Yeremia 31:1-40

  • Waisraeli waliobaki wataishi tena nchini (1-30)

    • Raheli awaombolezea watoto wake (15)

  • Agano jipya (31-40)

31  “Wakati huo,” asema Yehova, “Nitakuwa Mungu wa familia zote za Israeli, nao watakuwa watu wangu.”+   Yehova anasema hivi: “Watu waliookoka upanga walipata kibali nyikaniIsraeli alipokuwa akitembea kwenda mahali pake pa kupumzika.”   Kutoka mbali Yehova alinitokea na kusema: “Nimekupenda kwa upendo wa milele. Ndiyo sababu nimekuvuta kwangu kwa upendo mshikamanifu.*+   Kwa mara nyingine tena nitakujenga upya nawe utajengwa upya.+ Ewe bikira wa Israeli, utachukua tena matari yakoNa kwenda ukicheza dansi kwa shangwe.*+   Utapanda tena mashamba ya mizabibu kwenye milima ya Samaria;+Wanaopanda watapanda na kufurahia matunda yake.+   Kwa maana siku itafika ambayo walinzi walio kwenye milima ya Efraimu watapaza sauti wakisema: ‘Inukeni, twendeni juu Sayuni, kwa Yehova Mungu wetu.’”+   Kwa maana Yehova anasema hivi: “Mlilieni Yakobo kwa shangwe. Pigeni vigelegele vya shangwe kwa sababu mko juu ya mataifa.+ Tangazeni jambo hilo; sifuni na kusema,‘Ee Yehova, waokoe watu wako, Waisraeli wanaobaki.’+   Ninawarudisha kutoka nchi ya kaskazini.+ Nitawakusanya pamoja kutoka sehemu za mbali zaidi za dunia.+ Miongoni mwao kutakuwa na vipofu na vilema,+Mwanamke mwenye mimba na yule anayezaa, wote pamoja. Watarudi hapa wakiwa kutaniko kubwa.+   Watakuja wakilia.+ Nitawaongoza huku wakiomba kibali. Nitawaongoza kwenye vijito vya* maji,+Kwenye kijia tambarare ambacho hakitawafanya wajikwae. Kwa maana mimi ni Baba ya Israeli, naye Efraimu ni mzaliwa wangu wa kwanza.”+ 10  Sikieni neno la Yehova, enyi mataifa,Na mlitangaze kati ya visiwa vilivyo mbali sana:+ “Yule aliyemtawanya Israeli atamkusanya pamoja. Atamlinda kama mchungaji anavyochunga kundi lake.+ 11  Kwa maana Yehova atamkomboa Yakobo+Na kumwokoa* kutoka mikononi mwa yule aliye na nguvu zaidi yake.+ 12  Watakuja na kupiga vigelegele vya shangwe juu ya kilele cha Sayuni+Na kung’aa kwa sababu ya wema wa* Yehova,Kwa sababu ya nafaka na divai mpya+ na mafuta,Na kwa sababu ya wanakondoo na ndama.+ Watakuwa* kama bustani iliyonyweshwa maji vizuri,+Nao hawatadhoofika tena.”+ 13  “Wakati huo bikira atacheza dansi kwa shangwe,Pia wanaume vijana na wanaume wazee pamoja.+ Nitayageuza maombolezo yao yawe furaha.+ Nitawafariji na kuwafanya washangilie badala ya kuhuzunika.+ 14  Nami nitawashibisha makuhani kwa vitu vingi,*Na watu wangu watashiba wema wangu,”+ asema Yehova. 15  “Yehova anasema hivi: ‘Sauti inasikika kule Rama,+ maombolezo na kilio cha uchungu: Raheli anawalilia wanawe.*+ Amekataa kufarijiwa kuhusiana na wanawe,Kwa sababu hawako tena.’”+ 16  Yehova anasema hivi: “‘Zuia sauti yako usilie na macho yako yasitokwe na machozi,Kwa maana utapata thawabu kwa ajili ya kazi yako,’ asema Yehova. ‘Watarudi kutoka nchi ya adui.’+ 17  ‘Na kuna tumaini kwa ajili ya wakati wako ujao,’+ asema Yehova. ‘Wana wako watarudi kwenye eneo lao wenyewe.’”+ 18  “Hakika nimemsikia Efraimu akiomboleza,‘Umenirekebisha, nami nimerekebishwa,Kama ndama ambaye hajazoezwa. Nirudishe, nami nitageuka bila kusita,Kwa maana wewe ni Yehova Mungu wangu. 19  Kwa maana baada ya kugeuka nilijuta;+Baada ya kusaidiwa kuelewa nilipiga paja langu kwa huzuni. Niliaibika na kufedheheka,+Kwa maana nilibeba shutuma ya ujana wangu.’” 20  “Je, Efraimu si mwana mwenye thamani kwangu, au mtoto mpendwa?+ Kwa maana kila mara ninapomshutumu, bado ninamkumbuka. Ndiyo sababu hisia zangu zimechochewa* kwa ajili yake.+ Nami hakika nitamhurumia,” asema Yehova.+ 21  “Jiwekee alama za barabara,Na uweke vibao vya ishara.+ Kazia fikira barabara kuu, njia ambayo unapaswa kupitia.+ Rudi, ewe bikira wa Israeli, rudi kwenye majiji haya yako. 22  Utaendelea kuyumbayumba mpaka lini, ewe binti usiye mwaminifu? Kwa maana Yehova ameumba jambo jipya duniani: Mwanamke atamtafuta mwanamume kwa bidii.” 23  Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: “Watasema tena maneno haya katika nchi ya Yuda na katika majiji yake nitakapowakusanya na kuwarudisha mateka wao: ‘Yehova na akubariki, Ee makao ya uadilifu,+ Ee mlima mtakatifu.’+ 24  Na watu wa Yuda na majiji yake yote watakaa pamoja ndani yake, wakulima na wale wanaochunga kondoo.+ 25  Kwa maana nitamshibisha aliyechoka na kumjaza kila mtu aliyedhoofika.”+ 26  Ndipo nikaamka na kufungua macho yangu, na usingizi wangu ulikuwa mtamu. 27  “Tazama! Siku zinakuja,” asema Yehova, “nitakapoipanda nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda kwa mbegu ya* mwanadamu na kwa mbegu ya mifugo.”+ 28  “Na kama nilivyowakazia uangalifu ili kuwang’oa, kuwabomoa, kuwaangusha, kuwaharibu, na kuwadhuru,+ ndivyo nitakavyowakazia uangalifu ili kuwajenga na kuwapanda,”+ asema Yehova. 29  “Katika siku hizo hawatasema tena, ‘Akina baba walikula zabibu chachu, lakini meno ya wana ndiyo yaliyotiwa ukakasi.’*+ 30  Lakini wakati huo kila mtu atakufa kwa sababu ya kosa lake mwenyewe. Mtu yeyote atakayekula zabibu chachu, atatiwa ukakasi kwenye meno yake mwenyewe.” 31  “Tazama! Siku zinakuja,” asema Yehova, “nitakapofanya agano jipya pamoja na nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda.+ 32  Halitakuwa kama agano nililofanya pamoja na mababu zao siku niliyowashika mkono na kuwaongoza kutoka nchini Misri,+ ‘agano langu ambalo walilivunja,+ ingawa nilikuwa bwana* wao wa kweli,’ asema Yehova.” 33  “Kwa maana hili ndilo agano nitakalofanya pamoja na nyumba ya Israeli baada ya siku hizo,” asema Yehova. “Nitaitia sheria yangu ndani yao,+ nami nitaiandika katika moyo wao.+ Nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.”+ 34  “Nao hawatafundishana tena kila mtu na jirani yake na kila mtu na ndugu yake, wakisema, ‘Mjue Yehova!’+ kwa maana wote watanijua, kuanzia mdogo zaidi mpaka mkubwa zaidi kati yao,”+ asema Yehova. “Kwa maana nitalisamehe kosa lao, nami sitaikumbuka tena dhambi yao.”+ 35  Yehova,Ambaye hutoa jua ili liangaze wakati wa mchana,Sheria za* mwezi na nyota ili ziangaze usiku,Anayeitibua bahari na kuyavuruga mawimbi yake,Ambaye jina lake ni Yehova wa majeshi, anasema hivi:+ 36  “‘Ikiwa sheria hizo zitakoma,’ asema Yehova,‘Basi uzao wa Israeli utakoma daima kuwa taifa mbele zangu.’”+ 37  Yehova anasema hivi: “‘Ikiwa mbingu zilizo juu zinaweza kupimwa na misingi ya dunia iliyo chini kuchunguzwa, basi ninaweza kuukataa uzao wote wa Israeli kwa sababu ya yote ambayo wamefanya,’ asema Yehova.”+ 38  “Tazama! Siku zinakuja,” asema Yehova, “ambapo jiji litajengwa+ kwa ajili ya Yehova kutoka Mnara wa Hananeli+ mpaka Lango la Pembeni.+ 39  Nayo kamba ya kupimia+ itaenda moja kwa moja mpaka kwenye kilima cha Garebu, nayo itageuka na kuelekea Goa. 40  Na bonde lote la mizoga na la* majivu,* na matuta yote mpaka Bonde la Kidroni,+ mpaka kwenye pembe ya Lango la Farasi+ kuelekea mashariki, litakuwa kitu kitakatifu kwa Yehova.+ Halitang’olewa tena kamwe wala kubomolewa.”

Maelezo ya Chini

Au “nimeendelea kukutendea kwa upendo mshikamanifu.”
Au “utaenda kucheza dansi ya wale wanaocheka.”
Au “makorongo ya.”
Au “kumkomboa.”
Au “vitu vizuri kutoka kwa.”
Au “Nafsi yao itakuwa.”
Tnn., “mafuta.”
Au “watoto wake.”
Tnn., “matumbo yangu yamechochewa.”
Au “uzao wa.”
Au “yaliyotiwa ganzi.”
Au labda, “mume.”
Au “Amri za.”
Au “nchi yote tambarare ya chini ya mizoga na ya.”
Au “majivu yenye mafuta,” yaani, majivu yaliyojaa mafuta ya dhabihu.