Kulingana na Yohana 16:1-33

  • Wanafunzi wa Yesu watakabili kifo (1-4a)

  • Kazi ya roho takatifu (4b-16)

  • Huzuni ya wanafunzi itageuka kuwa shangwe (17-24)

  • Yesu aushinda Ulimwengu (25-33)

16  “Nimewaambia mambo haya ili msikwazike.  Watu watawafukuza katika masinagogi.+ Kwa kweli, saa inakuja ambayo kila mtu atakayewaua+ atafikiri kwamba amemtolea Mungu utumishi mtakatifu.  Lakini watafanya mambo haya kwa sababu hawamjui Baba wala mimi.+  Hata hivyo, nimewaambia mambo haya ili saa yake itakapofika, mkumbuke kwamba niliwaambia.+ “Sikuwaambia mambo haya mwanzoni, kwa sababu nilikuwa pamoja nanyi.  Lakini sasa ninaenda kwa Yule aliyenituma;+ na bado hakuna hata mmoja wenu anayeniuliza, ‘Unaenda wapi?’  Lakini kwa sababu nimewaambia mambo haya, mioyo yenu imejaa huzuni.+  Hata hivyo, ninawaambia ukweli, ninaenda zangu kwa faida yenu. Kwa maana nisipoenda, msaidizi+ hatakuja kwenu; lakini nikienda, nitamtuma kwenu.  Naye atakapokuja atauthibitishia waziwazi ulimwengu kuhusu dhambi na kuhusu uadilifu na kuhusu hukumu:  kwanza kuhusu dhambi,+ kwa sababu hawaniamini;*+ 10  kisha kuhusu uadilifu, kwa sababu ninaenda kwa Baba nanyi hamtaniona tena; 11  pia kuhusu hukumu, kwa sababu mtawala wa ulimwengu huu amehukumiwa.+ 12  “Bado nina mambo mengi ya kuwaambia, lakini hamwezi kuyastahimili kwa sasa. 13  Hata hivyo, huyo* atakapokuja, roho ya ile kweli,+ atawaongoza ninyi kwenye kweli yote, kwa maana hatasema kwa uamuzi wake mwenyewe, bali atasema mambo anayosikia, naye atawatangazia mambo yanayokuja.+ 14  Huyo atanitukuza,+ kwa sababu atawatangazia mambo aliyopokea kutoka kwangu.+ 15  Vitu vyote alivyo navyo Baba ni vyangu.+ Ndiyo sababu nilisema huyo atawatangazia mambo aliyopokea kutoka kwangu. 16  Baada ya muda kidogo hamtaniona tena,+ na baada ya muda kidogo mtaniona.” 17  Ndipo baadhi ya wanafunzi wake wakaulizana: “Anamaanisha nini anapotuambia, ‘Baada ya muda kidogo hamtaniona, na tena, baada ya muda kidogo mtaniona,’ na, ‘kwa sababu ninaenda kwa Baba’?” 18  Basi walikuwa wakisema: “Anamaanisha nini anaposema, ‘muda kidogo’? Hatuelewi anachozungumzia.” 19  Yesu alijua kwamba walitaka kumuuliza, basi akawaambia: “Je, mnaulizana hivyo kwa sababu nilisema: ‘Baada ya muda kidogo hamtaniona, na tena, baada ya muda kidogo mtaniona’? 20  Kwa kweli ninawaambia, mtalia na kuomboleza, lakini ulimwengu utashangilia; mtahuzunika, lakini huzuni yenu itageuka kuwa shangwe.+ 21  Mwanamke anapokuwa akizaa anahisi huzuni kwa sababu saa yake imefika, lakini baada ya kumzaa mtoto hakumbuki tena dhiki hiyo kwa sababu anashangilia kwamba mtu amezaliwa ulimwenguni. 22  Basi, ninyi pia mnahuzunika sasa; lakini nitawaona tena na mioyo yenu itashangilia+ na hakuna mtu atakayeondoa shangwe yenu. 23  Siku hiyo hamtaniuliza swali lolote. Kwa kweli ninawaambia, mkimwomba Baba jambo lolote,+ atawapa katika jina langu.+ 24  Kufikia sasa hamjaomba hata jambo moja katika jina langu. Ombeni nanyi mtapewa, ili shangwe yenu iwe kamili. 25  “Nimewaambia mambo haya kwa mifano. Saa inakuja ambapo sitazungumza nanyi tena kwa mifano, bali nitawaeleza waziwazi kumhusu Baba. 26  Siku hiyo mtamwomba Baba katika jina langu; ninaposema hivyo, simaanishi kwamba nitawaombea ninyi. 27  Kwa maana Baba mwenyewe anawapenda ninyi, kwa sababu mmenipenda+ na mmeamini kwamba nilikuja nikiwa mwakilishi wa Mungu.+ 28  Nilikuja nikiwa mwakilishi wa Baba, nami nimekuja ulimwenguni. Sasa ninaondoka ulimwenguni, nami ninarudi kwa Baba.”+ 29  Wanafunzi wake wakamwambia: “Ona! Sasa unazungumza waziwazi, nawe hutumii mifano. 30  Sasa tunafahamu kwamba unajua mambo yote na huhitaji kuulizwa swali na mtu yeyote. Kwa hiyo, tunaamini kwamba ulitoka kwa Mungu.” 31  Yesu akawajibu: “Je, sasa mnaamini? 32  Tazama! Saa inakuja, na kwa kweli imefika, wakati kila mmoja wenu atatawanyika na kwenda nyumbani kwake, nanyi mtaniacha peke yangu.+ Lakini siko peke yangu, kwa sababu Baba yuko pamoja nami.+ 33  Nimewaambia mambo haya ili kupitia kwangu muwe na amani.+ Ulimwenguni mtapata dhiki, lakini jipeni moyo! Mimi nimeushinda ulimwengu.”+

Maelezo ya Chini

Au “hawaonyeshi kwamba wananiamini.”
Maneno “huyo” na “naye” katika mstari wa 13 na 14 yanarejelea “msaidizi” aliyetajwa katika mstari wa 7. Yesu alitumia neno “msaidizi” (ambalo lina jinsia ya kiume katika Kigiriki) alipoipa roho takatifu sifa ya mtu ingawa ni nguvu isiyo na utu, na katika Kigiriki haina jinsia ya kiume wala ya kike.