Yeremia 51:1-64

  • Unabii dhidi ya Babiloni (1-64)

    • Babiloni litashindwa ghafla na Wamedi (8-12)

    • Kitabu chatupwa ndani ya Mto Efrati (59-64)

51  Yehova anasema hivi: “Tazameni, ninaleta upepo unaoharibuDhidi ya Babiloni+ na dhidi ya wakaaji wa Leb-kamai.*   Nitawatuma wapepetaji Babiloni,Nao watampepeta na kuifanya nchi yake kuwa tupu;Watamshambulia kutoka pande zote siku ya msiba.+   Anayepiga mishale asiupinde* upinde wake. Na yeyote asisimame akiwa amevaa koti lake la vita. Msiwahurumie vijana wake.+ Angamizeni jeshi lake lote.   Nao watauawa katika nchi ya Wakaldayo,Wakiwa wamechomwa kwa silaha katika barabara zake.+   Kwa maana Mungu wa Israeli na Yuda, Yehova wa majeshi, hajawaacha wakiwa wajane.+ Lakini nchi yao* imejaa hatia machoni pa Mtakatifu wa Israeli.   Kimbieni kutoka Babiloni,Kimbieni ili mwokoe uhai wenu.*+ Msiangamie kwa sababu ya kosa lake. Kwa maana ni wakati wa kisasi cha Yehova. Anamlipa kulingana na matendo yake.+   Babiloni amekuwa kikombe cha dhahabu mkononi mwa Yehova;Aliilewesha dunia yote. Mataifa yamekunywa divai yake;+Ndiyo sababu mataifa yameshikwa na wazimu.+   Babiloni ameanguka ghafla, naye amevunjika.+ Mwombolezeeni!+ Leteni zeri kwa ajili ya maumivu yake; labda atapona.”   “Tulijaribu kumponya Babiloni, lakini hakupona. Mwacheni, twendeni kila mmoja kwenye nchi yake.+ Kwa maana hukumu yake imefika mbinguni;Iko juu kama mawingu.+ 10  Yehova ametutendea haki.+ Njooni, tusimulie katika Sayuni kazi ya Yehova Mungu wetu.”+ 11  “Isugueni mishale;+ chukueni ngao za mviringo.* Yehova ameichochea roho ya wafalme wa Wamedi,+Kwa sababu anakusudia kuiangamiza Babiloni. Kwa maana hiki ndicho kisasi cha Yehova, kisasi kwa ajili ya hekalu lake. 12  Inueni ishara*+ dhidi ya kuta za Babiloni. Imarisheni ulinzi, wekeni walinzi. Watayarisheni wale wanaovizia. Kwa maana Yehova ametunga mbinu,Naye atatekeleza alichoahidi dhidi ya wakaaji wa Babiloni.”+ 13  “Ewe mwanamke unayekaa juu ya maji mengi,+Mwenye hazina nyingi,+Mwisho wako umefika, kikomo* chako cha kupata faida.+ 14  Yehova wa majeshi ameapa kwa nafsi yake,‘Nitakujaza wanaume wengi kama nzige,Nao watapiga kelele za ushindi juu yako.’+ 15  Yeye ndiye Muumba wa dunia kwa nguvu zake,Yule aliyeiimarisha ardhi inayozaa kwa hekima yake+Na aliyezitandaza mbingu kwa uelewaji wake.+ 16  Anapofanya sauti yake isikike,Maji yaliyo mbinguni huwa na msukosuko,Naye huyafanya mawingu yapande* kutoka kwenye miisho ya dunia. Hutengeneza radi* kwa ajili ya mvua,Naye huutoa upepo katika maghala yake.+ 17  Kila mtu anatenda bila kutumia akili na bila ujuzi. Kila fundi wa chuma ataaibishwa kwa sababu ya sanamu ya kuchongwa;+Kwa maana sanamu yake ya chuma* ni uwongo,Nazo hazina roho* ndani yake.+ 18  Sanamu hizo ni udanganyifu,*+ kazi ya mzaha. Siku yao ya hukumu itakapofika, zitaangamia. 19  Fungu la Yakobo si kama vitu hivyo,Kwa maana Yeye ndiye aliyeumba kila kitu,Hata fimbo ya urithi wake.+ Yehova wa majeshi ndilo jina lake.”+ 20  “Wewe ni rungu langu la vita, silaha ya vita,Kwa maana nitakutumia kuyavunjavunja mataifa. Nitakutumia kuziangamiza falme. 21  Nitakutumia kumvunjavunja farasi na mpandaji wake. Nitakutumia kulivunjavunja gari la vita na mwendeshaji wake. 22  Nitakutumia kumvunjavunja mwanamume na mwanamke. Nitakutumia kumvunjavunja mzee na mvulana. Nitakutumia kumvunjavunja mwanamume na mwanamke kijana. 23  Nitakutumia kumvunjavunja mchungaji na mifugo yake. Nitakutumia kumvunjavunja mkulima na kundi lake la wanyama. Nitakutumia kuwavunjavunja magavana na watawala wasaidizi. 24  Nami nitamlipa Babiloni na wakaaji wote wa UkaldayoKwa sababu ya uovu wote ambao wametenda huko Sayuni mbele ya macho yenu,”+ asema Yehova. 25  “Tazama, niko dhidi yako,+ ewe mlima wa uharibifu,” asema Yehova,“Wewe unayeiharibu dunia yote.+ Nitaunyoosha mkono wangu dhidi yako na kukubingirisha kutoka kwenye majabaliNa kukufanya uwe mlima ulioteketezwa kabisa.” 26  “Watu hawatachukua kutoka kwako jiwe la pembeni wala jiwe la msingi,Kwa sababu utabaki ukiwa milele,”+ asema Yehova. 27  “Inueni ishara* katika nchi.+ Pigeni pembe kati ya mataifa. Wekeni* mataifa ya kumshambulia. Iteni dhidi yake falme za Ararati,+ Mini, na Ashkenazi.+ Wekeni juu yake ofisa mwandikishaji. Wafanyeni farasi waje kama nzige wenye miiba. 28  Wekeni* mataifa ya kumshambulia,Wafalme wa Umedi,+ magavana wake na watawala wake wote wasaidiziNa nchi zote wanazozitawala. 29  Nayo dunia itatetemeka na kutikisika,Kwa maana mawazo ya Yehova dhidi ya Babiloni yatatekelezwaIli kuifanya nchi ya Babiloni kuwa kitu cha kutisha, bila mkaaji.+ 30  Mashujaa wa Babiloni wameacha kupigana. Wanaketi kwenye ngome zao. Nguvu zao zimekwisha.+ Wamekuwa kama wanawake.+ Nyumba zake zimewashwa moto. Makomeo yake yamevunjwa.+ 31  Mleta habari mmoja anakimbia kukutana na mleta habari mwingine,Na mjumbe mmoja kukutana na mjumbe mwingine,Ili kumjulisha mfalme wa Babiloni kwamba jiji lake limetekwa kila upande,+ 32  Kwamba vivuko vimetekwa,+Kwamba mashua za mafunjo zimeteketezwa kwa moto,Na kwamba wanajeshi wana hofu.” 33  Kwa maana Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: “Binti ya Babiloni ni kama uwanja wa kupuria. Ni wakati wa kumkanyagia chini awe mgumu. Hivi karibuni wakati wake wa mavuno utafika.” 34  “Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni ameninyafua;+Amenivuruga. Ameniweka chini kama chombo kitupu. Amenimeza kama nyoka mkubwa;+Amelijaza tumbo lake kwa vitu vyangu vizuri. Amenioshea mbali. 35  ‘Babiloni na alipizwe kwa sababu ya ukatili niliotendewa mimi na mwili wangu!’ asema mkaaji wa Sayuni.+ ‘Na wakaaji wa Ukaldayo na walipizwe kwa sababu ya damu yangu!’ asema Yerusalemu.” 36  Kwa hiyo Yehova anasema hivi: “Ninaitetea kesi yako,+Nami nitakulipizia kisasi.+ Nitaikausha bahari yake na kuvikausha visima vyake.+ 37  Na Babiloni atakuwa marundo ya mawe,+Pango la mbwamwitu,+Kitu cha kutisha na kitu cha kupigiwa mluzi,Bila mkaaji.+ 38  Wote pamoja watanguruma kama wanasimba.* Watanguruma kama watoto wa simba.” 39  “Watakapokuwa wamesisimka, nitaandaa karamu yao na kuwalewesha,Ili wafurahi;+Kisha watalala usingizi wa kudumu,Nao hawataamka kutoka katika usingizi huo,”+ asema Yehova. 40  “Nitawashusha chini kama wanakondoo kwenda machinjioni,Kama kondoo dume pamoja na mbuzi.” 41  “Jinsi Sheshaki* alivyotekwa,+Jinsi Sifa ya dunia yote ilivyokamatwa!+ Jinsi ambavyo Babiloni amekuwa kitu cha kutisha kati ya mataifa! 42  Bahari imekuja juu ya Babiloni. Mawimbi yake mengi yamemfunika. 43  Majiji yake yamekuwa kitu cha kutisha, nchi isiyo na maji na jangwa. Nchi ambayo hakuna mtu atakayeishi wala kupitia humo.+ 44  Nitamkazia fikira Beli+ huko Babiloni,Nami nitatoa kinywani mwake kile alichomeza.+ Mataifa hayatamiminika kwake tena. Na ukuta wa Babiloni utaanguka.+ 45  Tokeni kati yake, watu wangu!+ Kimbieni ili mwokoe uhai wenu*+ kutoka kwa hasira ya Yehova inayowaka!+ 46  Msife moyo wala msiogope kwa sababu ya habari itakayosikiwa nchini. Katika mwaka mmoja habari itakuja,Na mwaka unaofuata habari nyingine,Kuhusu ukatili nchini na kuhusu mtawala akimshambulia mtawala mwingine. 47  Kwa hiyo tazama! siku zinakujaNitakapozikazia fikira sanamu za kuchongwa za Babiloni. Nchi yake yote itaaibishwa,Na watu wake wote waliouawa wataanguka ndani yake.+ 48  Mbingu na dunia na vyote vilivyomoVitapiga vigelegele vya shangwe kwa sababu ya Babiloni,+Kwa maana waangamizaji watamvamia kutoka kaskazini,”+ asema Yehova. 49  “Babiloni hakusababisha tu kuuawa kwa Waisraeli walioanguka+Bali pia huko Babiloni watu waliouawa wa dunia yote wameanguka. 50  Ninyi mnaoponyoka upanga, endeleeni kupiga mwendo, msisimame tuli!+ Mkumbukeni Yehova kutoka mbali,Yerusalemu na aingie moyoni mwenu.”+ 51  “Tumeaibishwa, kwa maana tumesikia dhihaka. Nyuso zetu zimefunikwa kwa fedheha,Kwa maana watu wa nchi ya kigeni* wameshambulia mahali patakatifu pa nyumba ya Yehova.”+ 52  “Kwa hiyo tazameni! siku zinakuja,” asema Yehova,“Nitakapozikazia fikira sanamu zake za kuchongwa,Na katika nchi yake yote waliojeruhiwa watalia kwa maumivu.”+ 53  “Hata Babiloni akipanda juu mbinguni,+Hata akiimarisha ngome zake ndefu,Watakaomwangamiza watakuja kutoka kwangu,”+ asema Yehova. 54  “Sikilizeni! Kuna kilio kikubwa kutoka Babiloni,+Sauti ya msiba mkubwa kutoka nchi ya Wakaldayo,+ 55  Kwa maana Yehova analiangamiza Babiloni,Atainyamazisha sauti yake kubwa,Na mawimbi yao yatavuma kama maji mengi. Kelele ya sauti yao itasikika. 56  Kwa maana mwangamizaji ataishambulia Babiloni;+Mashujaa wake watakamatwa,+Pinde zao zitavunjwavunjwa,Kwa maana Yehova ni Mungu wa kisasi.+ Bila shaka atalipa kisasi.+ 57  Nitawalewesha wakuu wake na watu wake wenye hekima,+Magavana wake na watawala wake wasaidizi na mashujaa wake,Nao watalala usingizi wa kudumu,Nao hawataamka kutoka katika usingizi huo,”+ asema Mfalme, ambaye jina lake ni Yehova wa majeshi. 58  Yehova wa majeshi anasema hivi: “Ingawa ukuta wa Babiloni ni mpana, utabomolewa kabisa,+Na ingawa malango yake ni marefu, yatawashwa moto. Watu watafanya kazi ya bure;Mataifa yatajichosha ili tu kuuchochea moto.”+ 59  Hili ndilo neno ambalo nabii Yeremia alimwamuru Seraya mwana wa Neria+ mwana wa Mahseya alipoenda na Mfalme Sedekia wa Yuda huko Babiloni katika mwaka wa nne wa utawala wake; Seraya alikuwa msimamizi wa makao. 60  Yeremia aliandika katika kitabu kimoja msiba wote ambao ungepata Babiloni, maneno hayo yote yaliyoandikwa dhidi ya Babiloni. 61  Isitoshe, Yeremia akamwambia Seraya: “Utakapofika Babiloni na kuliona jiji hilo, lazima uyasome kwa sauti kubwa maneno haya yote. 62  Kisha useme, ‘Ee Yehova, umesema dhidi ya mahali hapa kwamba pataangamizwa na kubaki bila mkaaji, mwanadamu au mnyama, na kwamba patabaki ukiwa milele.’+ 63  Na utakapomaliza kukisoma kitabu hiki, utakifunga kwenye jiwe na kukitupa katikati ya Mto Efrati. 64  Kisha useme, ‘Hivi ndivyo Babiloni atakavyozama naye hatainuka tena kamwe+ kwa sababu ya msiba ambao ninamletea; nao watachoka.’”+ Maneno ya Yeremia yamefikia hapa.

Maelezo ya Chini

Inaonekana hili ni jina la siri la Ukaldayo.
Tnn., “asiukanyage.”
Yaani, nchi ya Wakaldayo.
Au “nafsi yenu.”
Au labda, “jazeni podo.”
Au “nguzo ya ishara.”
Tnn., “kipimo.”
Au “huufanya mvuke upande.”
Au labda, “malango.”
Au “sanamu yake ya kuyeyushwa.”
Au “pumzi.”
Au “ubatili.”
Au “nguzo ya ishara.”
Tnn., “Takaseni.”
Tnn., “Takaseni.”
Tnn., “Nebukadreza,” njia nyingine ya kuandika jina hili.
Au “wanasimba wenye manyoya marefu shingoni.”
Inaonekana hili ni jina la siri la Babeli (Babiloni).
Au “nafsi zenu.”
Au “wageni.”