Yeremia 23:1-40

  • Wachungaji wazuri na wabaya (1-4)

  • Usalama chini ya “chipukizi adilifu” (5-8)

  • Manabii wa uwongo washutumiwa (9-32)

  • “Mzigo” wa Yehova (33-40)

23  “Ole wao wachungaji wanaowaangamiza na kuwatawanya kondoo wa malisho yangu!” asema Yehova.+  Kwa hiyo Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi dhidi ya wachungaji wanaowachunga watu wangu: “Mmewatawanya kondoo wangu; mliendelea kuwatawanya, nanyi hamjawakazia fikira.”+ “Basi nitawakazia ninyi fikira kwa sababu ya matendo yenu maovu,” asema Yehova.  “Kisha nitawakusanya kondoo wangu waliobaki kutoka katika nchi zote ambako nilikuwa nimewatawanya,+ nami nitawarudisha kwenye malisho yao,+ nao watazaana na kuwa wengi.+  Nami nitaweka wachungaji juu yao ambao kwa kweli watawachunga.+ Hawataogopa tena wala kuwa na hofu, na hakuna yeyote atakayekosekana,” asema Yehova.  “Tazameni! Siku zinakuja,” asema Yehova, “nitakapomwinulia Daudi chipukizi adilifu.*+ Na mfalme atatawala+ na kuwa na ufahamu na kutekeleza haki na uadilifu katika nchi.+  Katika siku zake Yuda ataokolewa,+ na Israeli atakaa kwa usalama.+ Naye ataitwa jina hili: Yehova Ni Uadilifu Wetu.”+  “Hata hivyo, siku zinakuja,” asema Yehova, “wakati ambapo hawatasema tena, ‘Kwa hakika kama Yehova anavyoishi, aliyewatoa watu wa Israeli nchini Misri!’+  badala yake watasema, ‘Kwa hakika kama Yehova anavyoishi, aliyewatoa na kuwarudisha wazao wa nyumba ya Israeli kutoka katika nchi ya kaskazini na kutoka katika nchi zote nilizowatawanya,’ nao watakaa katika nchi yao wenyewe.”+  Kuhusu manabii: Moyo wangu umevunjika ndani yangu. Mifupa yangu yote inatetemeka. Mimi ni kama mtu aliyelewaNa kama mtu aliyelemewa na divai,Kwa sababu ya Yehova na kwa sababu ya maneno yake matakatifu. 10  Kwa maana nchi imejaa wazinzi;+Kwa sababu ya laana nchi inaomboleza+Na malisho ya nyikani yamekauka.+ Njia yao ni ya uovu, nao wanatumia vibaya nguvu zao. 11  “Nabii pamoja na kuhani wamechafuliwa.*+ Hata katika nyumba yangu mwenyewe nimeupata uovu wao,”+ asema Yehova. 12  “Basi kijia chao kitakuwa na utelezi na giza,+Watasukumwa na kuanguka. Kwa maana nitawaletea msibaKatika mwaka wa kuwaadhibu,” asema Yehova. 13  “Na kwa manabii wa Samaria+ nimeona jambo linalochukiza sana. Unabii wao unachochewa na Baali,Nao wanawapotosha watu wangu Waisraeli. 14  Na kwa manabii wa Yerusalemu nimeona mambo mabaya sana. Wanafanya uzinzi+ na kutembea katika uwongo;+Wanawatia moyo* watenda maovu,Nao hawageuki na kuuacha uovu wao. Wote ni kama Sodoma kwangu,+Na wakaaji wake ni kama Gomora.”+ 15  Kwa hiyo Yehova wa majeshi anasema hivi dhidi ya manabii hao: “Tazama, ninawafanya wale pakangaNa kuwapa maji yenye sumu wanywe.+ Kwa maana kutoka kwa manabii wa Yerusalemu uasi imani umeenea katika nchi yote.” 16  Yehova wa majeshi anasema hivi: “Msiyasikilize maneno ya manabii wanaowatabiria ninyi.+ Wanawadanganya.* Wanasema maono ya moyo wao wenyewe,+Si kutoka katika kinywa cha Yehova.+ 17  Wanawaambia tena na tena wale wasioniheshimu,‘Yehova amesema hivi: “Mtakuwa na amani.”’+ Nao wanamwambia kila mtu anayefuata moyo wake mkaidi,‘Hutapatwa na msiba wowote.’+ 18  Kwa maana ni nani amesimama katika kikundi cha marafiki wa karibu wa YehovaIli aone na kulisikia neno lake? Ni nani amelikazia fikira neno lake ili alisikie? 19  Tazameni! Dhoruba ya upepo ya Yehova italipuka kwa ghadhabu;Kama tufani inayozunguka, itazunguka ikishuka juu ya kichwa cha waovu.+ 20  Hasira ya Yehova haitapoaMpaka atakapotekeleza na kutimiza makusudi ya moyo wake. Mtaelewa jambo hilo waziwazi katika siku za mwisho. 21  Sikuwatuma manabii, lakini walikimbia. Sikuongea nao, lakini walitabiri.+ 22  Lakini ikiwa wangesimama katika kikundi changu cha marafiki wa karibu,Wangewafanya watu wangu wayasikie maneno yanguNao wangewarudisha kutoka kwenye njia yao mbaya na matendo yao maovu.”+ 23  “Je, mimi ni Mungu nikiwa karibu tu,” auliza Yehova, “ na si Mungu nikiwa mbali pia?” 24  “Je, mtu yeyote anaweza kujificha mahali pa siri ambapo siwezi kumwona?”+ auliza Yehova. “Je, mimi sizijazi mbingu na dunia?”+ auliza Yehova. 25  “Nimewasikia manabii wanaotabiri uwongo katika jina langu wakisema, ‘Niliota ndoto! Niliota ndoto!’+ 26  Jambo hili litaendelea mpaka lini katika moyo wa manabii hao, kutabiri uwongo? Wao ni manabii wa udanganyifu wa moyo wao wenyewe.+ 27  Wanakusudia kuwafanya watu wangu walisahau jina langu kupitia ndoto wanazosimuliana, kama baba zao walivyolisahau jina langu kwa sababu ya Baali.+ 28  Nabii aliye na ndoto na asimulie ndoto hiyo, lakini yule aliye na neno langu anapaswa kulisema neno langu kwa ukweli.” “Nyasi ina uhusiano gani na nafaka?” auliza Yehova. 29  “Je, neno langu si kama moto,”+ auliza Yehova, “na kama nyundo ya chuma inayopasua-pasua jabali?”+ 30  “Basi nitawaadhibu manabii,” asema Yehova, “wanaoibiana maneno yangu.”+ 31  “Nitawaadhibu manabii,” asema Yehova, “wanaotumia ulimi wao kusema, ‘Anasema hivi!’”+ 32  “Nitawaadhibu manabii wa ndoto za uwongo,” asema Yehova, “wanaozisimulia na kuwapotosha watu wangu kwa sababu ya uwongo wao na kujigamba kwao.”+ “Lakini sikuwatuma wala kuwaamuru. Basi hawatawafaidi watu hawa hata kidogo,”+ asema Yehova. 33  “Na watu hawa au nabii au kuhani akiwauliza, ‘Mzigo* wa Yehova ni nini?’ mtawajibu hivi: ‘“Ninyi watu ndio mzigo! Nami nitawatupa,”+ asema Yehova.’ 34  Naye nabii au kuhani au mtu anayesema, ‘Huu ndio mzigo* wa Yehova!’ Nitamkazia fikira mtu huyo na nyumba yake. 35  Hivi ndivyo kila mmoja wenu anavyomwambia mwenzake na pia ndugu yake, ‘Yehova ametoa jibu gani? Na Yehova amesema nini?’ 36  Lakini msiutaje tena mzigo* wa Yehova, kwa maana mzigo* ni neno la kila mtu binafsi, nanyi mmeyabadili maneno ya Mungu aliye hai, Yehova wa majeshi, Mungu wetu. 37  “Utamuuliza nabii huyo hivi: ‘Yehova amekupa jibu gani? Na Yehova amesema nini? 38  Nanyi mkiendelea kusema, “Mzigo* wa Yehova!” Yehova anasema hivi: “Kwa sababu mnasema, ‘Hili neno ndilo mzigo* wa Yehova,’ baada ya mimi kuwaambia, ‘Msiseme: “Mzigo* wa Yehova!”’ 39  tazameni! Nitawainua juu na kuwatupa kutoka mbele zangu, ninyi pamoja na jiji nililowapa ninyi na mababu zenu. 40  Nami nitawaletea aibu ya milele na fedheha ya milele, ambayo haitasahauliwa.”’”+

Maelezo ya Chini

Au “mrithi mwadilifu.”
Au “wameasi imani.”
Tnn., “Wanaitia nguvu mikono ya.”
Au “Wanawajaza matumaini ya uwongo.”
Au “Ujumbe unaochosha.” Neno hilo la Kiebrania lina maana mbili: “ujumbe mzito kutoka kwa Mungu” au “kitu kinachochosha.”
Au “ujumbe unaochosha.”
Au “ujumbe unaochosha.”
Au “ujumbe unaochosha.”
Au “Ujumbe unaochosha.”
Au “ujumbe unaochosha.”
Au “Ujumbe unaochosha.”