku bila mwelekeo katika njia zake, 24  Punda wa mwituni aliyezoea nyika,Anayenusa upepo katika tamaa yake.* Ni nani anayeweza kumzuia anaposhikwa na nyege? Hakuna yeyote kati ya wale wanaomtafuta atakayelazimika kujichosha. Watampata katika majira yake.* 25  Izuie miguu yako isitembee bila viatuNa koo lako lisiwe na kiu. Lakini ulisema, ‘Hakuna tumaini lolote!+ Hakuna! Nimewapenda wageni,*+Nami nitawafuata.’+ 26  Kama aibu ya mwizi anapokamatwa,Ndivyo watu wa nyumba ya Israeli walivyoaibishwa,Wao, wafalme wao na wakuu wao,Makuhani wao na manabii wao.+ 27  Wanauambia mti, ‘Wewe ni baba yangu,’+ Na jiwe, ‘Wewe ulinizaa.’ Lakini wamenigeuzia mimi mgongo wao badala ya uso wao.+ Watakapopatwa na msiba watasema,‘Simama utuokoe!’+ 28  Sasa iko wapi miungu yako uliyojitengenezea?+ Na isimame ikiwa inaweza kukuokoa unapopatwa na msiba. Kwa maana miungu yako imekuwa mingi kama majiji yako, Ee Yuda.+ 29  ‘Kwa nini unaendelea kushindana nami? Kwa nini nyote mmeniasi?’+ asema Yehova. 30  Nimewapiga wana wenu bila matokeo.+ Hawakukubali nidhamu yoyote;+Upanga wenu wenyewe uliwaangamiza manabii wenu,+Kama simba anayeshambulia. 31  Enyi kizazi hiki, fikirieni wenyewe neno la Yehova. Je, nimekuwa kama nyika kwa IsraeliAu nchi yenye giza linalokandamiza? Kwa nini watu hawa, watu wangu, wamesema, ‘Tunazurura kwa uhuru. Hatutakuja kwako tena’?+ 32  Je, bikira anaweza kuyasahau mapambo yake,Na bibi harusi mavazi yake ya kifuani?* Lakini watu wangu wamenisahau mimi kwa siku zisizohesabika.+ 33  Ewe mwanamke, jinsi unavyotayarisha njia yako kwa ustadi ili kutafuta upendo! Umejizoeza katika njia za uovu.+ 34  Hata pindo za nguo zako zina madoa ya damu ya maskini* wasio na hatia,+Ingawa sikuwapata wakivunja ili kuingia;Imejaa kwenye pindo zako zote.+ 35  Lakini unasema, ‘Sina hatia. Hakika hasira yake imeniondokea.’ Sasa ninaleta hukumu dhidi yakoKwa sababu unasema, ‘Sijatenda dhambi.’ 36  Kwa nini unaiona njia yako isiyo thabiti kuwa jambo dogo? Utaona aibu kwa sababu ya Misri pia,+Kama vile ulivyoona aibu kwa sababu ya Ashuru.+ 37  Kwa sababu hiyo pia utatoka mikono yako ikiwa juu ya kichwa chako,+Kwa maana Yehova amewakataa wale unaowategemea;Hawatakuletea mafanikio.”

Maelezo ya Chini

Au “upendo wako mshikamanifu.”
Au “visiwa vya.”
Au “kuchonga,” inaelekea kwenye mwamba.
Au “Wanasimba wenye manyoya marefu shingoni.”
Au “Memfisi.”
Yaani, Mto Efrati.
Yaani, kijito cha Mto Nile.
Au “katika tamaa ya nafsi yake.”
Tnn., “mwezi wake.”
Au “Nimeipenda miungu ya kigeni.”
Au “ukumbuu wake wa harusi?”
Au “nafsi za maskini.”