Yeremia 3:1-25

  • Kina cha uasi imani wa Israeli (1-5)

  • Israeli na Yuda wana hatia ya uzinzi (6-11)

  • Mwito wa kutubu (12-25)

3  Watu huuliza: “Mtu akimfukuza mke wake naye aondoke na kuchukuliwa na mwanamume mwingine, je, mtu huyo anapaswa kumrudia tena?” Je, nchi hiyo haijachafuliwa kabisa?+ “Umefanya ukahaba na marafiki wengi,+Na je, sasa unapaswa kurudi kwangu?” asema Yehova.   “Inua macho yako kuelekea vilima vitupu uone. Ni wapi ambapo hukubakwa? Ulikaa kando ya barabara kwa ajili yao,Kama mtu anayehamahama* nyikani. Unaendelea kuichafua nchiKwa ukahaba wako na uovu wako.+   Kwa hiyo manyunyu ya mvua yamezuiwa,+Na hakuna mvua ya masika. Una uso wenye* ushupavu kama mwanamke anayefanya ukahaba;Umekataa kuona aibu.+   Lakini sasa unaniambia kwa sauti kubwa,‘Baba yangu, wewe ni rafiki yangu tangu ujana wangu!+   Je, mtu anapaswa kuendelea kuwa na uchungu milele,Au kuwa na kinyongo sikuzote?’ Unasema hivyo,Lakini unaendelea kufanya mambo yote maovu unayoweza kufanya.”+  Katika siku za mfalme Yosia,+ Yehova aliniambia: “‘Je, umeona mambo ambayo Israeli asiye mwaminifu ametenda? Amepanda juu ya kila mlima mrefu na kwenda chini ya kila mti wenye majani mengi ili afanye ukahaba.+  Hata baada ya kufanya mambo hayo yote, niliendelea kumwambia arudi kwangu,+ lakini hakurudi; na Yuda akaendelea kumtazama dada yake mwenye hila.+  Nilipoona hivyo, nikamfukuza Israeli asiye mwaminifu akiwa na cheti kamili cha talaka+ kwa sababu ya uzinzi wake.+ Lakini Yuda dada yake mwenye hila hakuogopa; yeye pia alienda na kufanya ukahaba.+  Aliona ukahaba wake kuwa jambo dogo, naye akaendelea kuichafua nchi na kufanya uzinzi na mawe na miti.+ 10  Licha ya hayo yote, Yuda dada yake mwenye hila hakurudi kwangu kwa moyo wake wote, bali kwa kujifanya tu,’ asema Yehova.” 11  Kisha Yehova akaniambia: “Israeli asiye mwaminifu amekuwa mwadilifu kuliko Yuda mwenye hila.+ 12  Nenda uitangazie kaskazini maneno haya:+ “‘“Rudi, Ee Israeli mwasi,” asema Yehova.’+ ‘“Sitakutazama kwa hasira,*+ kwa maana mimi ni mshikamanifu,” asema Yehova.’ ‘“Sitaendelea kuwa na kinyongo milele. 13  Ila tu ukubali hatia yako, kwa maana umemwasi Yehova Mungu wako. Uliendelea kutawanya wema wako* kwa wageni* chini ya kila mti wenye majani mengi, lakini hukuitii sauti yangu,” asema Yehova.’” 14  “Rudini, enyi wana waasi,” asema Yehova. “Kwa maana nimekuwa bwana wenu* wa kweli; nami nitawachukua, mmoja kutoka katika jiji moja na wawili kutoka katika familia moja, nami nitawaleta Sayuni.+ 15  Nami nitawapa wachungaji wanaoupendeza moyo wangu,+ nao watawalisha kwa ujuzi na ufahamu. 16  Mtakuwa wengi nanyi mtazaa matunda nchini siku hizo,” asema Yehova.+ “Hawatasema tena, ‘Sanduku la agano la Yehova!’ Halitaingia moyoni, wala hawatalikumbuka au kulitamani, nalo halitatengenezwa tena. 17  Wakati huo wataliita Yerusalemu kiti cha ufalme cha Yehova;+ na mataifa yote yatakusanywa pamoja kwa jina la Yehova katika Yerusalemu,+ nao hawataufuata tena kwa ukaidi moyo wao mwovu.” 18  “Siku hizo watatembea pamoja, nyumba ya Yuda kando ya nyumba ya Israeli,+ na pamoja watatoka katika nchi ya kaskazini na kuingia katika nchi niliyowapa mababu zenu kuwa urithi.+ 19  Nami nilifikiri, ‘Jinsi nilivyokuweka kati ya wana na kukupa nchi inayotamanika, urithi maridadi zaidi kati ya mataifa!’*+ Pia nilifikiri mtaniita ‘Baba yangu!’ na kwamba hamtageuka na kuacha kunifuata.’ 20  ‘Kwa kweli kama mke anavyomwacha mume wake* kwa hila, ninyi pia, enyi watu wa nyumba ya Israeli, mmenitendea kwa hila,’+ asema Yehova.” 21  Sauti imesikika kwenye vilima vilivyo vitupu,Kulia na kusihi kwa watu wa Israeli,Kwa maana wameipotosha njia yao;Wamemsahau Yehova Mungu wao.+ 22  “Rudini, ninyi wana waasi. Nitaiponya hali yenu ya uasi.”+ “Tupo hapa! Tumekuja kwako,Kwa maana wewe, Ee Yehova, ni Mungu wetu.+ 23  Kwa kweli vilima na machafuko juu ya milima ni udanganyifu.+ Kwa kweli wokovu wa Israeli uko kwa Yehova Mungu wetu.+ 24  Lakini jambo la aibu limekula* kazi ngumu ya mababu zetu tangu ujana wetu,+Makundi yao na mifugo yao,Wana wao na mabinti wao. 25  Na tulale chini katika aibu yetu,Fedheha yetu na itufunike,Kwa maana tumemtendea dhambi Yehova Mungu wetu,+Sisi na baba zetu tangu ujana wetu mpaka leo hii,+Nasi hatujaitii sauti ya Yehova Mungu wetu.”

Maelezo ya Chini

Tnn., “Mwarabu.”
Tnn., “paji lenye.”
Tnn., “Sitaufanya uso wangu uanguke juu yako.”
Tnn., “njia zako.”
Au “miungu ya kigeni.”
Au labda, “mume wenu.”
Tnn., “majeshi ya mataifa.”
Tnn., “mwenzake.”
Au “mungu wa aibu amekula.”