Kulingana na Yohana 21:1-25

  • Yesu awatokea wanafunzi wake (1-14)

  • Petro amhakikishia Yesu kwamba anampenda (15-19)

    • “Lisha kondoo wangu wadogo” (17)

  • Wakati ujao wa mwanafunzi aliyependwa na Yesu (20-23)

  • Umalizio (24, 25)

21  Baada ya mambo hayo, Yesu alijifunua* tena kwa wanafunzi kwenye Bahari ya Tiberia. Alijifunua katika njia hii.  Simoni Petro, Tomasi (aliyeitwa Pacha),+ Nathanaeli+ kutoka Kana ya Galilaya, wana wa Zebedayo,+ na wanafunzi wake wengine wawili, walikuwa pamoja.  Simoni Petro akawaambia: “Ninaenda kuvua samaki.” Wakamwambia: “Sisi pia tutaenda nawe.” Basi wakaenda, wakapanda mashua, lakini usiku huo hawakuvua chochote.+  Hata hivyo, kulipoanza kupambazuka, Yesu alisimama kando ya bahari, lakini wanafunzi hawakutambua ni Yesu.+  Basi Yesu akawauliza: “Watoto, mna chakula chochote?”* Wakamjibu: “Hapana!”  Akawaambia: “Utupeni wavu upande wa kulia wa mashua, nanyi mtapata.” Basi wakautupa, lakini wakashindwa kuuvuta kwa sababu samaki walikuwa wengi sana.+  Ndipo mwanafunzi ambaye Yesu alimpenda+ akamwambia Petro: “Ni Bwana!” Simoni Petro, aliposikia kwamba ni Bwana, akavaa* vazi lake la nje kwa maana alikuwa uchi,* akajitumbukiza baharini.  Lakini wale wanafunzi wengine wakaja katika ile mashua ndogo, wakiukokota wavu wenye samaki wengi kwa maana hawakuwa mbali na nchi kavu, walikuwa umbali wa mita 90* hivi.  Walipofika ufuoni wakaona moto wa makaa na juu yake palikuwa na samaki na mkate. 10  Yesu akawaambia: “Leteni baadhi ya samaki mliowavua sasa hivi.” 11  Basi Simoni Petro akapanda kwenye mashua na kuuvuta hadi ufuoni wavu uliojaa samaki wakubwa 153. Ingawa walikuwa wengi sana wavu haukupasuka. 12  Yesu akawaambia: “Njooni mpate kiamshakinywa.” Hakuna hata mmoja wa wanafunzi aliyekuwa na ujasiri wa kumuuliza: “Wewe ni nani?” kwa sababu walijua ni Bwana. 13  Yesu akaja, akachukua mkate na kuwapa, na samaki vilevile. 14  Sasa hiyo ilikuwa mara ya tatu+ Yesu kuwatokea wanafunzi baada ya kufufuliwa kutoka kwa wafu. 15  Baada ya kupata kiamshakinywa, Yesu akamuuliza Simoni Petro: “Simoni mwana wa Yohana, je, unanipenda kuliko hawa?” Petro akamjibu: “Ndiyo, Bwana, unajua ninakupenda.” Yesu akamwambia: “Lisha wanakondoo wangu.”+ 16  Akamuuliza mara ya pili: “Simoni mwana wa Yohana, je, unanipenda?” Petro akamjibu: “Ndiyo, Bwana, unajua ninakupenda.” Yesu akamwambia: “Chunga kondoo wangu wadogo.”+ 17  Akamuuliza mara ya tatu: “Simoni mwana wa Yohana, je, unanipenda?” Petro akahuzunika kwamba alimuuliza mara ya tatu: “Je, unanipenda?” Kwa hiyo akamjibu: “Bwana, wewe unajua mambo yote; unajua kwamba ninakupenda.” Yesu akamwambia: “Lisha kondoo wangu wadogo.+ 18  Kwa kweli ninakuambia, ulipokuwa kijana, ulikuwa unavaa mwenyewe na kutembea kokote ulikotaka. Lakini utakapozeeka, utanyoosha mikono yako na mtu mwingine atakuvalisha na kukupeleka usikotaka.” 19  Alisema hivyo ili kuonyesha angemtukuza Mungu kwa kifo cha namna gani. Baada ya kusema hayo, akamwambia: “Endelea kunifuata.”+ 20  Petro alipogeuka, akamwona mwanafunzi ambaye Yesu alimpenda+ akiwafuata, yule ambaye kwenye mlo wa jioni alikuwa ameegemea nyuma kifuani pa Yesu, akamuuliza: “Bwana, ni nani anayekusaliti?” 21  Basi alipomwona, Petro akamuuliza Yesu: “Bwana, namna gani kuhusu mtu huyu?” 22  Yesu akamwambia: “Ikiwa ni mapenzi yangu akae mpaka nije, hilo linakuhusuje? Wewe endelea kunifuata.” 23  Basi habari ikaenea miongoni mwa akina ndugu kwamba mwanafunzi huyo hatakufa. Hata hivyo, Yesu hakumwambia kwamba hatakufa, bali alisema: “Ikiwa ni mapenzi yangu akae mpaka nije, hilo linakuhusuje?” 24  Huyo ndiye mwanafunzi+ anayetoa ushahidi huu kuhusu mambo haya, na ambaye aliyaandika mambo haya, nasi tunajua kwamba ushahidi wake ni wa kweli. 25  Kwa kweli, pia kuna mambo mengine mengi aliyofanya Yesu, ambayo kama yangeandikwa kirefu, nadhani ulimwengu haungekuwa na nafasi ya kuviweka vitabu vya kukunjwa ambavyo vingeandikwa.+

Maelezo ya Chini

Au “aliwatokea.”
Au “samaki wowote.”
Au “akajifunga.”
Au “alikuwa amevaa mavazi machache.”
Karibu futi 300. Tnn., “mikono 200 hivi.” Angalia Nyongeza B14.