Yeremia 43:1-13

  • Watu wakataa kutii kisha waenda Misri (1-7)

  • Neno la Yehova kwa Yeremia nchini Misri (8-13)

43  Yeremia alipomaliza kuwaambia watu wote maneno hayo yote kutoka kwa Yehova Mungu wao, kila neno ambalo Yehova Mungu wao alikuwa amemtuma awaambie,  Azaria mwana wa Hoshaya, Yohanani+ mwana wa Karea, na watu wote wenye kimbelembele wakamwambia Yeremia: “Unasema uwongo! Yehova Mungu wetu hakukutuma useme, ‘Msiende kukaa Misri.’  Lakini Baruku+ mwana wa Neria anakuchochea dhidi yetu ili kututia mikononi mwa Wakaldayo, ili watuue au kutupeleka uhamishoni Babiloni.”+  Basi Yohanani mwana wa Karea na wakuu wote wa jeshi na watu wote hawakuitii sauti ya Yehova kwamba wabaki katika nchi ya Yuda.  Badala yake, Yohanani mwana wa Karea na wakuu wote wa jeshi wakawachukua watu wote wa Yuda waliobaki ambao walikuwa wamerudi kuishi katika nchi ya Yuda kutoka katika mataifa yote ambako walikuwa wametawanywa.+  Wakawachukua wanaume, wanawake, watoto, mabinti wa mfalme, na kila mtu ambaye Nebuzaradani+ mkuu wa walinzi alikuwa amemwacha pamoja na Gedalia+ mwana wa Ahikamu+ mwana wa Shafani,+ na pia nabii Yeremia na Baruku mwana wa Neria.  Nao wakaingia nchini Misri, kwa maana hawakuitii sauti ya Yehova, wakaenda mpaka Tahpanhesi.+  Kisha neno la Yehova likamjia Yeremia huko Tahpanhesi likisema:  “Beba mkononi mwako mawe makubwa, nawe uyafiche katika saruji kwenye ngazi ya matofali iliyo kwenye mlango wa nyumba ya Farao huko Tahpanhesi, huku wanaume Wayahudi wakitazama. 10  Kisha uwaambie, ‘Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: “Tazameni, ninamwita Nebukadneza* mfalme wa Babiloni, mtumishi wangu,+ nami nitakiweka kiti chake cha ufalme juu ya mawe haya ambayo nimeyaficha, naye atalitandaza hema lake la kifalme juu yake.+ 11  Naye ataingia na kuipiga nchi ya Misri.+ Yeyote aliyekusudiwa kufa kwa ugonjwa hatari atakufa kwa ugonjwa hatari, na yeyote aliyekusudiwa kwenda utekwani ataenda utekwani, na yeyote aliyekusudiwa kufa kwa upanga atakufa kwa upanga.+ 12  Nami nitaziwasha moto nyumba za* miungu ya Misri,+ naye ataiteketeza na kuichukua mateka. Atajifunika kwa nchi ya Misri kama mchungaji anavyojifunika kwa vazi lake, naye ataondoka huko kwa amani.* 13  Naye atazivunja vipandevipande nguzo za* Beth-shemeshi* katika nchi ya Misri, naye ataziteketeza kwa moto nyumba za* miungu ya Misri.”’”

Maelezo ya Chini

Tnn., “Nebukadreza,” njia nyingine ya kuandika jina hili.
Au “atayawasha moto mahekalu ya.”
Au “bila madhara.”
Au “minara ya.”
Au “Nyumba (Hekalu la) ya Jua,” yaani, Heliopolisi.
Au “mahekalu ya.”