Kulingana na Yohana 15:1-27

  • Mfano wa mzabibu wa kweli (1-10)

  • Amri ya kuonyesha upendo kama wa Kristo (11-17)

    • ‘Hakuna aliye na upendo mkuu kuliko huu’ (13)

  • Ulimwengu unawachukia wanafunzi wa Yesu (18-27)

15  “Mimi ndiye mzabibu wa kweli, naye Baba yangu ndiye mkulima.  Yeye huliondoa kila tawi ndani yangu lisilozaa matunda, naye hulisafisha kila tawi linalozaa matunda, ili lizae matunda zaidi.+  Tayari ninyi ni safi kwa sababu ya neno ambalo nimewaambia.+  Kaeni katika muungano pamoja nami, nami nitakaa katika muungano pamoja nanyi. Kama vile tawi lisivyoweza kuzaa matunda likiwa peke yake lisipobaki katika mzabibu, vivyo hivyo hamwezi kuzaa matunda msipokaa katika muungano pamoja nami.+  Mimi ndiye mzabibu; nanyi ndio matawi. Yeyote anayekaa katika muungano pamoja nami, nami katika muungano pamoja naye, huyo huzaa matunda mengi;+ kwa maana bila mimi hamwezi kufanya lolote kamwe.  Ikiwa yeyote hakai katika muungano pamoja nami, atatupwa kama tawi kisha atakauka. Nao watu hukusanya matawi hayo na kuyatupa ndani ya moto, nayo huteketea.  Mkikaa katika muungano pamoja nami, na maneno yangu yakae ndani yenu, ombeni chochote mnachotaka nanyi mtapewa.+  Baba yangu hutukuzwa kwa jambo hili, kwamba mwendelee kuzaa matunda mengi na kujithibitisha kuwa wanafunzi wangu.+  Kama vile Baba alivyonipenda,+ ndivyo nimewapenda ninyi; kaeni katika upendo wangu. 10  Mkishika amri zangu, mtakaa katika upendo wangu, kama vile ambavyo nimeshika amri za Baba na kukaa katika upendo wake. 11  “Nimewaambia mambo haya, ili shangwe yangu iwe ndani yenu na shangwe yenu ijae.+ 12  Hii ndiyo amri yangu, kwamba mpendane kama vile nilivyowapenda.+ 13  Hakuna mtu aliye na upendo mkuu kuliko huu, kwamba mtu atoe uhai wake* kwa ajili ya rafiki zake.+ 14  Ninyi ni rafiki zangu ikiwa mnafanya mambo ninayowaamuru.+ 15  Siwaiti ninyi tena watumwa, kwa sababu mtumwa hajui mambo ambayo bwana wake hufanya. Lakini nimewaita rafiki, kwa sababu nimewajulisha mambo yote niliyosikia kutoka kwa Baba yangu. 16  Ninyi hamkunichagua, bali mimi niliwachagua na kuwaweka rasmi mwende na kuendelea kuzaa matunda na kwamba matunda yenu yadumu, ili hata mkimwomba Baba jambo lolote katika jina langu, awape.+ 17  “Mambo haya ninawaamuru, kwamba mpendane.+ 18  Ikiwa ulimwengu unawachukia, kumbukeni kwamba umenichukia mimi kabla ya kuwachukia ninyi.+ 19  Kama mngekuwa sehemu ya ulimwengu, ulimwengu ungependa kilicho chake. Sasa kwa sababu ninyi si sehemu ya ulimwengu,+ bali nimewachagua kutoka ulimwenguni, kwa sababu hiyo ulimwengu unawachukia.+ 20  Kumbukeni neno nililowaambia: Mtumwa si mkuu kuliko bwana wake. Ikiwa wamenitesa mimi, watawatesa ninyi pia;+ ikiwa wamelishika neno langu, watalishika lenu pia. 21  Lakini watawatendea mambo yote haya kwa ajili ya jina langu, kwa sababu hawamjui Yule aliyenituma.+ 22  Kama singekuja na kuzungumza nao, hawangekuwa na dhambi.+ Lakini sasa hawana kisingizio kwa ajili ya dhambi yao.+ 23  Anayenichukia mimi anamchukia Baba+ yangu pia. 24  Kama singefanya kati yao kazi ambazo hakuna mwingine aliyezifanya, hawangekuwa na dhambi;+ lakini sasa wameniona, nao wamenichukia mimi na pia Baba yangu. 25  Lakini hilo lilifanyika ili kutimiza neno lililoandikwa katika Sheria yao: ‘Walinichukia bila sababu.’+ 26  Atakapokuja msaidizi ambaye nitawatumia kutoka kwa Baba, roho ya ile kweli,+ inayotoka kwa Baba, huyo atatoa ushahidi kunihusu;+ 27  nanyi, mtatoa ushahidi,+ kwa sababu mmekuwa pamoja nami tangu mwanzoni.

Maelezo ya Chini

Au “nafsi yake.”