Yeremia 39:1-18

  • Kuanguka kwa Yerusalemu (1-10)

    • Sedekia akimbia kisha akamatwa (4-7)

  • Yeremia atalindwa (11-14)

  • Uhai wa Ebed-meleki utaokolewa (15-18)

39  Katika mwaka wa tisa wa utawala wa Mfalme Sedekia wa Yuda, katika mwezi wa kumi, Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni alikuja Yerusalemu na jeshi lake lote, na kulizingira jiji hilo.+  Katika mwaka wa 11 wa utawala wa Sedekia, mwezi wa nne, siku ya tisa ya mwezi huo, walibomoa sehemu ya ukuta wa jiji.+  Na wakuu wote wa mfalme wa Babiloni wakaingia na kuketi katika Lango la Kati,+ yaani, Nergal-shareza yule Samgari, Nebo-sarsekimu yule Rabsarisi,* Nergal-shareza yule Rabmagi,* na wakuu wengine wote wa mfalme wa Babiloni.  Mfalme Sedekia wa Yuda na wanajeshi wote walipowaona walikimbia,+ wakatoka jijini wakati wa usiku kupitia njia ya bustani ya mfalme, kupitia lango lililokuwa kati ya kuta mbili, nao wakafuata njia inayoelekea Araba.+  Lakini jeshi la Wakaldayo likawafuatia, nao wakamfikia Sedekia katika jangwa tambarare la Yeriko.+ Wakamkamata na kumleta kwa Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni kule Ribla+ katika nchi ya Hamathi,+ ambako alimhukumu.  Mfalme wa Babiloni akaagiza wana wa Sedekia wachinjwe mbele ya macho yake kule Ribla, na mfalme wa Babiloni akaagiza wakuu wote wa Yuda wachinjwe.+  Ndipo akayapofusha macho ya Sedekia, kisha akamfunga kwa pingu za shaba ili ampeleke Babiloni.+  Halafu Wakaldayo wakaiteketeza nyumba ya* mfalme na nyumba za watu,+ nao wakazibomoa kabisa kuta za Yerusalemu.+  Nebuzaradani+ mkuu wa walinzi akawapeleka uhamishoni kule Babiloni watu waliobaki jijini, na wale waliojisalimisha kwake, na yeyote aliyebaki. 10  Lakini Nebuzaradani mkuu wa walinzi aliwaacha katika nchi ya Yuda baadhi ya watu maskini kabisa, wale ambao hawakuwa na chochote. Siku hiyo aliwapatia pia mashamba ya mizabibu na mashamba mengine ili wayalime.*+ 11  Ndipo Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni akamwagiza hivi Nebuzaradani mkuu wa walinzi kumhusu Yeremia: 12  “Mchukue nawe umtunze; usimdhuru, na umpe chochote atakachokuomba.”+ 13  Basi Nebuzaradani mkuu wa walinzi, Nebushazbani yule Rabsarisi,* Nergal-shareza yule Rabmagi,* na wakuu wote wa mfalme wa Babiloni wakawatuma watu 14  wamtoe Yeremia katika Ua wa Walinzi+ na kumkabidhi kwa Gedalia+ mwana wa Ahikamu+ mwana wa Shafani+ ili apelekwe nyumbani kwake. Basi akaishi pamoja na watu wengine. 15  Yeremia alipokuwa amefungiwa katika Ua wa Walinzi,+ neno la Yehova lilimjia likisema: 16  “Nenda umwambie Ebed-meleki+ Mwethiopia, ‘Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: “Ninayatimiza maneno yangu kuhusu jiji hili ili kuleta msiba wala si mema, na siku hiyo utayaona yakitimia.”’ 17  “‘Lakini nitakuokoa siku hiyo,’ asema Yehova, ‘nawe hutatiwa mikononi mwa watu unaowaogopa.’ 18  “‘Kwa maana hakika nitakuokoa, nawe hutakufa kwa upanga. Uhai wako utakuwa* kama nyara,*+ kwa sababu ulinitumaini,’+ asema Yehova.”

Maelezo ya Chini

Tnn., “Nebukadreza,” njia nyingine ya kuandika jina hili.
Au kulingana na mpangilio tofauti wa maandishi ya Kiebrania, “Nergal-shareza, Samgari-nebo, Sarsekimu, Rabsarisi.”
Au “mchawi mkuu (mnajimu).”
Tnn., “Nebukadreza,” njia nyingine ya kuandika jina hili.
Au “jumba la.”
Au labda, “wafanye utumishi wa lazima.”
Tnn., “Nebukadreza,” njia nyingine ya kuandika jina hili.
Au “ofisa mkuu wa makao ya mfalme.”
Au “mchawi mkuu (mnajimu).”
Au “nafsi yako itakuwa.”
Au “Utaponyoka na uhai wako.”