Yeremia 49:1-39

  • Unabii dhidi ya Amoni (1-6)

  • Unabii dhidi ya Edomu (7-22)

    • Nchi ya Edomu haitakuwa taifa tena (17, 18)

  • Unabii dhidi ya Damasko (23-27)

  • Unabii dhidi ya Kedari na Hasori (28-33)

  • Unabii dhidi ya Elamu (34-39)

49  Kuhusu Waamoni,+ Yehova anasema hivi: “Je, Israeli hana wana: Je, hana mrithi? Kwa nini Malkamu+ amemiliki Gadi?+ Na kwa nini watu wake wanaishi katika majiji ya Israeli?”   “‘Kwa hiyo tazameni! siku zinakuja,’ asema Yehova,‘Nitakapofanya king’ora cha vita kisikike* dhidi ya jiji la Raba+ la Waamoni.+ Atakuwa kilima chenye ukiwa,Na miji yake itawashwa moto.’ ‘Na Israeli atawamiliki wale walioichukua nchi yake,’+ asema Yehova.   ‘Omboleza, ewe Heshboni, kwa maana Ai ameharibiwa! Lieni kwa sauti, enyi miji ya Raba. Vaeni nguo za magunia. Ombolezeni na mzungukezunguke kati ya mazizi ya mawe,*Kwa maana Malkamu atapelekwa uhamishoni,Pamoja na makuhani wake na wakuu wake.+   Kwa nini unajigamba kuhusu mabonde,*Kuhusu eneo lako tambarare linalotiririka, ewe binti usiye mwaminifu,Unayezitumaini hazina zakoNa unayesema: “Ni nani atakayenishambulia?”’”   “‘Tazama, ninakuletea jambo la kutisha,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi,‘Kutoka kwa wale wote wanaokuzunguka. Utatawanywa kila upande,Na hakuna atakayewakusanya wale wanaokimbia.’”   “‘Lakini baadaye nitawakusanya Waamoni waliotekwa,’ asema Yehova.”  Kuhusu Edomu, Yehova wa majeshi anasema hivi: “Je, hakuna tena hekima yoyote huko Temani?+ Je, ushauri mzuri umetoweka kwa wale walio na uelewaji? Je, hekima yao imeoza?   Kimbieni, geukeni! Nendeni mkakae katika sehemu za chini zenye kina, enyi wakaaji wa Dedani!+ Kwa maana nitamletea Esau msibaWakati wangu wa kumkazia fikira utakapofika.   Ikiwa wavunaji wa zabibu wangekuvamia,Je, hawangeacha zabibu chache za kuokotwa? Kama wezi wangekuja usiku,Wangesababisha uharibifu kadiri wapendavyo.+ 10  Lakini nitamvua Esau awe uchi. Nitafichua maficho yake,Ili asiweze kujificha. Watoto wake na ndugu zake na majirani zake wataangamizwa,+Naye hatakuwepo tena.+ 11  Waache mayatima wako,Nami nitawahifadhi hai,Na wajane wako watanitumaini.” 12  Kwa maana Yehova anasema hivi: “Tazama! Ikiwa wale ambao hawajahukumiwa kunywa kikombe lazima wakinywe, je, wewe utaachwa kabisa bila kuadhibiwa? Hutaachwa bila kuadhibiwa, kwa maana lazima ukinywe.”+ 13  “Kwa maana nimeapa kwa nafsi yangu mwenyewe,” asema Yehova, “kwamba Bosra litakuwa kitu cha kutisha,+ shutuma, uharibifu, na laana; na majiji yake yote yatakuwa magofu ya kudumu.”+ 14  Nimesikia habari kutoka kwa Yehova,Mjumbe ametumwa kati ya mataifa aseme hivi: “Jikusanyeni pamoja na mumshambulie;Jitayarisheni ili kupigana.”+ 15  “Kwa maana tazama! Nimekufanya uwe mdogo sana kati ya mataifa,Umedharauliwa kati ya wanadamu.+ 16  Mtetemeko uliosababisha umekudanganya,Kimbelembele cha moyo wako,Ewe unayekaa katika mapango ya jabali,Unayekaa kwenye kilima kirefu zaidi. Ingawa unajenga kiota chako juu kama tai,Nitakushusha chini kutoka huko,” asema Yehova. 17  “Na lazima Edomu awe kitu cha kutisha.+ Kila mtu anayepita kando yake atatazama kwa hofu na kupiga mluzi kwa sababu ya mapigo yake yote. 18  Kama Sodoma na Gomora na miji jirani ilivyoangamizwa,”+ Yehova anasema, “hakuna mtu atakayekaa huko, na hakuna mtu atakayeishi huko.+ 19  “Tazameni! Kama simba anayetoka kwenye vichaka+ vikubwa kando ya Yordani, mtu fulani atayashambulia malisho yaliyo salama, lakini kwa muda mfupi nitamfanya Edomu akimbie kutoka nchini. Nami nitaweka juu ya nchi hiyo yule aliyechaguliwa. Kwa maana ni nani aliye kama mimi, na ni nani atakayenipinga? Ni mchungaji gani anayeweza kusimama mbele zangu?+ 20  Kwa hiyo sikieni, enyi watu, uamuzi ambao* Yehova amefanya dhidi ya Edomu na mawazo yake dhidi ya wakaaji wa Temani:+ Hakika walio wadogo katika kundi watakokotwa. Atayafanya makao yao yawe ukiwa kwa sababu yao.+ 21  Dunia imetetemeka kwa sauti ya kuanguka kwao. Kuna kilio kikubwa! Sauti imesikika mpaka kwenye Bahari Nyekundu.+ 22  Tazameni! Atateremka na kushuka kwa ghafla kama tai,+Naye atanyoosha mabawa yake juu ya Bosra.+ Siku hiyo moyo wa mashujaa wa EdomuUtakuwa kama moyo wa mwanamke anayezaa.” 23  Kuhusu Damasko:+ “Hamathi+ na Arpadi wameaibishwa,Kwa maana wamesikia habari mbaya. Wanayeyuka kwa woga. Kuna msukosuko baharini ambao hauwezi kutulizwa. 24  Damasko amekufa moyo. Amegeuka ili kukimbia, lakini ameshikwa na hofu. Amepatwa na taabu na uchungu,Kama mwanamke anayezaa. 25  Kwa nini jiji lenye sifa halijaachwa,Mji wa furaha? 26  Kwa maana vijana wake wataanguka katika viwanja vyake vya jiji,Na wanajeshi wote wataangamia siku hiyo,” asema Yehova wa majeshi. 27  “Nitauwasha moto ukuta wa Damasko,Nao utaiteketeza kabisa minara yenye ngome ya Ben-hadadi.”+ 28  Kuhusu Kedari+ na falme za Hasori, ambazo Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni alizishambulia na kuzishinda, Yehova anasema hivi: “Inukeni, pandeni mwende Kedari,Na muwaangamize wana wa Mashariki. 29  Mahema yao na mifugo yao itachukuliwa,Vitambaa vyao vya mahema na mali zao zote. Ngamia wao watachukuliwa,Nao watawalilia, ‘Kuna hofu kila mahali!’” 30  “Kimbieni, nendeni mbali sana! Nendeni mkae katika sehemu za chini zenye kina, enyi wakaaji wa Hasori,” asema Yehova. “Kwa maana Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni ametunga mbinu dhidi yenu,Naye amefanya mpango wa kuwashambulia.” 31  “Inukeni, shambulieni taifa lililo na amani,Linalokaa kwa usalama!” asema Yehova. “Halina milango wala makomeo; wanaishi peke yao. 32  Ngamia wao wataporwa,Na mifugo yao mingi itakuwa nyara. Nitawatawanya kwa kila upepo,*Wale ambao wananyoa nywele pembeni mwa vichwa vyao,+Nami nitaleta msiba wao kutoka kila upande,” asema Yehova. 33  “Na Hasori atakuwa pango la mbwamwitu,Ukiwa wa kudumu. Hakuna mtu atakayekaa huko,Na hakuna mtu atakayeishi ndani yake.” 34  Hili ndilo neno la Yehova lililomjia nabii Yeremia kuhusu Elamu+ mwanzoni mwa utawala wa Mfalme Sedekia+ wa Yuda: 35  “Yehova wa majeshi anasema hivi: ‘Ninauvunja upinde wa Elamu,+ chanzo cha* nguvu zao. 36  Nitaleta juu ya Elamu zile pepo nne kutoka kwenye miisho minne ya mbingu, nami nitawatawanya kwenye pepo hizi zote. Hakuna taifa ambako watu wa Elamu waliotawanywa hawataenda.’” 37  “Nitawavunjavunja Waelamu mbele ya maadui wao na mbele ya wale wanaotaka kuwaua; nami nitawaletea msiba, hasira yangu inayowaka,” asema Yehova. “Nami nitautuma upanga uwafuate mpaka nitakapowaangamiza kabisa.” 38  “Nami nitaweka kiti changu cha ufalme huko Elamu,+ na huko nitamwangamiza mfalme na wakuu,” asema Yehova. 39  “Lakini siku za mwisho, nitawakusanya watu wa Elamu waliotekwa,” asema Yehova.

Maelezo ya Chini

Au labda, “kelele za vita zisikike.”
Au “mazizi ya kondoo.”
Au “maeneo tambarare ya chini.”
Au “shauri ambalo.”
Tnn., “Nebukadreza,” njia nyingine ya kuandika jina hili.
Tnn., “Nebukadreza,” njia nyingine ya kuandika jina hili.
Au “kila upande.”
Tnn., “mwanzo wa.”