Yeremia 8:1-22

  • Watu wachagua njia inayopendwa na wengi (1-7)

  • Kuna hekima gani bila neno la Yehova? (8-17)

  • Yeremia aomboleza kwa sababu ya kuvunjika kwa Yuda (18-22)

    • “Je, hakuna zeri kule Gileadi?” (22)

8  “Wakati huo,” asema Yehova, “mifupa ya wafalme wa Yuda, mifupa ya wakuu wake, mifupa ya makuhani, mifupa ya manabii, na mifupa ya wakaaji wa Yerusalemu itatolewa katika makaburi yao.  Itatandazwa juani na mbele ya mwezi na kwa jeshi lote la mbinguni ambalo wamelipenda na kulitumikia na kulifuata na kulitafuta na kuliinamia.+ Haitakusanywa, wala haitazikwa. Itakuwa kama mbolea juu ya ardhi.”+  “Na wale watakaobaki na kuokoka wa familia hii yenye uovu watachagua kifo badala ya uhai katika sehemu zote ambazo nitawatawanya,” asema Yehova wa majeshi.  “Nawe unapaswa kuwaambia, ‘Yehova anasema hivi: “Je, wataanguka na wasisimame tena? Mtu akigeuka, je, yule mwingine hatageuka pia?   Kwa nini watu hawa, Yerusalemu, wanakosa uaminifu kwa ukosefu wa uaminifu unaodumu? Wanashika kwa nguvu udanganyifu;Wanakataa kugeuka.+   Nilitega sikio na kuendelea kusikiliza, lakini mazungumzo yao hayakuwa mazuri. Hakuna mtu aliyetubu uovu wake au kuuliza, ‘Nimefanya nini?’+ Kila mmoja anarudi tena na tena kwenye njia inayopendwa na wengi, kama farasi anayekimbia kasi kuingia vitani.   Hata korongo angani anajua majira yake;*Njiwa tetere na mbayuwayu na teleka* hawachelewi kurudi.* Lakini watu wangu hawaelewi hukumu ya Yehova.”’+   ‘Mnawezaje kusema: “Tuna hekima, nasi tuna sheria* ya Yehova”? Kwa hakika, kalamu ya uwongo*+ ya waandishi imetumiwa kuandika uwongo tu.   Wenye hekima wameaibishwa.+ Wameogopa nao watashikwa. Tazama! Wamelikataa neno la Yehova,Nao wana hekima gani? 10  Basi nitawapa wanaume wengine wake zao,Na mashamba yao nitawapa wamiliki wengine;+Kwa maana kuanzia mdogo zaidi mpaka mkubwa zaidi, kila mmoja anajipatia faida isiyo ya haki;+Kuanzia nabii mpaka kuhani, kila mmoja anatenda kwa ulaghai.+ 11  Nao wanajaribu kuponya kijuujuu jeraha* la binti ya watu wangu, wakisema,“Kuna amani! Kuna amani!” Wakati hakuna amani.+ 12  Je, wanaona aibu kwa sababu ya mambo yenye kuchukiza waliyotenda? Hawaoni aibu hata kidogo! Hata hawajui jinsi ya kufedheheka!+ Basi wataanguka kati ya wale walioanguka. Nitakapowaletea adhabu watajikwaa,”+ asema Yehova. 13  ‘Nitakapowakusanya, nitawamaliza,’ asema Yehova. ‘Hakutakuwa na zabibu zitakazobaki kwenye mzabibu, wala tini kwenye mtini, na majani yatanyauka. Nao watapoteza kile nilichowapa.’” 14  “Kwa nini tunaketi hapa? Tukusanyikeni pamoja tuingie katika majiji yenye ngome+ na kuangamia humo. Kwa maana Yehova Mungu wetu atatuangamiza,Naye anatupatia maji yenye sumu tunywe,+Kwa sababu tumemtendea Yehova dhambi. 15  Tulitumaini kupata amani, lakini hakuna jambo lolote jema lililokuja,Wakati wa kuponywa, lakini kuna hofu!+ 16  Mikoromo ya farasi wake inasikika kutoka Dani. Kwa sababu ya mlio wa farasi dume wake,Nchi nzima inatetemeka. Wanaingia na kuinyafua nchi na kila kitu kilichomo,Jiji na wakaaji wake.” 17  “Kwa maana ninawatuma nyoka kati yenu,Nyoka wenye sumu wasioweza kuchezeshwa,Nao hakika watawauma,” asema Yehova. 18  Huzuni yangu haiwezi kuponywa;Moyo wangu ni mgonjwa. 19  Kutoka nchi ya mbali kuna kilio cha kuomba msaadaKutoka kwa binti ya watu wangu: “Je, Yehova hayuko Sayuni? Au je, mfalme wake hayuko ndani yake?” “Kwa nini wamenikasirisha kwa sanamu zao za kuchongwa,Kwa miungu yao ya kigeni ya ubatili?” 20  “Mavuno yamepita, kiangazi kimeisha,Lakini hatujaokolewa!” 21  Nimevunjwavunjwa kwa sababu ya jeraha* la binti ya watu wangu;+Nimehuzunika. Nimepatwa na mshtuko. 22  Je, hakuna zeri* kule Gileadi?+ Au, je, hakuna mponyaji* huko?+ Kwa nini binti ya watu wangu hajaponywa?+

Maelezo ya Chini

Au “nyakati zake zilizowekwa.”
Au labda, “korongo.”
Au “kuhama.”
Au “mafundisho.”
Au “udanganyifu.”
Au “jeraha la kuvunjika.”
Au “jeraha la kuvunjika.”
Au “mafuta yanayotuliza.”
Au “tabibu.”