Yeremia 4:1-31

  • Kutubu kunaleta baraka (1-4)

  • Msiba utakuja kutoka kaskazini (5-18)

  • Uchungu wa Yeremia kuhusu msiba unaokuja (19-31)

4  “Ukirudi, Ee Israeli,” asema Yehova,“Ukirudi kwanguNa ukiondoa sanamu zako zenye kuchukiza kutoka mbele zangu,Basi hutakuwa mkimbizi.+   Nawe ukiapa,‘Kwa hakika kama Yehova anavyoishi!’ katika kweli, haki, na uadilifu,Ndipo mataifa yatakapojipatia baraka kupitia yeye,Nayo yatajigamba kwa sababu yake.”+  Kwa maana Yehova anawaambia hivi watu wa Yuda na Yerusalemu: “Jilimieni shamba linalofaa kwa kilimo,Nanyi msiendelee kupanda kati ya miiba.+   Jitahirini kwa ajili ya Yehova,Na kuondoa magovi ya mioyo yenu,+Ninyi watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalemu,Ili ghadhabu yangu isiwake kama motoNa iteketeze bila yeyote wa kuizima,Kwa sababu ya matendo yenu maovu.”+   Tangazeni jambo hilo Yuda, na kulihubiri Yerusalemu. Pazeni sauti na kupiga pembe katika nchi yote.+ Iteni kwa sauti na kusema: “Kusanyikeni pamoja,Nasi tukimbilie katika majiji yenye ngome.+   Inueni ishara* kuelekea Sayuni. Tafuteni kimbilio, na msisimame tuli,” Kwa maana ninaleta msiba kutoka kaskazini,+ kishindo kikubwa.   Ametokea kama simba kutoka kwenye kichaka chake;+Yule anayeyaangamiza mataifa ametoka.+ Ametoka mahali pake ili kuifanya nchi yako kuwa kitu cha kutisha. Majiji yako yatakuwa magofu, bila mkaaji.+   Kwa hiyo, vaeni nguo za magunia,+Ombolezeni* na kupiga mayowe,Kwa sababu hasira ya Yehova inayowaka haijaondoka juu yetu.   “Siku hiyo,” asema Yehova, “mfalme atakufa moyo,*+Pia wakuu watakufa moyo;*Makuhani watashikwa na hofu, nao manabii watashangaa.”+ 10  Kisha nikasema: “Ole wangu, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova! Kwa kweli umewadanganya kabisa watu hawa+ na Yerusalemu, kwa kusema, ‘Mtakuwa na amani,’+ wakati upanga uko kwenye koo zetu.”* 11  Wakati huo watu hawa na Yerusalemu wataambiwa: “Upepo unaokausha kutoka kwenye vilima vitupu vya jangwaniUtavuma juu ya binti ya* watu wangu;Hauji kupepeta wala kusafisha. 12  Upepo unaovuma kwa nguvu zote unatoka sehemu hizo kwa amri yangu. Sasa nitatangaza hukumu dhidi yao. 13  Tazameni! Atakuja kama mawingu ya mvua,Na magari yake ni kama upepo wa dhoruba.+ Farasi wake wanakimbia kwa kasi kuliko tai.+ Ole wetu, kwa sababu tumeangamia! 14  Usafishe moyo wako uwe safi kutokana na uovu, Ee Yerusalemu, ili uokolewe.+ Utafikiria mambo maovu mpaka lini? 15  Kwa maana sauti inaleta habari kutoka Dani,+Nayo inatangaza msiba kutoka kwenye milima ya Efraimu. 16  Tangazeni jambo hilo, naam, kwa mataifa;Litangazeni dhidi ya Yerusalemu.” “Walinzi* wanakuja kutoka nchi ya mbali,Nao watapaza sauti zao dhidi ya majiji ya Yuda. 17  Wanamshambulia kutoka pande zote kama walinzi wa shamba ambalo halijazingirwa na ukuta,+Kwa sababu ameniasi,”+ asema Yehova. 18  “Njia zako mwenyewe na matendo yako yataletwa juu yako.+ Jinsi msiba wako ulivyo mchungu,Kwa maana umefika mpaka moyoni mwako!” 19  Jamani maumivu yangu,* maumivu yangu! Ninahisi uchungu mwingi moyoni mwangu.* Moyo wangu unapigapiga ndani yangu. Siwezi kunyamaza,Kwa maana nimesikia* sauti ya pembe,King’ora cha vita.*+ 20  Msiba baada ya msiba umetangazwa,Kwa maana nchi yote imeharibiwa. Kwa ghafla, mahema yangu mwenyewe yameharibiwa,Kwa muda mfupi, vitambaa vya mahema yangu.+ 21  Nitaendelea kuona ishara* mpaka lini,Na kuendelea kusikia sauti ya pembe?+ 22  Kwa maana watu wangu ni wajinga;+Hawanitambui. Wao ni wana wapumbavu, wasio na uelewaji. Ni werevu* sana katika kutenda maovu,Lakini hawajui kutenda mema. 23  Niliiona nchi, na tazama! ilikuwa tupu na ukiwa.+ Nilitazama mbingu, na nuru yake haikuwepo.+ 24  Niliiona milima, na tazama! ilikuwa ikitetemeka,Na vilima vilikuwa vikitikisika.+ 25  Niliona, na tazama! hapakuwa na mtu yeyote,Na ndege wote wa angani walikuwa wamekimbia.+ 26  Niliona, na tazama! sasa shamba la matunda lilikuwa nyika,Na majiji yake yote yalikuwa yamebomolewa.+ Ilikuwa kwa sababu ya Yehova,Kwa sababu ya hasira yake inayowaka. 27  Kwa maana Yehova anasema hivi: “Nchi yote itaachwa ukiwa,+Lakini sitaiangamiza kabisa. 28  Kwa sababu hiyo nchi itaomboleza,+Na juu mbingu zitakuwa na giza.+ Ni kwa sababu nimesema, nami nimeamua,Nami sitabadili nia yangu,* wala sitaliacha jambo hilo.+ 29  Kwa sababu ya sauti ya wapanda farasi na wapiga-mishale,Jiji zima linakimbia.+ Wanaingia vichakani,Nao wanapanda kwenye miamba.+ Kila jiji linaachwa,Na hakuna mtu anayeishi humo.” 30  Sasa kwa kuwa umeangamizwa, utafanya nini? Ulikuwa ukivaa nguo nyekundu,Ukijipamba kwa mapambo ya dhahabu,Na kupanua macho yako kwa kuyapaka rangi nyeusi.* Lakini ulijirembesha bure,+Kwa maana waliokutamani wamekukataa;Sasa wanataka kukuua.+ 31  Kwa maana nimesikia sauti kama ya mwanamke mgonjwa,Maumivu kama ya mwanamke anayezaa mtoto wake wa kwanza,Sauti ya binti ya Sayuni ambaye anaendelea kuhemahema kwa nguvu. Anasema hivi akiinyoosha mikono yake:+ “Ole wangu, kwa maana nimechoka* kwa sababu ya wauaji!”

Maelezo ya Chini

Au “nguzo ya ishara.”
Au “Pigeni vifua vyenu.”
Au “watakosa ujasiri.”
Au “atakosa ujasiri.”
Au “upanga umefikia nafsi zetu.”
Tashihisi ya kishairi, ambayo labda inaonyesha sikitiko au huruma.
Yaani, wale wanaolitazama jiji ili wajue wakati wa kushambulia.
Tnn., “matumbo yangu.”
Tnn., “katika kuta za moyo wangu.”
Au “nafsi yangu imesikia.”
Au labda, “sauti ya kelele za vita.”
Au “nguzo ya ishara.”
Au “Wana hekima.”
Au “sitaghairi.”
Au “wanja.”
Au “nafsi yangu imechoka.”