Yeremia 36:1-32

  • Yeremia asema mambo kisha yaandikwa katika kitabu cha kukunjwa (1-7)(1-7)

  • Baruku asoma kwa sauti kitabu cha kukunjwa (8-19)

  • Yehoyakimu akichoma moto kitabu hicho cha kukunjwa (20-26)

  • Ujumbe waandikwa tena kwenye kitabu kipya cha kukunjwa (27-32)

36  Sasa katika mwaka wa nne wa utawala wa Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, neno hili lilimjia Yeremia kutoka kwa Yehova likisema:  “Chukua kitabu cha kukunjwa na uandike ndani yake maneno yote ambayo nimekuambia dhidi ya Israeli na Yuda+ na mataifa yote,+ tangu siku ya kwanza niliyozungumza nawe katika siku za utawala wa Yosia mpaka leo hii.+  Labda watu wa nyumba ya Yuda watakaposikia kuhusu msiba wote ninaokusudia kuwaletea, wataziacha njia zao za uovu, ili niwasamehe kosa lao na dhambi yao.”+  Kisha Yeremia akamwita Baruku+ mwana wa Neria, naye Yeremia akamwambia maneno yote ambayo Yehova alikuwa amemwambia, naye Baruku akayaandika maneno hayo katika kitabu cha kukunjwa Yeremia alipokuwa akiyasema.+  Kisha Yeremia akamwamuru Baruku: “Nimezuiliwa, siwezi kuingia katika nyumba ya Yehova.  Basi wewe ndiye utakayeingia na kusoma kwa sauti maneno ya Yehova yaliyo katika kitabu cha kukunjwa ulichoandika nilipokuwa nikiyasema. Yasome watu wakisikia katika nyumba ya Yehova siku ya kufunga; basi utawasomea watu wote wa Yuda wanaokuja kutoka katika majiji yao.  Labda ombi lao la kutaka kibali litamfikia Yehova, nao watageuka, kila mtu kutoka katika njia zake za uovu, kwa maana Yehova amewatangazia watu hawa hasira na ghadhabu kubwa.”  Basi Baruku mwana wa Neria akafanya yote ambayo nabii Yeremia alimwamuru; akasoma kwa sauti maneno ya Yehova yaliyokuwa katika kile kitabu cha kukunjwa kwenye nyumba ya Yehova.+  Katika mwaka wa tano wa utawala wa Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, katika mwezi wa tisa, watu wote wa Yerusalemu na watu wote waliokuja Yerusalemu kutoka katika majiji ya Yuda wakatangaza watu wafunge mbele za Yehova.+ 10  Kisha Baruku akasoma kwa sauti maneno ya Yeremia yaliyokuwa katika kile kitabu cha kukunjwa kwenye nyumba ya Yehova, katika chumba* cha Gemaria+ mwana wa Shafani+ mwandishi,* katika ua wa juu, kwenye njia inayoelekea kwenye lango jipya la nyumba ya Yehova,+ watu wote wakisikia. 11  Mikaya mwana wa Gemaria mwana wa Shafani alipoyasikia maneno yote ya Yehova kutoka katika kile kitabu cha kukunjwa, 12  akashuka kwenda kwenye nyumba ya* mfalme, katika chumba cha mwandishi. Wakuu wote* walikuwa wameketi humo: mwandishi Elishama,+ Delaya mwana wa Shemaya, Elnathani+ mwana wa Akbori,+ Gemaria mwana wa Shafani, Sedekia mwana wa Hanania, na wakuu wengine wote. 13  Mikaya akawaambia maneno yote aliyokuwa ameyasikia Baruku aliposoma kile kitabu cha kukunjwa mbele ya watu. 14  Ndipo wakuu wote wakamtuma Yehudi mwana wa Nethania mwana wa Shelemia mwana wa Kushi kwa Baruku, wakisema: “Njoo na kitabu cha kukunjwa ulichosoma mbele ya watu.” Baruku mwana wa Neria akabeba kile kitabu cha kukunjwa mkononi mwake na kuingia walimokuwa. 15  Wakamwambia: “Tafadhali keti, nawe utusomee kitabu hicho kwa sauti.” Basi Baruku akawasomea kitabu hicho. 16  Sasa mara tu walipoyasikia maneno hayo yote, wakaangaliana kwa hofu, nao wakamwambia Baruku: “Lazima tumwambie mfalme maneno haya yote.” 17  Nao wakamuuliza Baruku: “Tafadhali tuambie jinsi ulivyoandika maneno haya yote. Je, aliyasema huku ukiandika?” 18  Baruku akawajibu: “Aliniambia maneno haya yote, nami nikayaandika kwa wino katika kitabu hiki cha kukunjwa.” 19  Wakuu wakamwambia Baruku: “Nenda ujifiche, wewe pamoja na Yeremia, na msiache mtu yeyote ajue mahali mlipo.”+ 20  Kisha wakaingia kwa mfalme, kwenye ua, na kukiweka kitabu hicho cha kukunjwa kwenye chumba cha mwandishi Elishama, nao wakamwambia mfalme kila kitu walichosikia. 21  Basi mfalme akamtuma Yehudi+ aende kuleta kitabu hicho cha kukunjwa, naye akakileta kutoka katika chumba cha mwandishi Elishama. Yehudi akaanza kukisoma mbele ya mfalme na wakuu wote waliokuwa wamesimama karibu na mfalme. 22  Mfalme alikuwa ameketi katika nyumba ya majira ya baridi kali, katika mwezi wa tisa,* huku jiko la makaa likiwaka mbele yake. 23  Kila mara Yehudi aliposoma safu tatu au nne, mfalme aliikata sehemu hiyo kwa kisu cha mwandishi na kuitupa ndani ya moto katika jiko la makaa, mpaka kitabu chote cha kukunjwa kilipoteketea katika jiko hilo. 24  Nao hawakushikwa na hofu yoyote; wala mfalme wala watumishi wake wote waliosikia maneno hayo hawakuyararua mavazi yao. 25  Ingawa Elnathani,+ Delaya,+ na Gemaria+ walimsihi mfalme asikiteketeze kitabu hicho cha kukunjwa, hakuwasikiliza. 26  Isitoshe, mfalme akawaamuru Yerahmeeli mwana wa mfalme, Seraya mwana wa Azrieli, na Shelemia mwana wa Abdeeli wamkamate mwandishi Baruku na nabii Yeremia, lakini Yehova akaendelea kuwaficha.+ 27  Na neno hili la Yehova likamjia Yeremia tena baada ya mfalme kukiteketeza kile kitabu cha kukunjwa kilichokuwa na maneno ambayo Baruku aliyaandika Yeremia alipokuwa akiyasema:+ 28  “Chukua kitabu kingine cha kukunjwa nawe uandike ndani yake maneno yaleyale yaliyokuwa kwenye kile kitabu cha kwanza cha kukunjwa, ambacho Mfalme Yehoyakimu wa Yuda alikiteketeza.+ 29  Nawe unapaswa kusema hivi dhidi ya Mfalme Yehoyakimu wa Yuda: ‘Yehova anasema hivi: “Umekiteketeza kitabu hiki cha kukunjwa na kusema, ‘Kwa nini umeandika ndani yake, “Mfalme wa Babiloni atakuja hakika na kuiharibu nchi hii na kumwangamiza mwanadamu na mnyama kutoka humu”?’+ 30  Kwa hiyo Yehova anasema hivi dhidi ya Mfalme Yehoyakimu wa Yuda, ‘Hatakuwa na mtu yeyote atakayeketi kwenye kiti cha ufalme cha Daudi,+ na maiti yake itaachwa nje kwenye joto wakati wa mchana na baridi kali wakati wa usiku.+ 31  Nitamwadhibu yeye na wazao wake* na watumishi wake kwa sababu ya kosa lao, nami nitawaletea wao na wakaaji wa Yerusalemu na watu wa Yuda msiba wote niliotangaza dhidi yao,+ lakini hawakusikiliza.’”’”+ 32  Kisha Yeremia akachukua kitabu kingine cha kukunjwa na kumpa Baruku mwana wa Neria, mwandishi,+ naye akaandika maneno yote aliyoambiwa na Yeremia ambayo yalikuwa katika kile kitabu cha kukunjwa ambacho Mfalme Yehoyakimu wa Yuda alikuwa amekiteketeza motoni.+ Na maneno mengine mengi kama hayo yakaongezwa.

Maelezo ya Chini

Au “chumba cha kulia chakula.”
Au “aliyenakili maandishi.”
Au “Maofisa wote wa makao ya mfalme.”
Au “jumba la.”
Nusu ya pili ya Novemba na nusu ya kwanza ya Desemba. Angalia Nyongeza B15.
Tnn., “mbegu yake.”