Yeremia 33:1-26

  • Ahadi ya kurudishwa (1-13)

  • Usalama chini ya “chipukizi adilifu” (14-16)

  • Agano pamoja na Daudi na makuhani (17-26)

    • Agano kuhusu mchana na usiku (20)

33  Neno la Yehova likamjia Yeremia mara ya pili, alipokuwa bado amezuiliwa katika Ua wa Walinzi,+ na kusema:  “Yehova, Muumba wa dunia, anasema hivi, Yehova aliyeiumba na kuifanya imara kabisa; Yehova ndilo jina lake,  ‘Niite, nami nitakujibu na kukuambia kwa utayari mambo makubwa na yasiyoeleweka ambayo hujayajua.’”+  “Kwa maana Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi kuhusu nyumba za jiji hili na kuhusu nyumba za wafalme wa Yuda ambazo zimebomolewa kwa sababu ya maboma ya kuzingira na kwa sababu ya upanga,+  na kuhusu wale wanaokuja kupigana na Wakaldayo, na kujaza maeneo haya mizoga ya wale niliowaua katika hasira yangu na katika ghadhabu yangu, wale ambao uovu wao umenifanya niufiche uso wangu kutoka kwenye jiji hili:  ‘Ninamponya na kumpa afya,+ nami nitawaponya na kuwafunulia wingi wa amani na kweli.+  Nami nitawarudisha mateka wa Yuda na mateka wa Israeli,+ nami nitawajenga kama nilivyofanya mwanzoni.+  Nami nitawatakasa kutokana na hatia yote ya dhambi walizonitendea,+ nami nitasamehe hatia yote ya dhambi zao na makosa waliyonikosea.+  Naye atakuwa kwangu jina la furaha, sifa, na uzuri mbele ya mataifa yote ya dunia yatakayosikia kuhusu wema wote nitakaowapa.+ Nao wataogopa na kutetemeka+ kwa sababu ya wema na amani ninayompa.’”+ 10  “Yehova anasema hivi, ‘Mahali hapa ambapo mtasema ni nchi iliyo ukiwa, isiyo na wanadamu wala mifugo, katika majiji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu zilizo tupu, bila wanadamu wala wakaaji wala mifugo, itasikika tena 11  sauti ya furaha na sauti ya shangwe,+ sauti ya bwana harusi na sauti ya bibi harusi, sauti ya wale wanaosema: “Mshukuruni Yehova wa majeshi, kwa maana Yehova ni mwema;+ upendo wake mshikamanifu unadumu milele!”’+ “‘Wataleta matoleo ya shukrani katika nyumba ya Yehova,+ kwa maana nitawarudisha mateka wa nchi, kama hapo mwanzoni,’ asema Yehova.” 12  “Yehova wa majeshi anasema hivi, ‘Katika eneo hili lenye ukiwa, lisilo na mtu au mifugo, na katika majiji yake yote kutakuwa tena na malisho kwa ajili ya wachungaji kupumzisha makundi yao.’+ 13  “‘Katika majiji ya eneo lenye milima, katika majiji ya eneo la chini, katika majiji ya kusini, katika nchi ya Benjamini, katika maeneo yanayozunguka Yerusalemu+ na katika majiji ya Yuda,+ makundi yatapita tena chini ya mikono ya mtu anayeyahesabu,’ asema Yehova.” 14  “‘Tazama! Siku zinakuja,’ asema Yehova, ‘nitakapotimiza ahadi nzuri niliyotoa kuhusu nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda.+ 15  Siku hizo na wakati huo nitamchipushia Daudi chipukizi adilifu,*+ naye atatenda haki na uadilifu katika nchi.+ 16  Siku hizo Yuda ataokolewa+ na Yerusalemu litakaa katika usalama.+ Naye ataitwa: Yehova Ni Uadilifu Wetu.’”+ 17  “Kwa maana Yehova anasema hivi, ‘Hutakosa kamwe mwanamume wa ukoo wa Daudi atakayeketi kwenye kiti cha ufalme cha nyumba ya Israeli,+ 18  wala makuhani Walawi hawatakosa mtu wa kusimama mbele zangu ili kutoa dhabihu nzima za kuteketeza, kuchoma matoleo ya nafaka, na kutoa dhabihu.’” 19  Nalo neno la Yehova likamjia Yeremia tena, na kusema: 20  “Yehova anasema hivi, ‘Ikiwa mngeweza kulivunja agano langu kuhusu mchana na agano langu kuhusu usiku, ili kuzuia mchana na usiku usije kwa wakati wake,+ 21  hapo ndipo agano langu pamoja na mtumishi wangu Daudi lingeweza kuvunjwa,+ ili asiwe na mwana anayetawala akiwa mfalme kwenye kiti chake cha ufalme,+ na pia agano langu pamoja na makuhani, Walawi, wahudumu wangu.+ 22  Kama jeshi la mbinguni lisivyoweza kuhesabiwa wala mchanga wa bahari usivyoweza kupimwa, ndivyo nitakavyouzidisha uzao wa* mtumishi wangu Daudi na Walawi wanaonihudumia.’” 23  Nalo neno la Yehova likamjia tena Yeremia, na kusema: 24  “Je, hujasikia yale ambayo watu hawa wanasema, ‘Yehova atazikataa familia mbili alizozichagua’? Nao wanawavunjia heshima watu wangu, na hawawatambui tena kuwa taifa. 25  “Yehova anasema hivi: ‘Kwa hakika kama nilivyoweka imara agano langu kuhusu mchana na usiku,+ sheria za* mbingu na dunia,+ 26  vivyo hivyo sitaukataa kamwe uzao wa* Yakobo na wa mtumishi wangu Daudi, hivi kwamba nisichukue kutoka kwa uzao wake* watawala wa wazao wa* Abrahamu, Isaka, na Yakobo. Kwa maana nitawakusanya mateka wao+ na kuwahurumia.’”+

Maelezo ya Chini

Au “mrithi mwadilifu.”
Tnn., “mbegu ya.”
Au “amri za.”
Tnn., “mbegu ya.”
Tnn., “mbegu yake.”
Tnn., “mbegu ya.”