Kulingana na Yohana 1:1-51

  • Neno akawa mwili (1-18)

  • Ushahidi uliotolewa na Yohana Mbatizaji (19-28)

  • Yesu, Mwanakondoo wa Mungu (29-34)

  • Wanafunzi wa kwanza wa Yesu (35-42)

  • Filipo na Nathanaeli (43-51)

1  Hapo mwanzo Neno alikuwako,+ naye Neno alikuwa pamoja na Mungu,+ na Neno alikuwa mungu.*+  Mwanzoni yeye alikuwa pamoja na Mungu.  Vitu vyote vilikuja kuwako kupitia kwake,+ na bila yeye hakuna hata kitu kimoja kilichokuja kuwako. Kile ambacho kimekuja kuwako  kupitia kwake kilikuwa uzima, na uzima ulikuwa nuru ya wanadamu.+  Nuru inang’aa gizani,+ lakini giza halijaishinda.  Kuna mtu aliyetumwa akiwa mwakilishi wa Mungu; jina lake lilikuwa Yohana.+  Mtu huyo alikuja akiwa shahidi, ili atoe ushahidi kuhusu nuru,+ ili watu wa namna zote waamini kupitia kwake.  Yeye hakuwa nuru hiyo,+ bali alikuja kutoa ushahidi kuhusu nuru hiyo.  Nuru ya kweli inayowaangazia watu wa aina zote ilikuwa karibu kuja ulimwenguni.+ 10  Alikuwa ulimwenguni,+ nao ulimwengu ulikuja kuwako kupitia kwake,+ lakini ulimwengu haukumjua. 11  Alikuja nyumbani kwake mwenyewe, lakini watu wake mwenyewe hawakumkubali. 12  Hata hivyo, wale wote waliompokea, aliwapa mamlaka ya kuwa watoto wa Mungu,+ kwa sababu walikuwa na imani* katika jina lake.+ 13  Nao hawakuzaliwa kutokana na damu, wala mapenzi ya mwili au mapenzi ya mwanadamu, bali kutokana na Mungu.+ 14  Kwa hiyo Neno akawa mwili,+ akakaa kati yetu, nasi tukauona utukufu wake, utukufu ulio kama wa mwana mzaliwa pekee+ kutoka kwa baba; naye alikuwa amejaa kibali cha Mungu* na kweli. 15  (Yohana alitoa ushahidi kumhusu, ndiyo, alisema kwa sauti kubwa: “Huyu ndiye niliyesema kumhusu, ‘Yule anayekuja nyuma yangu amenitangulia, kwa maana alikuwapo kabla yangu.’”)+ 16  Kwa maana sote tulipokea kutokana na wingi alio nao, hata fadhili zisizostahiliwa juu ya fadhili zisizostahiliwa. 17  Kwa sababu Sheria ilitolewa kupitia Musa,+ lakini fadhili zisizostahiliwa+ na kweli zilikuja kupitia Yesu Kristo.+ 18  Hakuna mwanadamu ambaye amemwona Mungu wakati wowote;+ mungu mzaliwa pekee+ aliye kando ya Baba,*+ ndiye ameeleza kumhusu.+ 19  Huu ndio ushahidi aliotoa Yohana, Wayahudi walipowatuma makuhani na Walawi kutoka Yerusalemu wakamuulize: “Wewe ni nani?”+ 20  Naye akakiri na hakukana, akisema: “Mimi siye Kristo.” 21  Nao wakamuuliza: “Basi, wewe ni nani? Je, wewe ndiye Eliya?”+ Akajibu: “Mimi siye.” “Je, wewe ndiye yule Nabii?”+ Akajibu: “Hapana!” 22  Kwa hiyo wakamwambia: “Wewe ni nani? Tuambie ili tupate jibu la kuwapa wale waliotutuma. Unasema nini juu yako mwenyewe?” 23  Akasema: “Mimi ni mtu anayepaza sauti nyikani, ‘Nyoosheni njia ya Yehova,’*+ kama alivyosema nabii Isaya.”+ 24  Sasa wale waliotumwa walitoka kwa Mafarisayo. 25  Basi wakamuuliza: “Kwa nini unabatiza ikiwa wewe si Kristo au Eliya au yule Nabii?” 26  Yohana akawajibu: “Mimi ninabatiza katika maji. Kuna mtu aliyesimama miongoni mwenu msiyemjua, 27  yule anayekuja nyuma yangu, ambaye sistahili kufungua kamba za viatu vyake.”+ 28  Mambo hayo yalifanyika huko Bethania ng’ambo ya Yordani, ambako Yohana alikuwa akibatiza watu.+ 29  Siku iliyofuata alimwona Yesu akimjia, naye akasema: “Ona, Mwanakondoo+ wa Mungu ambaye huondoa dhambi+ ya ulimwengu!+ 30  Huyu ndiye niliyesema kumhusu: ‘Nyuma yangu anakuja mwanamume ambaye amenitangulia, kwa sababu alikuwapo kabla yangu.’+ 31  Hata mimi sikumjua, lakini nilikuja kubatiza katika maji ili afunuliwe kwa Israeli.”+ 32  Yohana pia alitoa ushahidi akisema: “Niliona roho ikishuka kama njiwa kutoka mbinguni, nayo ikakaa juu yake.+ 33  Hata mimi sikumjua, bali Yule aliyenituma nikabatize katika maji aliniambia: ‘Yeyote ambaye utaona roho ikishuka na kukaa juu yake,+ huyo ndiye anayebatiza kwa roho takatifu.’+ 34  Mimi nimeona, nami nimetoa ushahidi kwamba huyo ndiye Mwana wa Mungu.”+ 35  Tena siku iliyofuata, Yohana alikuwa amesimama pamoja na wawili kati ya wanafunzi wake. 36  Alipomtazama Yesu akipita akasema: “Ona, Mwanakondoo+ wa Mungu!” 37  Wanafunzi hao wawili walipomsikia akisema hivyo, wakamfuata Yesu. 38  Ndipo Yesu akageuka na alipowaona wakimfuata, akawauliza: “Mnatafuta nini?” Wakamwambia: “Rabi (neno ambalo linapotafsiriwa linamaanisha, “Mwalimu”), unakaa wapi?” 39  Akawaambia: “Njooni, nanyi mtaona.” Basi wakaenda na kuona mahali alipokuwa akikaa, nao wakakaa pamoja naye siku hiyo; ilikuwa karibu saa kumi.* 40  Andrea,+ ndugu ya Simoni Petro alikuwa mmoja wa wale wawili waliosikia mambo aliyosema Yohana na kumfuata Yesu. 41  Kwanza alimpata Simoni ndugu yake na kumwambia: “Tumempata Masihi”+ (neno ambalo linapotafsiriwa linamaanisha, “Kristo”), 42  kisha akampeleka kwa Yesu. Yesu akamtazama na kumwambia: “Wewe ni Simoni+ mwana wa Yohana; utaitwa Kefa” (linalotafsiriwa kuwa, “Petro”).+ 43  Siku iliyofuata Yesu alitaka kwenda Galilaya. Basi akamkuta Filipo+ na kumwambia: “Njoo uwe mfuasi wangu.” 44  Filipo alitoka Bethsaida, jiji walilotoka Andrea na Petro. 45  Filipo akamkuta Nathanaeli+ na kumwambia: “Tumempata yule ambaye Musa, katika Sheria, na Manabii waliandika kumhusu: Yesu, mwana wa Yosefu,+ kutoka Nazareti.” 46  Lakini Nathanaeli akamuuliza: “Je, kitu chochote kizuri kinaweza kutoka Nazareti?” Filipo akamjibu: “Njoo uone.” 47  Yesu alipomwona Nathanaeli akija, akasema hivi kumhusu: “Ona, Mwisraeli kwa hakika ambaye hamna udanganyifu ndani yake.”+ 48  Nathanaeli akamuuliza: “Umenijuaje?” Yesu akamjibu: “Nilikuona ulipokuwa chini ya mtini, kabla ya Filipo kukuita.” 49  Nathanaeli akamwambia: “Rabi, wewe ni Mwana wa Mungu, wewe ni Mfalme wa Israeli.”+ 50  Yesu akasema: “Je, unaamini kwa sababu nimekuambia nilikuona chini ya mtini? Utaona mambo makubwa kuliko haya.” 51  Kisha akamwambia: “Kwa kweli ninawaambia, mtaona mbingu imefunguliwa na malaika wa Mungu wakipanda na kushuka kwa Mwana wa binadamu.”+

Maelezo ya Chini

Au “alikuwa wa kimungu.”
Au “walionyesha imani.”
Au “alijaa fadhili zisizostahiliwa.”
Au “kifuani pa Baba.” Inamaanisha mahali pa heshima ya pekee au pendeleo.”
Yaani, karibu saa 10 jioni.