Yeremia 48:1-47

  • Unabii dhidi ya Moabu (1-47)

48  Kuhusu Moabu,+ Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: “Ole wake Nebo,+ kwa maana ameangamizwa! Kiriathaimu+ ameaibishwa na kutekwa. Kimbilio salama limeaibishwa* na kuvunjwavunjwa.+   Hawamsifu tena Moabu. Kule Heshboni wamepanga njama ya kumwangusha:+ ‘Njooni, tumkomeshe asiwe taifa.’ Wewe pia, ewe Madmeni, unapaswa kukaa kimya,Kwa maana upanga unakufuata.   Kuna sauti ya kilio kutoka Horonaimu,+Ya uharibifu na anguko kubwa.   Moabu amevunjwa. Watoto wake wanalia kwa sauti.   Kwenye njia inayopanda kwenda Luhithi wanaendelea kulia huku wakipanda. Na kwenye njia inayoshuka kutoka Horonaimu wanasikia vilio vya taabu kwa sababu ya msiba.+   Kimbieni, okoeni uhai wenu!* Ni lazima muwe kama mberoshi nyikani.   Kwa sababu unatumaini kazi zako na hazina zako,Wewe pia utatekwa. Na Kemoshi+ atapelekwa uhamishoni,Pamoja na makuhani wake na wakuu wake.   Mwangamizaji atakuja katika kila jiji,Na hakuna jiji litakaloponyoka.+ Hakika bonde litaangamia,*Na nchi tambarare itaharibiwa,* kama alivyosema Yehova.   Mwekeeni Moabu alama,Kwa maana atakapoanguka na kuwa magofu atakimbia,Na majiji yake yatakuwa kitu cha kutisha,Bila mkaaji.+ 10  Alaaniwe mtu anayefanya kazi ya Yehova kwa uzembe! Alaaniwe mtu anayeuzuia upanga wake usimwage damu! 11  Wamoabu hawajasumbuliwa tangu ujana wao,Kama divai iliyotulia kwenye machicha. Hawajamiminwa kutoka katika chombo kimoja kwenda kingine,Nao hawajawahi kamwe kupelekwa uhamishoni. Ndiyo sababu ladha yao imebaki vilevile,Na harufu yao haijabadilika. 12  “‘Kwa hiyo tazama! siku zinakuja,’ asema Yehova, ‘nitakapowatuma watu wawapindue. Watawapindua na kumwaga kabisa kile kilicho ndani ya vyombo vyao, nao wataivunja mitungi yao mikubwa vipandevipande. 13  Na Wamoabu wataona aibu kwa sababu ya Kemoshi, kama watu wa nyumba ya Israeli walivyoona aibu kwa sababu ya Betheli, iliyokuwa tegemeo lao.+ 14  Mnawezaje kuthubutu kusema: “Sisi ni mashujaa hodari, walio tayari kwa vita”?’+ 15  ‘Moabu ameangamizwa,Majiji yake yamevamiwa,+Na vijana wao walio bora wamechinjwa,’+ Asema Mfalme, ambaye jina lake ni Yehova wa majeshi.+ 16  Msiba wa Wamoabu unakuja hivi karibuni,Na anguko lao linakaribia upesi.+ 17  Wote wanaowazunguka watawasikitikia,Wote wanaolijua jina lao. Waambieni hivi: ‘Jinsi fimbo yenye nguvu ilivyovunjwa, fimbo ya urembo!’ 18  Shuka chini kutoka kwenye utukufu wako,Nawe uketi katika kiu,* ewe binti unayekaa Diboni,+Kwa maana mwangamizaji wa Moabu amekuja kukushambulia,Ataziharibu sehemu zako zenye ngome.+ 19  Simama kando ya barabara utazame, wewe mkaaji wa Aroeri.+ Muulize mwanamume anayekimbia na mwanamke anayeponyoka. ‘Ni nini ambacho kimetokea?’ 20  Moabu ameaibishwa na kushikwa na hofu. Omboleza na ulie kwa sauti. Tangazeni kule Arnoni+ kwamba Moabu ameangamizwa. 21  “Hukumu imekuja kwenye nchi tambarare,*+ dhidi ya Holoni, Yahazi,+ na Mefaathi;+ 22  dhidi ya Diboni,+ Nebo,+ na Beth-diblathaimu; 23  dhidi ya Kiriathaimu,+ Beth-gamuli, na Beth-meoni;+ 24  dhidi ya Keriothi+ na Bosra; na dhidi ya majiji yote ya nchi ya Moabu, yaliyo mbali na yaliyo karibu. 25  ‘Nguvu za* Moabu zimekatwa;Na mkono wake umevunjwa,’ asema Yehova. 26  ‘Mlewesheni,+ kwa maana amejikweza dhidi ya Yehova.+ Moabu anagaagaa katika matapishi yake,Naye ni kitu cha kudhihakiwa. 27  Je, kwako Israeli hakuwa kitu cha kudhihakiwa?+ Je, alipatikana kati ya wezi,Hivi kwamba utikise kichwa chako na kumshutumu? 28  Ondokeni katika majiji, mkae kwenye jabali, ninyi wakaaji wa Moabu,Na muwe kama njiwa anayejenga kiota kwenye kuta za korongo.’” 29  “Tumesikia kuhusu kiburi cha Moabu—ana majivuno sana—Kuhusu kujisifu kwake, kiburi chake, majivuno yake, na jinsi moyo wake ulivyotutumuka.”+ 30  “‘Ninajua ghadhabu yake,’ asema Yehova,‘Lakini maneno yake matupu yatakuwa ya bure. Hayatafanya chochote. 31  Ndiyo sababu nitaiombolezea Moabu,Nitalia kwa sauti kwa ajili ya Moabu yoteNa kuwaombolezea wanaume wa Kir-heresi.+ 32  Nitakulilia kwa kilio kinachoshinda kilio cha Yazeri,+Nitakulilia, ewe mzabibu wa Sibma.+ Machipukizi yako yanayositawi yamevuka bahari. Yamefika mpaka baharini, mpaka Yazeri. Mwangamizaji ameshuka kwenyeMatunda yako ya wakati wa kiangazi na mavuno yako ya zabibu.+ 33  Furaha na shangwe vimeondolewa katika shamba la matundaNa katika nchi ya Moabu.+ Nimefanya divai iache kutiririka kutoka kwenye shinikizo la divai. Hakuna mtu atakayelikanyaga shinikizo la divai kwa vigelegele vya shangwe. Watapaza sauti lakini si kwa shangwe.’”+ 34  “‘Kuna kilio kikubwa kutoka Heshboni+ mpaka Eleale.+ Wanapaza sauti yao mpaka Yahazi,+Kutoka Soari mpaka Horonaimu,+ mpaka Eglath-shelishiya. Hata maji ya Nimrimu yatabaki ukiwa.+ 35  Nitamwondoa kabisa katika Moabu,’ asema Yehova,‘Mtu anayeleta toleo mahali pa juuNa mtu anayemtolea dhabihu mungu wake. 36  Ndiyo sababu moyo wangu utaiombolezea* Moabu kama filimbi,*+Na moyo wangu utawaombolezea* wanaume wa Kir-heresi kama filimbi.* Kwa kuwa utajiri aliopata utaangamia. 37  Kwa maana kila kichwa kina upara,+Na ndevu zote zimenyolewa. Kila mkono umekatwakatwa,+Nao wamevaa nguo za magunia kiunoni!’”+ 38  “‘Juu ya paa zote za MoabuNa katika viwanja vyake vyote vya jiji,Hakuna kitu kingine ila maombolezo. Kwa maana nimemvunja MoabuKama chombo kilichotupwa,’ asema Yehova. 39  ‘Jinsi alivyo na hofu! Ombolezeni! Jinsi Moabu alivyougeuza mgongo wake kwa aibu! Moabu amekuwa kitu cha kudhihakiwa,Kitu cha kutisha kwa wote wanaomzunguka.’” 40  “Kwa maana Yehova anasema hivi: ‘Tazama! Kama tai anayeshuka chini kwa ghafla,+Atanyoosha mabawa yake juu ya Moabu.+ 41  Miji itatekwa,Na ngome zake zitachukuliwa. Siku hiyo moyo wa mashujaa wa MoabuUtakuwa kama moyo wa mwanamke anayezaa.’” 42  “‘Na Moabu ataangamizwa asiwe taifa,+Kwa maana amejikweza dhidi ya Yehova.+ 43  Hofu na shimo na mtego viko mbele yako,Ewe mkaaji wa Moabu,’ asema Yehova. 44  ‘Yeyote anayekimbia hofu ataanguka shimoni,Na yeyote anayetoka shimoni atanaswa na mtego.’ ‘Kwa maana nitawaletea watu wa Moabu mwaka wao wa adhabu,’ asema Yehova. 45  ‘Katika kivuli cha Heshboni, wale wanaokimbia wanasimama wakiwa wameishiwa na nguvu. Kwa maana moto utatoka HeshboniNa mwali wa moto utatoka katikati ya Sihoni.+ Utateketeza kabisa paji la uso wa MoabuNa fuvu la wana wa ghasia.’+ 46  ‘Ole wako, ewe Moabu! Watu wa Kemoshi+ wameangamia. Kwa maana wana wako wamechukuliwa mateka,Na mabinti zako wamepelekwa uhamishoni.+ 47  Lakini siku za mwisho nitawakusanya watu wa Moabu waliotekwa,’ asema Yehova. ‘Hukumu ya Moabu imefikia hapa.’”+

Maelezo ya Chini

Au “Kilele salama kimeaibishwa.”
Au “nafsi zenu.”
Au “nchi tambarare ya chini itaangamia.”
Au “uwanda utaharibiwa.”
Au labda, “kwenye ardhi kavu.”
Au “uwanda.”
Tnn., “Pembe ya.”
Yaani, filimbi iliyopigwa wakati wa kuomboleza kwenye mazishi.
Au “utakuwa na msukosuko kwa ajili ya.”
Yaani, filimbi iliyopigwa wakati wa kuomboleza kwenye mazishi.
Au “utakuwa na msukosuko kwa ajili ya.”