Kulingana na Yohana 20:1-31

  • Kaburi tupu (1-10)

  • Yesu amtokea Maria Magdalene (11-18)

  • Yesu awatokea wanafunzi wake (19-23)

  • Tomasi awa na shaka lakini baadaye asadikishwa (24-29)

  • Kusudi la kitabu hiki cha kukunjwa (30, 31)

20  Siku ya kwanza ya juma, Maria Magdalene alienda mapema kwenye kaburi,*+ kulipokuwa bado na giza, naye akaona jiwe limeondolewa kwenye kaburi.*+  Basi akakimbia kwenda kwa Simoni Petro na yule mwanafunzi mwingine, ambaye Yesu alimpenda,+ naye akawaambia: “Wamemwondoa Bwana kaburini,+ nasi hatujui wamemlaza wapi.”  Ndipo Petro na yule mwanafunzi mwingine wakaelekea kaburini.  Wote wawili wakaanza kukimbia pamoja, lakini yule mwanafunzi mwingine akakimbia upesi kuliko Petro akatangulia kufika kwenye kaburi.  Akainama, akaona vitambaa vya kitani hapo chini,+ lakini hakuingia ndani.  Ndipo Simoni Petro akaja akimfuata, akaingia kaburini. Naye akaona vile vitambaa vya kitani hapo chini.  Kitambaa ambacho Yesu alikuwa amefungwa kichwani hakikuwa pamoja na vitambaa vingine bali kilikuwa kimekunjwa na kuwekwa kando.  Kisha yule mwanafunzi mwingine aliyetangulia kufika kwenye kaburi akaingia pia, naye akaona na kuamini.  Kwa maana bado hawakuwa wameelewa andiko linalosema kwamba lazima afufuliwe kutoka kwa wafu.+ 10  Basi wanafunzi hao wakarudi nyumbani kwao. 11  Hata hivyo, Maria akaendelea kusimama nje ya kaburi akilia. Alipokuwa akilia, akainama kutazama ndani ya kaburi, 12  naye akaona malaika wawili+ waliovaa mavazi meupe wakiwa wameketi mahali ulipokuwa umelazwa mwili wa Yesu, mmoja kichwani na mwingine miguuni. 13  Nao wakamuuliza: “Mwanamke, kwa nini unalia?” Akawajibu: “Wamemwondoa Bwana wangu, nami sijui wamemlaza wapi.” 14  Baada ya kusema hayo, akageuka na kumwona Yesu akiwa amesimama hapo, lakini hakutambua kwamba ni Yesu.+ 15  Yesu akamuuliza: “Mwanamke, kwa nini unalia? Unamtafuta nani?” Maria, akifikiri kwamba ni mtunza-bustani, akamwambia: “Bwana, ikiwa umemchukua, niambie umemlaza wapi, nami nitamwondoa.” 16  Yesu akamwita: “Maria!” Alipogeuka akasema kwa Kiebrania: “Raboni!” (maana yake “Mwalimu!”) 17  Yesu akamwambia: “Acha kuning’ang’ania, kwa maana bado sijapanda kwenda kwa Baba. Lakini nenda kwa ndugu zangu,+ nawe uwaambie, ‘Ninapanda kwenda kwa Baba yangu+ na Baba yenu na kwa Mungu wangu+ na Mungu wenu.’” 18  Maria Magdalene akaenda na kuwaambia wanafunzi: “Nimemwona Bwana!” Kisha akawaambia alichoambiwa na Yesu.+ 19  Ilipofika jioni siku hiyo, siku ya kwanza ya juma, milango ikiwa imefungwa mahali ambapo wanafunzi walikuwa kwa sababu ya kuwaogopa Wayahudi, Yesu akaja na kusimama katikati yao na kuwaambia: “Na muwe na amani.”+ 20  Baada ya kusema hayo, akawaonyesha mikono yake na ubavu wake.+ Basi wanafunzi wakashangilia walipomwona Bwana.+ 21  Yesu akawaambia tena: “Na muwe na amani.+ Kama vile ambavyo Baba amenituma,+ mimi pia ninawatuma ninyi.”+ 22  Baada ya kusema hivyo akapuliza juu yao na kuwaambia: “Pokeeni roho takatifu.+ 23  Mkimsamehe mtu yeyote dhambi zake, atasamehewa; msipomsamehe mtu yeyote dhambi zake, hatasamehewa.” 24  Lakini Tomasi,+ mmoja wa wale 12, aliyeitwa Pacha, hakuwa pamoja nao Yesu alipokuja. 25  Basi wale wanafunzi wengine walikuwa wakimwambia: “Tumemwona Bwana!” Lakini akawaambia: “Nisipoona alama za misumari kwenye mikono yake na kutia kidole changu katika alama hizo kisha niutie mkono wangu ubavuni mwake,+ sitaamini kamwe.” 26  Basi, siku nane baadaye wanafunzi wake walikuwa tena ndani ya nyumba, na Tomasi alikuwa pamoja nao. Yesu akaja, ingawa milango ilikuwa imefungwa, naye akasimama katikati yao na kusema: “Na muwe na amani.”+ 27  Kisha akamwambia Tomasi: “Weka kidole chako hapa, uone mikono yangu, na ulete mkono wako uguse ubavu wangu, ili uache kuwa na shaka* bali uamini.” 28  Tomasi akamjibu: “Bwana wangu na Mungu wangu!” 29  Yesu akamwambia: “Je, umeamini kwa sababu umeniona? Wenye furaha ni wale ambao wanaamini ingawa bado hawajaona.” 30  Kwa kweli, Yesu alifanya pia miujiza mingine mingi mbele ya wanafunzi, ambayo haijaandikwa katika kitabu hiki cha kukunjwa.+ 31  Lakini mambo haya yameandikwa ili mwamini kwamba Yesu ndiye Kristo, Mwana wa Mungu, na kwa sababu ya kuamini, mpate uzima kupitia jina lake.+

Maelezo ya Chini

Au “kaburi la ukumbusho.”
Au “kaburi la ukumbusho.”
Tnn., “kuwa asiyeamini.”