Yoeli 1:1-20

  • Shambulizi kali la wadudu (1-14)

  • “Siku ya Yehova iko karibu” (15-20)

    • Nabii amlilia Yehova (19, 20)

1  Neno la Yehova lililomjia Yoeli* mwana wa Pethueli:   “Sikilizeni jambo hili, enyi wazee,Sikilizeni kwa makini, enyi wakaaji wote wa nchi.* Je, jambo kama hili limewahi kutokea katika siku zenuAu katika siku za mababu zenu?+   Wasimulieni wana wenu jambo hilo,Na acheni wana wenu wawasimulie wana wao kulihusu,Na wana wao wasimulie kizazi kitakachofuata.   Kilichoachwa na nzige wanaokula sana, kimeliwa na nzige wanaoruka katika makundi;+Na kilichoachwa na nzige wanaoruka katika makundi, kimeliwa na tunutu;Na kilichoachwa na tunutu, kimeliwa na parare* wanaokula sana.+   Enyi walevi,+ amkeni mlie! Pigeni mayowe, ninyi nyote mnaokunywa divai,Kwa sababu divai tamu imeondolewa vinywani mwenu.+   Kwa maana taifa limeivamia nchi yangu, lenye nguvu na lisilo na idadi.+ Meno yake ni meno ya simba,+ na mataya yake ni ya simba.   Limeharibu mzabibu wangu na kuacha mtini wangu ukiwa kisiki,Limebambua magamba yote na kuyatupa pembeni,Na kuacha matawi yake yakiwa meupe.   Ombolezeni kwa sauti kama bikira* aliyevaa nguo za maguniaAnayeomboleza kwa ajili ya bwana harusi* wa ujana wake.   Toleo la nafaka+ na toleo la kinywaji+ hayapo tena kwenye nyumba ya Yehova;Makuhani, wahudumu wa Yehova, wanaomboleza. 10  Mashamba yameharibiwa, ardhi inaomboleza;+Kwa kuwa nafaka imeharibiwa, divai mpya imekauka, mafuta yametoweka.+ 11  Wakulima wamefadhaika, watunzaji wa mizabibu wanapiga mayowe,Kwa sababu ya ngano na shayiri;Kwa maana mavuno ya shambani yameharibika. 12  Mzabibu umekauka,Mtini umenyauka. Mkomamanga, mtende, na mtofaa,Miti yote shambani imekauka;+Kwa maana badala ya kuwa na shangwe, watu wameshikwa na aibu. 13  Vaeni* nguo za magunia na kuomboleza,* enyi makuhani;Pigeni mayowe, enyi wahudumu wa madhabahu.+ Ingieni na kulala hekaluni usiku kucha mkiwa mmevaa nguo za magunia, enyi wahudumu wa Mungu wangu;Kwa maana matoleo ya nafaka+ na matoleo ya vinywaji+ hayaletwi tena katika nyumba ya Mungu wenu. 14  Tangazeni watu wafunge;* waiteni watu kwenye kusanyiko takatifu.+ Wakusanyeni wazee, pamoja na wakaaji wote wa nchi,Kwenye nyumba ya Yehova Mungu wenu,+ nanyi mlilieni Yehova awasaidie. 15  Ole kwa sababu ya ile siku! Kwa maana siku ya Yehova iko karibu,+Nayo itakuja kama maangamizi kutoka kwa Mweza-Yote! 16  Je, chakula hakijaondolewa mbele ya macho yetu wenyewe,Na shangwe na furaha kutoka katika nyumba ya Mungu wetu? 17  Mbegu* zimenyauka chini ya sepetu zao. Maghala yamebaki ukiwa. Maghala ya nafaka yamebomolewa, kwa maana nafaka imekauka. 18  Hata mifugo inalia kwa uchungu! Makundi ya ng’ombe yanatangatanga huku na huku, kwa maana hayana malisho! Na hata makundi ya kondoo yamepata adhabu. 19  Nitakuita wewe, Ee Yehova;+Kwa maana moto umeteketeza kabisa malisho nyikani,Na mwali wa moto umeteketeza miti yote shambani. 20  Hata wanyama wa mwituni wanasubiri kwa hamu uwasaidie,Kwa sababu vijito vya maji vimekaukaNa moto umeteketeza kabisa malisho nyikani.”

Maelezo ya Chini

Maana yake “Yehova Ni Mungu.”
Au “dunia.”
Au “panzi.”
Au “mwanamwali.”
Au “mume.”
Tnn., “Jifungeni.”
Tnn., “kujipiga vifua.”
Tnn., “Takaseni mfungo.”
Au labda, “Tini zilizokaushwa.”