Yeremia 45:1-5

  • Ujumbe wa Yehova kwa Baruku (1-5)

45  Hili ndilo neno ambalo nabii Yeremia alimwambia Baruku+ mwana wa Neria alipoandika katika kitabu maneno haya aliyoambiwa na Yeremia+ katika mwaka wa nne wa utawala wa Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda:  “Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi kukuhusu wewe, Baruku,  ‘Umesema: “Ole wangu, kwa maana Yehova ameongeza huzuni kwenye maumivu yangu! Nimechoka kwa sababu ya kulia kwa maumivu, nami sijapata mahali pa kupumzika.”’  “Mwambie, ‘Yehova anasema hivi: “Tazama! Kile ambacho nimekijenga ninakibomoa, na kile nilichokipanda ninaking’oa—nchi yote.+  Lakini unajitafutia* mambo makuu. Acha kuyatafuta mambo hayo.”’ “‘Kwa maana, niko karibu kuleta msiba dhidi ya wote wenye mwili,’*+ asema Yehova, ‘na popote utakapoenda, nitakupa uhai wako* kuwa nyara.’”*+

Maelezo ya Chini

Au “unatarajia.”
Au “watu wote.”
Au “nafsi yako.”
Au “nitaacha uponyoke na uhai wako.”