Yeremia 25:1-38

  • Kesi ya Yehova dhidi ya mataifa (1-38)

    • Mataifa yatatumikia Babiloni kwa miaka 70 (11)

    • Kikombe cha divai ya ghadhabu ya Mungu (15)

    • Msiba kutoka taifa moja hadi lingine (32)

    • Wale ambao Yehova atawaua (33)

25  Neno lililomjia Yeremia kuhusu watu wote wa Yuda katika mwaka wa nne wa utawala wa Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, ambao ulikuwa mwaka wa kwanza wa Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni.  Nabii Yeremia alisema hivi kuhusu* watu wote wa Yuda na wakaaji wote wa Yerusalemu:  “Tangu mwaka wa 13 wa utawala wa Yosia+ mwana wa Amoni, mfalme wa Yuda, mpaka leo hii, miaka hii 23, neno la Yehova limenijia, nami niliendelea kuwaambia tena na tena,* lakini hamkusikiliza.+  Na Yehova aliwatuma kwenu watumishi wake wote manabii, aliwatuma tena na tena,* lakini hamkusikiliza, wala kutega sikio lenu ili msikie.+  Walikuwa wakisema, ‘Tafadhali, geukeni kila mmoja wenu kutoka katika njia zenu za uovu na matendo yenu maovu;+ nanyi mtaendelea kukaa kwa muda mrefu katika nchi ambayo Yehova aliwapa ninyi na mababu zenu zamani.  Msiifuate miungu mingine na kuiabudu na kuiinamia, na kunikasirisha kwa kazi ya mikono yenu; la sivyo nitawaletea msiba.’  “‘Lakini hamkunisikiliza,’ asema Yehova, ‘Badala yake mlinikasirisha kwa kazi ya mikono yenu, na kujiletea msiba.’+  “Kwa hiyo Yehova wa majeshi anasema hivi: ‘“Kwa sababu hamkuyatii maneno yangu,  ninaziita familia zote za kaskazini,”+ asema Yehova, “ninamwita Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni, mtumishi wangu,+ nami nitawaleta dhidi ya nchi hii+ na dhidi ya wakaaji wake na dhidi ya mataifa haya yote yanayozunguka.+ Nitawaangamiza na kuwafanya kuwa kitu cha kutisha na kitu cha kupigiwa mluzi na magofu ya kudumu. 10  Nitakomesha sauti ya furaha na sauti ya shangwe ndani yao,+ sauti ya bwana harusi na sauti ya bibi harusi,+ sauti ya jiwe la kusagia na nuru ya taa. 11  Na nchi hii yote itakuwa magofu na kitu cha kutisha, na mataifa haya yatalazimika kumtumikia mfalme wa Babiloni kwa miaka 70.”’+ 12  “‘Lakini miaka 70 itakapotimia,+ nitamfanya mfalme wa Babiloni awajibike* na pia taifa hilo kwa sababu ya kosa lao,’+ asema Yehova, ‘nami nitaifanya nchi ya Wakaldayo kuwa mahame na ukiwa daima.+ 13  Nitatimiza maneno yangu yote niliyosema dhidi ya nchi hiyo, yote yaliyoandikwa katika kitabu hiki ambayo Yeremia ametabiri dhidi ya mataifa yote. 14  Kwa maana mataifa mengi na wafalme wakuu+ watawafanya kuwa watumwa,+ nami nitawalipa kulingana na matendo yao na kazi ya mikono yao wenyewe.’”+ 15  Kwa maana Yehova Mungu wa Israeli aliniambia hivi: “Chukua kikombe hiki cha divai ya ghadhabu kutoka mkononi mwangu, nawe uyanyweshe mataifa yote ambayo ninakutuma kwao. 16  Nao watakunywa na kupepesuka na kutenda kama wendawazimu kwa sababu ya upanga ninaotuma miongoni mwao.”+ 17  Basi nikakichukua kile kikombe kutoka mkononi mwa Yehova na kuyanywesha mataifa yote ambayo Yehova alinituma kwao:+ 18  kuanzia Yerusalemu na majiji ya Yuda,+ wafalme wake na wakuu wake, ili kuyafanya kuwa magofu, kitu cha kutisha, kitu cha kupigiwa mluzi na laana,+ kama ilivyo leo; 19  kisha mfalme Farao wa Misri na watumishi wake, wakuu wake, na watu wake wote,+ 20  na watu wa mataifa mbalimbali waliochangamana nao; wafalme wote wa nchi ya Usi; wafalme wote wa nchi ya Wafilisti,+ Ashkeloni,+ Gaza, Ekroni, na watu waliobaki wa Ashdodi; 21  Edomu,+ Moabu,+ na Waamoni;+ 22  wafalme wote wa Tiro, wafalme wote wa Sidoni,+ na wafalme wa kisiwa kilicho baharini; 23  Dedani,+ Tema, Buzi, na wale wote wanaonyoa nywele pembeni mwa vichwa vyao;+ 24  wafalme wote wa Waarabu+ na wafalme wote wa watu wa mataifa mbalimbali wanaokaa nyikani; 25  wafalme wote wa Zimri, wafalme wote wa Elamu,+ na wafalme wote wa Wamedi;+ 26  na wafalme wote wa kaskazini walio karibu na walio mbali, mmoja baada ya mwingine, na falme nyingine zote za dunia zilizo juu ya ardhi; na mfalme wa Sheshaki*+ atakunywa baada yao. 27  “Nawe unapaswa kuwaambia, ‘Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: “Kunyweni, mlewe, mtapike na kuanguka hivi kwamba msiweze kusimama+ kwa sababu ya upanga ninaotuma miongoni mwenu.”’ 28  Nao wakikataa kukichukua kikombe kutoka mkononi mwako ili wanywe, waambie, ‘Yehova wa majeshi anasema hivi: “Lazima mnywe! 29  Kwa maana tazama! ikiwa ninaleta msiba kwanza juu ya jiji linaloitwa kwa jina langu,+ je, ninyi pia hampaswi kuadhibiwa?”’+ “‘Hamtakosa kuadhibiwa, kwa maana ninauita upanga dhidi ya wakaaji wote wa dunia,’ asema Yehova wa majeshi. 30  “Nawe unapaswa kuwatabiria maneno haya yote, uwaambie,‘Yehova atanguruma kutoka juu,Kutoka katika makao yake matakatifu atafanya sauti yake isikike. Atanguruma kwa sauti kubwa dhidi ya makao yake yanayodumu. Atapaza sauti kama watu wanaokanyaga shinikizo la divai,Ataimba kwa ushindi dhidi ya wakaaji wote wa dunia.’ 31  ‘Kelele zitasikika mpaka kwenye miisho ya dunia,Kwa maana Yehova ana kesi dhidi ya mataifa. Yeye binafsi atawahukumu wanadamu wote.*+ Naye atawaangamiza waovu kwa upanga,’ asema Yehova. 32  Yehova wa majeshi anasema hivi: ‘Tazameni! Msiba unaenea kutoka taifa mpaka taifa,+Na tufani kubwa itaachiliwa kutoka sehemu za mbali zaidi za dunia.+ 33  “‘Na wale ambao Yehova atawaua siku hiyo watatapakaa kutoka mwisho mmoja wa dunia mpaka mwisho wa pili wa dunia. Hawataombolezewa, wala kukusanywa wala kuzikwa. Watakuwa kama mbolea juu ya ardhi.’ 34  “Ombolezeni, enyi wachungaji, na mlie kwa sauti! Mgaegae, enyi watu mashuhuri wa kundi,Kwa sababu wakati wenu wa kuchinjwa na kutawanywa umefika,Nanyi mtaanguka kama chombo chenye thamani! 35  Wachungaji hawana mahali pa kukimbilia,Na watu mashuhuri wa kundi hawawezi kuponyoka. 36  Sikilizeni! Kilio cha wachungajiNa kuomboleza kwa watu mashuhuri wa kundi,Kwa maana Yehova anaharibu malisho yao. 37  Na makao yenye amani yamefanywa yasiwe na uhaiKwa sababu ya hasira ya Yehova inayowaka. 38  Ametoka katika pangolake kama mwanasimba,*+Kwa maana nchi yao imekuwa kitu cha kutishaKwa sababu ya upanga wenye ukatiliNa kwa sababu ya hasira yake inayowaka.”

Maelezo ya Chini

Tnn., “Nebukadreza,” njia nyingine ya kuandika jina hili.
Au “aliwaambia hivi.”
Tnn., “kuamka mapema na kusema.”
Tnn., “akiamka mapema na kuwatuma.”
Tnn., “Nebukadreza,” njia nyingine ya kuandika jina hili.
Au “nitamwadhibu mfalme wa Babiloni.”
Inaonekana hili ni jina la siri la Babeli (Babiloni).
Tnn., “wote wenye mwili wa nyama.”
Au “mwanasimba mwenye manyoya marefu shingoni.”