Kulingana na Yohana 2:1-25

  • Harusi huko Kana; abadili maji kuwa divai (1-12)

  • Yesu asafisha hekalu (13-22)

  • Yesu anajua kilicho ndani ya mwanadamu (23-25)

2  Basi siku ya tatu kulikuwa na karamu ya ndoa katika Kana ya Galilaya, na mama ya Yesu alikuwa huko.  Yesu na wanafunzi wake pia walikuwa wamealikwa kwenye karamu hiyo ya ndoa.  Divai ilipopungua mama ya Yesu akamwambia: “Hawana divai.”  Lakini Yesu akamjibu: “Mwanamke, jambo hilo linatuhusuje mimi na wewe?* Bado saa yangu haijafika.”  Mama yake akawaambia wahudumu: “Fanyeni lolote atakalowaambia.”  Kulikuwa na mitungi sita ya maji hapo kulingana na sheria za utakaso za Wayahudi,+ kila mmoja ulikuwa na uwezo wa kuchukua vipimo* viwili au vitatu vya maji.  Yesu akawaambia: “Ijazeni mitungi hiyo maji.” Nao wakaijaza pomoni.  Akawaambia: “Choteni kidogo na kumpelekea msimamizi wa karamu.” Basi wakampelekea.  Msimamizi wa karamu alipoonja maji yaliyokuwa yamegeuzwa kuwa divai, bila kujua divai ilitoka wapi (lakini wahudumu waliokuwa wamechota maji hayo walijua), akamwita bwana harusi 10  akamwambia: “Kila mtu hutoa divai nzuri kwanza, kisha hutoa divai hafifu wakati ambapo watu wameingiwa na kileo. Lakini wewe umehifadhi divai nzuri mpaka sasa.” 11  Yesu alifanya muujiza huo wake wa kwanza katika Kana ya Galilaya, kwa hiyo akaonyesha utukufu wake,+ na wanafunzi wake wakamwamini. 12  Baada ya hayo, Yesu, mama yake, ndugu zake,+ na wanafunzi wake wakashuka kwenda Kapernaumu,+ lakini hawakukaa huko siku nyingi. 13  Pasaka+ ya Wayahudi ilikuwa imekaribia, basi Yesu akapanda kwenda Yerusalemu. 14  Alipoingia hekaluni akakuta watu wakiuza ng’ombe, kondoo, na njiwa,+ pia, wale waliobadili pesa walikuwa kwenye viti vyao. 15  Basi akatengeneza mjeledi wa kamba na kuwafukuza hekaluni wote waliokuwa na kondoo na ng’ombe, akamwaga sarafu za wale waliobadili pesa na kupindua meza zao.+ 16  Akawaambia wale waliokuwa wakiuza njiwa: “Ondoeni vitu hivi hapa! Acheni kuifanya nyumba ya Baba yangu kuwa nyumba ya biashara!”*+ 17  Wanafunzi wake wakakumbuka kwamba imeandikwa: “Bidii kwa ajili ya nyumba yako itanila.”+ 18  Kwa hiyo, Wayahudi wakamuuliza: “Utatuonyesha ishara gani,+ kwa maana unafanya mambo haya?” 19  Yesu akawajibu: “Libomoeni hekalu hili, na kwa siku tatu nitalisimamisha.”+ 20  Kisha Wayahudi wakasema: “Hekalu hili lilijengwa kwa miaka 46, je, wewe utalisimamisha kwa siku tatu?” 21  Lakini alikuwa akizungumza kuhusu hekalu la mwili wake.+ 22  Hata hivyo, alipofufuliwa kutoka kwa wafu, wanafunzi wake wakakumbuka alikuwa akisema jambo hilo,+ nao wakaamini andiko na maneno ambayo Yesu alikuwa amesema. 23  Hata hivyo, alipokuwa Yerusalemu kwenye sherehe ya Pasaka, watu wengi wakamwamini, kwa sababu waliona miujiza aliyokuwa akifanya. 24  Lakini Yesu alijihadhari nao kwa sababu aliwajua wote 25  na hakuhitaji mtu yeyote atoe ushahidi kuhusu mwanadamu, kwa maana alijua kilicho ndani ya mwanadamu.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “Nina nini nawe, mwanamke?” Hii ni nahau au msemo unaoonyesha kukataa jambo. Matumizi ya neno “mwanamke” hayaonyeshi ukosefu wa heshima.
Yaelekea kipimo hicho kilikuwa bathi iliyokuwa sawa na lita 22. Angalia Nyongeza B14.
Au “soko.”