Yeremia 50:1-46

  • Unabii dhidi ya Babiloni (1-46)

    • Kimbieni kutoka Babiloni (8)

    • Watu wa Israeli watarudishwa (17-19)

    • Maji ya Babiloni yatakaushwa kabisa (38)

    • Babiloni halitakaliwa tena (39, 40)

50  Neno ambalo Yehova alisema kuhusu Babiloni,+ kuhusu nchi ya Wakaldayo, kupitia nabii Yeremia:   “Semeni jambo hili kati ya mataifa na mlitangaze. Inueni ishara* na mlitangaze. Msifiche jambo lolote! Semeni, ‘Babiloni ametekwa.+ Beli ameaibishwa.+ Merodaki ameshikwa na hofu. Sanamu zake zimeaibishwa. Sanamu zake zinazochukiza* zimeshikwa na hofu.’   Kwa maana taifa limemshambulia kutoka kaskazini.+ Linaifanya nchi yake kuwa kitu cha kutisha;Hakuna mtu anayekaa ndani yake. Mwanadamu na pia mnyama wamekimbia;Wameenda zao.”  “Siku hizo na wakati huo,” asema Yehova, “watu wa Israeli na watu wa Yuda watakuja pamoja.+ Watatembea wakilia,+ na pamoja watamtafuta Yehova Mungu wao.+  Watauliza njia ya kwenda Sayuni, nyuso zao zikiwa zimeelekezwa upande huo,+ wakisema, ‘Njooni, tujiunge na Yehova katika agano la milele ambalo halitasahauliwa.’+  Watu wangu wamekuwa kundi la kondoo waliopotea.+ Wachungaji wao wenyewe waliwafanya wapotee.+ Waliwapeleka kwenye milima, wakitangatanga kutoka mlima mpaka kilima. Wamepasahau mahali pao pa kupumzika.  Wale wote wanaowapata wamewanyafua,+ na maadui wao wamesema, ‘Hatuna hatia, kwa sababu walimtendea dhambi Yehova, walimtendea dhambi Yehova ambaye ni makao ya uadilifu na tumaini la mababu zao.’”   “Kimbieni kutoka Babiloni,Tokeni katika nchi ya Wakaldayo,+Na muwe kama wanyama wanaolitangulia kundi.   Kwa maana sasa ninaamsha na kuleta dhidi ya BabiloniKusanyiko la mataifa makubwa kutoka katika nchi ya kaskazini.+ Watamshambulia wakiwa wamejipanga kivita;Kutoka hapo atatekwa. Mishale yao ni kama ya shujaaInayosababisha wazazi wafiwe na watoto;+Hairudi bila matokeo. 10  Ukaldayo itakuwa nyara.+ Wale wote wanaochukua nyara kutoka kwake watashiba kabisa,”+ asema Yehova. 11  “Kwa maana mliendelea kushangilia,+ mliendelea kufurahiMlipokuwa mkiupora urithi wangu mwenyewe.+ Kwa maana mliendelea kukanyagakanyaga kama ndama jike kwenye nyasi,Nanyi mkaendelea kulia kama farasi dume. 12  Mama yenu ameaibishwa.+ Yule aliyewazaa amekata tamaa. Tazameni! Yeye ndiye mdogo zaidi kati ya mataifa,Nyika isiyo na maji na ambayo ni jangwa.+ 13  Kwa sababu ya ghadhabu ya Yehova hatakaliwa;+Atakuwa ukiwa kabisa.+ Yeyote anayepita kando ya Babiloni atatazama kwa hofuNa kupiga mluzi kwa sababu ya mapigo yake yote.+ 14  Mshambulieni Babiloni mkiwa mmejipanga kivita kila upande,Ninyi nyote mnaoupinda* upinde. Mpigeni mishale, msiuache mshale wowote,+Kwa maana amemtendea dhambi Yehova.+ 15  Mpigieni kelele za vita kila upande. Amejisalimisha.* Nguzo zake zimeanguka, kuta zake zimebomolewa,+Kwa maana ni kisasi cha Yehova.+ Jilipizieni kisasi dhidi yake. Mtendeeni kama alivyotenda.+ 16  Mkatilieni mbali mpandaji wa mbegu kutoka BabiloniNa yule anayebeba mundu wakati wa mavuno.+ Kwa sababu ya upanga ulio katili, kila mtu atarudi kwa watu wake mwenyewe,Kila mtu atakimbilia nchi yake mwenyewe.+ 17  “Watu wa Israeli ni kondoo+ waliotawanyika. Simba wamewatawanya.+ Kwanza mfalme wa Ashuru aliwanyafua;+ kisha Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni akaguguna mifupa yao.+ 18  Kwa hiyo Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Nitamtendea mfalme wa Babiloni na nchi yake kama nilivyomtendea mfalme wa Ashuru.+ 19  Nami nitamrudisha Israeli kwenye malisho yake,+ naye atalisha juu ya Karmeli na juu ya Bashani,+ naye atashiba kwenye milima ya Efraimu+ na ya Gileadi.’”+ 20  “Siku hizo na wakati huo,” asema Yehova,“Hatia ya Israeli itatafutwa,Lakini hakutakuwa na hatia yoyote,Na dhambi za Yuda hazitapatikana,Kwa maana nitawasamehe wale nitakaowaacha wabaki.”+ 21  “Panda ukashambulie nchi ya Merathaimu na wakaaji wa Pekodi.+ Acha wauawe na kuangamizwa* kabisa,” asema Yehova. “Fanya yote niliyokuamuru. 22  Kuna sauti ya vita nchini,Msiba mkubwa. 23  Jinsi nyundo ya chuma ya dunia yote ilivyokatwa na kuvunjwa!+ Jinsi ambavyo Babiloni amekuwa kitu cha kutisha kati ya mataifa!+ 24  Nimekutegea mtego, nawe umenaswa, Ee Babiloni,Nawe hukujua. Ulipatikana na kukamatwa,+Kwa maana ulimpinga Yehova. 25  Yehova amefungua ghala lake,Naye anatoa silaha za ghadhabu yake.+ Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi, ana kaziKatika nchi ya Wakaldayo. 26  Mshambulieni kutoka sehemu za mbali.+ Fungueni maghala yake.+ Mrundikeni kama marundo ya nafaka. Mwangamizeni kabisa.+ Naye asiwe na mtu yeyote anayebaki. 27  Waueni ng’ombe dume wake wote wachanga;+Na washuke kwenda machinjioni. Ole wao, kwa maana siku yao imefika,Wakati wao wa kuadhibiwa!* 28  Kuna sauti ya wale wanaokimbia,Wale wanaoponyoka kutoka nchi ya Babiloni,Ili kutangaza katika Sayuni kisasi cha Yehova Mungu wetu,Kisasi kwa ajili ya hekalu lake.+ 29  Waiteni wapiga-mishale dhidi ya Babiloni,Wote wanaoupinda* upinde.+ Pigeni kambi kumzunguka; msiache yeyote aponyoke. Mlipeni kulingana na matendo yake.+ Mtendeeni kama alivyotenda,+Kwa maana ametenda kwa kiburi dhidi ya Yehova,Dhidi ya Mtakatifu wa Israeli.+ 30  Basi vijana wake wataanguka katika viwanja vyake vya jiji,+Na wanajeshi wake wote wataangamia* siku hiyo,” asema Yehova. 31  “Tazama! Niko dhidi yako,+ ewe mkaidi,”+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi,“Kwa maana lazima siku yako itakuja, wakati ambapo nitakufanya uwajibike.* 32  Wewe, ewe mkaidi, utajikwaa na kuanguka,Hakutakuwa na mtu wa kukuinua.+ Nami nitayawasha moto majiji yako,Nao utateketeza kabisa kila kitu kinachokuzunguka.” 33  Yehova wa majeshi anasema hivi: “Watu wa Israeli na Yuda wamekandamizwa,Na wale wote wanaowachukua mateka wamewazuilia.+ Wamekataa kuwaachilia waende.+ 34  Lakini Mkombozi wao ana nguvu.+ Yehova wa majeshi ndilo jina lake.+ Bila shaka atatetea kesi yao,+Ili kuipumzisha nchi+Na kuwafadhaisha wakaaji wa Babiloni.”+ 35  “Kuna upanga dhidi ya Wakaldayo,” asema Yehova,“Dhidi ya wakaaji wa Babiloni na dhidi ya wakuu wake na dhidi ya watu wake wenye hekima.+ 36  Kuna upanga dhidi ya wale wanaoongea maneno matupu,* nao watatenda kipumbavu. Kuna upanga dhidi ya mashujaa wake, nao watashikwa na hofu.+ 37  Kuna upanga dhidi ya farasi wao na magari yao ya vita,Na dhidi ya watu wa mataifa mbalimbali waliochangamana nao,Nao watakuwa kama wanawake.+ Kuna upanga dhidi ya hazina zake, nazo zitaporwa.+ 38  Kuna uharibifu dhidi ya maji yake, nayo yatakaushwa.+ Kwa maana ni nchi ya sanamu za kuchongwa,+Na kwa sababu ya maono yao yanayotisha wanaendelea kutenda kiwazimu. 39  Kwa hiyo, viumbe wa jangwani watakaa pamoja na wanyama wanaopiga mayowe,Na mbuni watakaa ndani yake.+ Hakutakuwa na wakaaji tena ndani yake,Wala watu hawataishi humo kwa vizazi vyote.”+ 40  “Kama Mungu alivyoangamiza Sodoma na Gomora+ na miji jirani,”+ asema Yehova, “hakuna mtu atakayekaa huko, na hakuna mtu atakayeishi huko.+ 41  Tazama! Watu wanakuja kutoka kaskazini;Taifa kubwa na wafalme wakuu+ watainuliwaKutoka sehemu za mbali zaidi za dunia.+ 42  Wanatumia upinde na mkuki.+ Ni wakatili na hawataonyesha rehema.+ Sauti yao ni kama bahari inayovuma,+Wakiwa wamepanda farasi wao. Wamejipanga kivita kama mtu mmoja dhidi yako, ewe binti ya Babiloni.+ 43  Mfalme wa Babiloni amesikia habari kuwahusu,+Na mikono yake imelegea.+ Amepata maumivu,Uchungu kama wa mwanamke anayezaa. 44  “Tazama! Kama simba anayetoka kwenye vichaka vikubwa kando ya Yordani, mtu fulani atayashambulia malisho yaliyo salama, lakini kwa muda mfupi nitawafanya Waedomu wakimbie kutoka nchini. Nami nitaweka juu ya nchi hiyo yule aliyechaguliwa.+ Kwa maana ni nani aliye kama mimi, na ni nani atakayenipinga? Ni mchungaji gani anayeweza kusimama mbele zangu?+ 45  Kwa hiyo sikieni, enyi watu, uamuzi ambao* Yehova amefanya dhidi ya Babiloni+ na mawazo yake dhidi ya nchi ya Wakaldayo. Hakika walio wadogo katika kundi watakokotwa. Atayafanya makao yao yabaki ukiwa kwa sababu yao.+ 46  Sauti ya kutekwa kwa Babiloni itafanya dunia itetemeke,Na kilio kitasikika kati ya mataifa.”+

Maelezo ya Chini

Au “nguzo ya ishara.”
Huenda neno la Kiebrania linahusiana na neno “mavi,” nalo hutumiwa kuonyesha dharau.
Tnn., “mnaoukanyaga.”
Tnn., “Amempa mkono wake.”
Tnn., “Nebukadreza,” njia nyingine ya kuandika jina hili.
Au “uwaangamize.”
Au “kuwajibishwa.”
Tnn., “wanaoukanyaga.”
Tnn., “watanyamazishwa.”
Au “wakati ambao nitakuadhibu.”
Au “manabii wa uwongo.”
Au “shauri ambalo.”