Yeremia 9:1-26

  • Yeremia ahuzunika sana (1-3a)

  • Yehova aiadhibu Yuda (3b-16)

  • Nchi ya Yuda yaombolezewa (17-22)

  • Jigambe kuhusu kumjua Yehova (23-26)

9  Laiti kichwa changu kingekuwa maji,Na macho yangu chemchemi ya machozi!+ Ndipo ningelia usiku na mchanaKwa ajili ya watu wangu waliouawa.   Laiti ningepata mahali ambapo wasafiri hulala nyikani! Ndipo ningewaacha watu wangu na kwenda mbali nao,Kwa maana wote ni wazinzi,+Kundi la watu wenye hila.   Wanaupinda ulimi wao kama upinde;Uwongo, badala ya uaminifu, umeenea nchini.+ “Wanatoka uovu hadi uovu zaidi,Nao hawanisikilizi,”+ asema Yehova.   “Kila mtu, jihadhari na jirani yako,Wala usimwamini hata ndugu yako. Kwa maana kila ndugu ni msaliti,+Na kila jirani ni mchongezi.+   Kila mtu anamdanganya jirani yake,Na hakuna yeyote anayesema ukweli. Wameufundisha ulimi wao kusema uwongo.+ Wanajichosha kwa kufanya makosa.   Unaishi katikati ya udanganyifu. Katika udanganyifu wao walikataa kunijua mimi,” asema Yehova.   Kwa hiyo Yehova wa majeshi anasema hivi: “Nitawayeyusha na kuwajaribu,+Kwa maana ni nini kingine ninachoweza kumtendea binti ya watu wangu?   Ulimi wao ni mshale unaoua na kusema udanganyifu. Kwa kinywa chake mtu anazungumza na jirani yake kuhusu amani,Lakini ndani anamvizia.”   “Je, sipaswi kuwafanya wawajibike kwa sababu ya mambo haya?” asema Yehova. “Je, sipaswi* kujilipizia kisasi dhidi ya taifa kama hili?+ 10  Nitalia na kuiombolezea milimaNa kuimba wimbo wa huzuni* kwa ajili ya malisho ya nyikani,Kwa maana yameteketezwa hivi kwamba hakuna mwanadamu anayepita humo,Na sauti ya mifugo haisikiwi. Ndege wa angani na wanyama wamekimbia; wametoweka.+ 11  Nitalifanya Yerusalemu kuwa rundo la mawe,+ mapango ya mbwamwitu,+Nami nitayafanya majiji ya Yuda yawe ukiwa, bila mkaaji.+ 12  Ni nani mwenye hekima ya kutosha kuelewa jambo hili? Kinywa cha Yehova kimezungumza na nani, ili atangaze jambo hilo? Kwa nini nchi imeangamia? Kwa nini imeteketezwa kama nyika,Hivi kwamba hakuna mtu anayepita humo?” 13  Yehova akajibu: “Kwa sababu wameikataa sheria* yangu niliyowapa, na kwa sababu hawajaifuata na kutii sauti yangu. 14  Badala yake, walifuata kwa ukaidi mioyo yao wenyewe,+ na kuzifuata sanamu za Baali, kama baba zao walivyowafundisha kufanya.+ 15  Kwa hiyo, Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Tazama, ninawafanya watu hawa wale pakanga, nami nitawafanya wanywe maji yenye sumu.+ 16  Nitawatawanya kati ya mataifa ambayo wao na baba zao hawajayajua,+ nami nitatuma upanga uwafuate mpaka nitakapowaangamiza kabisa.’+ 17  Yehova wa majeshi anasema hivi: ‘Tendeni kwa uelewaji. Waiteni wanawake wanaoimba nyimbo za huzuni,*+Nanyi waiteni wanawake stadi waje, 18  Ili waje haraka na kutuombolezea,Ili macho yetu yabubujike machoziNa kope zetu zitiririke maji.+ 19  Kwa maana sauti ya maombolezo imesikika kutoka Sayuni:+ “Jinsi tulivyoangamizwa! Jinsi aibu yetu ilivyo nyingi! Kwa maana tumeiacha nchi, nao wamezibomoa nyumba zetu.”+ 20  Enyi wanawake, sikieni neno la Yehova. Sikio lenu na lipokee neno la kinywa chake. Wafundisheni mabinti wenu maombolezo haya,Na mfundishane wimbo huu wa huzuni.*+ 21  Kwa maana kifo kimeingia kupitia madirisha yetu;Kimeingia ndani ya minara yetu yenye ngomeIli kuwaondoa watoto barabaraniNa vijana kwenye viwanja vya jiji.’+ 22  Sema, ‘Yehova anasema hivi: “Maiti za watu zitaanguka kama mbolea juu ya ardhi shambani,Kama safu ya miganda ya nafaka iliyotoka kukatwa na mvunaji,Bila mtu wa kuikusanya.”’”+ 23  Yehova anasema hivi: “Mtu mwenye hekima asijigambe kwa sababu ya hekima yake;+Mtu mwenye nguvu asijigambe kwa sababu ya nguvu zake;Na tajiri asijigambe kwa sababu ya utajiri wake.”+ 24  “Lakini yule anayejigamba na ajigambe* kwa jambo hili: Kwamba ana ufahamu na ujuzi kunihusu,+Kwamba mimi ni Yehova, Ninayetenda kwa upendo mshikamanifu, haki, na uadilifu duniani,+Kwa maana ninapendezwa na mambo hayo,”+ asema Yehova. 25  “Tazama! Siku zinakuja,” asema Yehova, “nami nitamwadhibu* kila mtu aliyetahiriwa lakini bado hajatahiriwa,+ 26  yaani, Misri+ na Yuda+ na Edomu+ na Waamoni+ na Moabu+ na wale wote wanaonyoa nywele pembeni mwa vichwa vyao ambao wanakaa nyikani;+ kwa maana mataifa yote hayajatahiriwa, na watu wote wa nyumba ya Israeli hawajatahiriwa moyoni.”+

Maelezo ya Chini

Au “nafsi yangu haipaswi.”
Au “wimbo wa maombolezo.”
Au “wameyakataa mafundisho.”
Au “nyimbo za maombolezo.”
Au “wimbo huu wa maombolezo.”
Au “anayejisifu na ajisifu.”
Au “nitamfanya awajibike.”