Yeremia 30:1-24

  • Ahadi za kurudishwa na kuponywa (1-24)

30  Neno hili lilimjia Yeremia kutoka kwa Yehova, likisema:  “Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Andika katika kitabu maneno yote ninayokuambia.  Kwa maana “tazama! siku zinakuja,” asema Yehova, “nitakapowakusanya watu wangu waliotekwa, Israeli na Yuda,”+ asema Yehova, “nami nitawarudisha katika nchi niliyowapa mababu zao, nao wataimiliki tena.”’”+  Haya ndiyo maneno ambayo Yehova aliwaambia watu wa Israeli na Yuda.   Yehova anasema hivi: “Tumesikia sauti za kutetemeka;Kuna hofu, na hakuna amani.   Ulizeni, tafadhali, ikiwa mwanamume anaweza kujifungua mtoto. Hivyo basi, kwa nini ninamwona kila mwanamume mwenye nguvu akishika tumbo lake*Kama mwanamke anayejifungua?+ Kwa nini kila uso umegeuka rangi?   Ole wangu! Kwa maana siku hiyo inatisha sana.*+ Hakuna nyingine kama hiyo,Wakati wa taabu kwa Yakobo. Lakini ataokolewa kutokana nayo.”  “Na siku hiyo,” asema Yehova wa majeshi, “nitaivunja nira kutoka shingoni mwako, na mikanda yako nitaikata* vipande viwili; na wageni* hawatamfanya* tena kuwa mtumwa wao.  Watamtumikia Yehova Mungu wao na Daudi mfalme wao, ambaye nitamweka juu yao.”+ 10  “Nawe, mtumishi wangu Yakobo, usiogope,” asema Yehova,“Wala usihofu, Ee Israeli.+ Kwa maana nitakuokoa kutoka mbaliNa uzao wako kutoka katika nchi waliyopelekwa utekwani.+ Yakobo atarudi na kuwa na utulivu bila usumbufu,Na hakuna yeyote atakayewaogopesha.”+ 11  “Kwa maana mimi niko pamoja nawe,” asema Yehova, “ili nikuokoe. Lakini nitaleta maangamizi katika mataifa yote ambako nilikutawanya;+Lakini wewe, sitakuangamiza.+ Nitakutia nidhamu* kwa kiwango kinachofaa,Nami sitakuacha kamwe bila kukuadhibu.”+ 12  Kwa maana Yehova anasema hivi: “Hakuna matibabu kwa ajili ya jeraha lako.*+ Kidonda chako hakiwezi kupona. 13  Hakuna mtu wa kukutetea,Hakuna njia ya kukiponya kidonda chako. Hakuna dawa ya kukuponya. 14  Wapenzi wako wote wamekusahau.+ Hawakutafuti tena. Kwa maana nimekupiga kwa pigo la adui,+Kwa adhabu ya mtu mkatili,Kwa sababu ya hatia yako kubwa na dhambi zako nyingi.+ 15  Kwa nini unapaza kilio kwa sababu ya jeraha lako?* Maumivu yako hayawezi kupona! Kwa sababu ya hatia yako kubwa na dhambi zako nyingi+Nimekutendea hivyo. 16  Kwa hiyo wale wote wanaokumeza, watamezwa,+Na maadui wako wote watapelekwa pia utekwani.+ Wale wanaokupora wataporwa,Nami nitawatia mikononi mwa waporaji wale wote wanaokupora.”+ 17  “Lakini nitakurudishia afya yako na kuyaponya majeraha yako,”+ asema Yehova,“Ingawa walikuita mtu aliyetengwa: ‘Sayuni, asiyetafutwa na yeyote.’”+ 18  Yehova anasema hivi: “Ninawakusanya mateka wa mahema ya Yakobo,+Nami nitayahurumia makao yake. Jiji litajengwa upya juu ya kilima chake,+Na mnara wenye ngome utasimama mahali pake panapofaa. 19  Na kutoka kwao kutakuwa na shukrani na sauti za kicheko.+ Nitawazidisha, nao hawatakuwa wachache;+Nitawafanya kuwa wengi,*Nao hawatakuwa duni.+ 20  Wanawe watakuwa kama walivyokuwa zamani,Na kusanyiko lake litaimarishwa kabisa mbele zangu.+ Nitakabiliana na wote wanaomkandamiza.+ 21  Mtu wake mashuhuri atatoka kati yake,Na mtawala wake atatoka kati yake. Nitamfanya akaribie, naye atanikaribia.” “La sivyo, ni nani anayeweza kuthubutu kunikaribia?”* asema Yehova. 22  “Nanyi mtakuwa watu wangu,+ nami nitakuwa Mungu wenu.”+ 23  Tazameni! Dhoruba ya Yehova ya upepo italipuka kwa ghadhabu,+Tufani inayofagia ambayo inazunguka ikishuka juu ya kichwa cha waovu. 24  Hasira inayowaka ya Yehova haitapoaMpaka atakapotekeleza na kutimiza makusudi ya moyo wake.+ Mtaelewa jambo hilo katika siku za mwisho.+

Maelezo ya Chini

Au “kiuno chake.”
Tnn., “ni kuu.”
Tnn., “pingu zako nitazikata.”
Au “wageni kutoka nchi nyingine.”
Au “hawatawafanya.”
Au “Nitakurekebisha.”
Au “jeraha lako la kuvunjika.”
Au “jeraha lako la kuvunjika.”
Au labda, “waheshimiwe.”
Tnn., “kutoa moyo wake kuwa rehani ili anikaribie?”