Yeremia 21:1-14

  • Yehova akataa ombi la Sedekia (1-7)

  • Watu kuchagua uzima au kifo (8-14)

21  Yeremia alipokea neno kutoka kwa Yehova wakati Mfalme Sedekia+ alipomtuma kwake Pashuri+ mwana wa Malkiya na Sefania+ mwana wa Maaseya, kuhani, akiomba hivi:  “Tafadhali mwombe Yehova ushauri kwa ajili yetu, kwa sababu Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni anapigana vita dhidi yetu.+ Labda Yehova atatutendea mojawapo ya matendo yake yanayostaajabisha, ili mfalme huyo atuache na kwenda zake.”+  Yeremia akawaambia, “Mwambieni Sedekia hivi:  ‘Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: “Tazama, ninazigeuza dhidi yenu* silaha za vita zilizo mikononi mwenu, mnazotumia kupigana na mfalme wa Babiloni+ na Wakaldayo wanaowazingira nje ya ukuta. Nami nitawakusanya katikati ya jiji hili.  Na mimi mwenyewe nitapigana nanyi+ kwa mkono ulionyooshwa na kwa mkono wenye nguvu, kwa hasira na kwa ghadhabu na kwa ukali mwingi.+  Nitawapiga wakaaji wa jiji hili, mwanadamu na mnyama pia. Watakufa kwa ugonjwa hatari sana.”’+  “‘“Baada ya hayo,” asema Yehova, “Nitamtia Mfalme Sedekia wa Yuda na watumishi wake na watu wa jiji hili—wale watakaookoka ugonjwa hatari, upanga, na njaa kali—mikononi mwa Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni, mikononi mwa maadui wao na mikononi mwa wale wanaotaka kuwaua.*+ Atawaua kwa upanga. Hatawasikitikia wala kuwahurumia wala kuwaonyesha rehema yoyote.”’+  “Nawe utawaambia watu hawa, ‘Yehova anasema hivi: “Tazameni, ninaweka mbele yenu njia ya uzima na njia ya kifo.  Wale watakaobaki katika jiji hili watakufa kwa upanga, kwa njaa kali, na kwa ugonjwa hatari. Lakini yeyote atakayetoka na kujisalimisha kwa Wakaldayo wanaowazingira ataendelea kuishi, naye atapata uhai wake* kama nyara.”’*+ 10  “‘“Kwa maana nimelikataa* jiji hili nalo litapata msiba wala si mema,”+ asema Yehova. “Litatiwa mikononi mwa mfalme wa Babiloni,+ naye ataliteketeza kwa moto.”+ 11  “‘Utawaambia watu wa nyumba ya mfalme wa Yuda: Sikieni neno la Yehova. 12  Enyi watu wa nyumba ya Daudi, Yehova anasema hivi: “Tekelezeni haki kila asubuhi,Na mtu anayenyang’anywa, mwokoeni kutoka mikononi mwa mtu laghai,+Ili ghadhabu yangu isiwake kama moto+Na kuteketeza bila mtu wa kuuzimaKwa sababu ya matendo yenu maovu.”’+ 13  ‘Tazama, niko dhidi yako, ewe mkaaji wa bondeni,*Ewe mwamba wa nchi tambarare,’ asema Yehova. ‘Na wewe unayeuliza: “Ni nani atakayeshuka kupigana nasi? Na ni nani atakayevamia makao yetu?” 14  Nitakufanya uwajibike*Kulingana na matendo yenu,’+ asema Yehova. ‘Nami nitawasha moto katika msitu wake,Nao utateketeza vitu vyote vinavyomzunguka.’”+

Maelezo ya Chini

Tnn., “Nebukadreza,” njia nyingine ya kuandika jina hili.
Au “ninawageuzia.”
Au “wanaotafuta nafsi yao.”
Tnn., “Nebukadreza,” njia nyingine ya kuandika jina hili.
Au “nafsi yake.”
Au “ataponyoka na uhai wake.”
Tnn., “nimeukaza uso wangu dhidi ya.”
Au “nchi tambarare ya chini.”
Au “Nitakuadhibu.”