Yeremia 6:1-30

  • Kuzingirwa kwa Yerusalemu kunakaribia (1-9)

  • Ghadhabu ya Yehova dhidi ya Yerusalemu (10-21)

    • Wanasema “Kuna amani!” wakati hakuna amani (14)

  • Watavamiwa kikatili kutoka kaskazini (22-26)

  • Yeremia atakuwa mpimaji wa madini (27-30)

6  Kimbilieni usalama, enyi wana wa Benjamini, mbali na Yerusalemu. Pigeni pembe+ huko Tekoa;+Washeni ishara ya moto Beth-hakeremu! Kwa maana msiba unakuja kutoka kaskazini, msiba mkubwa.+   Binti ya Sayuni anafanana na mwanamke mrembo na mwororo.+   Wachungaji watakuja na mifugo yao. Watapiga mahema yao kumzunguka pande zote,+Kila mmoja akilisha mifugo anayotunza.+   “Jitayarisheni kupigana vita naye!* Simameni, tumshambulie wakati wa adhuhuri!” “Ole wetu, kwa maana siku inakwisha,Kwa maana vivuli vya jioni vinarefuka!”   “Simameni, tumshambulie usikuNa kuiharibu minara yake yenye ngome.”+   Kwa maana Yehova wa majeshi anasema hivi: “Kateni miti na mjenge boma la kuzingira Yerusalemu.+ Yeye ni jiji ambalo lazima liadhibiwe;*Hamna lolote ndani yake isipokuwa ukandamizaji.+   Kama tangi linavyohifadhi maji yake yakiwa baridi,Ndivyo anavyohifadhi uovu wake ukiwa baridi. Ukatili na maangamizi yanasikiwa ndani yake;+Ugonjwa na tauni viko mbele zangu daima.   Nakuonya, Ee Yerusalemu, la sivyo nitakuacha* kwa chuki;+Nitakufanya uwe ukiwa, nchi isiyo na wakaaji.”+   Yehova wa majeshi anasema hivi: “Watawaokota kikamilifu Waisraeli watakaobaki kama zabibu za mwisho zilizo kwenye mzabibu. Pitisha mkono wako tena kama mtu anayekusanya zabibu kwenye mizabibu.” 10  “Nitazungumza na nani na kumwonya? Ni nani atakayesikiliza? Tazama! Masikio yao yamezibwa* hivi kwamba hawawezi kusikiliza.+ Tazama! Neno la Yehova limekuwa kitu wanachokidharau;+Hawapendezwi nalo. 11  Basi nimejawa na ghadhabu ya Yehova,Nami nimechoka kuizuia ndani yangu.”+ “Imwage juu ya mtoto aliye barabarani,+Juu ya vikundi vya vijana waliokusanyika pamoja. Wote watakamatwa, mwanamume pamoja na mke wake,Wazee pamoja na waliozeeka sana.*+ 12  Watu wengine watapewa nyumba zao,Pamoja na mashamba yao na wake zao.+ Kwa maana nitaunyoosha mkono wangu dhidi ya wakaaji wa nchi,” asema Yehova. 13  “Kwa maana kuanzia mdogo zaidi mpaka mkubwa zaidi, kila mmoja anajipatia faida isiyo ya haki;+Kuanzia nabii mpaka kuhani, kila mmoja anatenda kwa ulaghai.+ 14  Nao wanajaribu kuponya kijuujuu jeraha* la watu wangu, wakisema,‘Kuna amani! Kuna amani!’ Wakati hakuna amani.+ 15  Je, wanaona aibu kwa sababu ya mambo yanayochukiza waliyotenda? Hawaoni aibu hata kidogo! Hata hawajui jinsi ya kufedheheka!+ Basi wataanguka miongoni mwa wale walioanguka. Nitakapowaadhibu watajikwaa,” asema Yehova. 16  Yehova anasema hivi: “Simameni kwenye makutano ya barabara mwone. Ulizeni kuhusu barabara za zamani za kale,Ulizeni mahali ilipo njia nzuri, nanyi mtembee ndani yake,+Nanyi mtajipumzisha.”* Lakini wanasema: “Hatutatembea kwenye njia hiyo.”+ 17  “Nami nikawaweka walinzi+ waliosema,‘Isikilizeni sauti ya pembe!’”+ Lakini wakasema: “Hatutaisikiliza.”+ 18  “Kwa hiyo sikieni, enyi mataifa! Nawe ujue, Ee kusanyiko,Jambo litakalowapata. 19  Sikiliza, Ee dunia! Ninawaletea msiba watu hawa+Kama matunda ya mipango yao,Kwa maana hawakuyasikiliza maneno yanguNao waliikataa sheria* yangu.” 20  “Ninafaidikaje mnapoleta ubani kutoka ShebaNa utete wenye manukato kutoka nchi ya mbali? Dhabihu zenu nzima za kuteketezwa hazikubaliki,Na dhabihu zenu hazinipendezi.”+ 21  Kwa hiyo Yehova anasema hivi: “Ninawawekea watu hawa vikwazo,Nao watajikwaa juu yake,Akina baba na wana pia,Jirani na mwenzake,Nao wataangamia wote.”+ 22  Yehova anasema hivi: “Tazama! Watu wanakuja kutoka nchi ya kaskazini,Na taifa kubwa litaamshwa kutoka sehemu za mbali zaidi za dunia.+ 23  Watashika upinde na mkuki. Ni wakatili na hawatakuwa na huruma. Sauti yao itanguruma kama bahari,Nao wanapanda farasi.+ Wanajipanga kivita dhidi yako kama mwanamume wa vita, Ee binti ya Sayuni.” 24  Tumesikia habari zake. Mikono yetu imelegea.+ Taabu imetushika,Maumivu kama ya* mwanamke anayezaa.+ 25  Usiende shambani,Wala usitembee barabarani,Kwa maana adui ana upanga;Kuna hofu kila upande. 26  Ee binti ya watu wangu,Vaa nguo za magunia+ na ugaegae katika majivu. Omboleza kana kwamba unamwombolezea mwana wa pekee, kwa kilio cha uchungu,+Kwa maana mwangamizaji atatushambulia kwa ghafla.+ 27  “Nimekufanya wewe* kuwa mpimaji wa madini miongoni mwa watu wangu,Mtu anayefanya uchunguzi kamili;Unapaswa kuangalia na kuchunguza njia yao. 28  Wote ni watu wakaidi kabisa,+Wanaotembea huku na huku wakichongea.+ Wao ni kama shaba na chuma;Wote wamepotoka. 29  Vifaa vya kuvukuta vimeunguzwa. Risasi inatoka kwenye moto wao. Mtu anaendelea kuwasafisha sana lakini anafanya kazi ya bure,+Na wale wabaya hawajatengwa.+ 30  Hakika watu watawaita fedha iliyokataliwa,Kwa maana Yehova amewakataa.”+

Maelezo ya Chini

Tnn., “Takaseni vita dhidi yake.”
Au “liwajibishwe.”
Au “nafsi yangu itakuacha.”
Tnn., “Sikio lao halijatahiriwa.”
Tnn., “wale waliojaa siku.”
Au “jeraha la kuvunjika.”
Au “mtazipumzisha nafsi zenu.”
Au “waliyakataa mafundisho.”
Tnn., “Uchungu wa kuzaa kama wa.”
Yaani, Yeremia.