Kulingana na Yohana 3:1-36

  • Yesu na Nikodemo (1-21)

    • Kuzaliwa tena (3-8)

    • Mungu aliupenda ulimwengu (16)

  • Yohana atoa ushahidi wa mwisho kumhusu Yesu (22-30)

  • Yule aliyetoka juu (31-36)

3  Kulikuwa na Farisayo aliyeitwa Nikodemo,+ mtawala wa Wayahudi.  Alienda kwa Yesu usiku+ na kumwambia: “Rabi,+ tunajua kwamba wewe ni mwalimu na umetoka kwa Mungu, kwa maana hakuna anayeweza kufanya miujiza+ kama unayofanya isipokuwa Mungu awe pamoja naye.”+  Yesu akamwambia: “Kwa kweli ninakuambia, mtu asipozaliwa tena,*+ hawezi kuuona Ufalme wa Mungu.”+  Nikodemo akamuuliza: “Mtu akiwa mzee anawezaje kuzaliwa tena? Hawezi kuingia tumboni mwa mama yake mara ya pili na kuzaliwa, sivyo?”  Yesu akajibu: “Kwa kweli ninakuambia, mtu asipozaliwa kwa maji+ na roho,+ hawezi kuingia katika Ufalme wa Mungu.  Kile ambacho kimezaliwa kwa mwili ni mwili, na kile ambacho kimezaliwa kwa roho ni roho.  Usishangae kwa sababu nimekuambia: Lazima ninyi mzaliwe tena.  Upepo huvuma mahali unapotaka, nawe unasikia ukivuma, lakini hujui mahali unapotoka wala mahali unapoenda. Ndivyo alivyo kila mtu ambaye amezaliwa kwa roho.”+  Nikodemo akamuuliza: “Mambo haya yanawezekanaje?” 10  Yesu akamjibu: “Je, wewe ni mwalimu wa Israeli na bado hujui mambo haya? 11  Kwa kweli ninakuambia, yale tunayojua tunayasema, na yale ambayo tumeyaona tunatoa ushahidi kuyahusu, lakini ninyi hampokei ushahidi tunaotoa. 12  Ikiwa nimewaambia mambo ya duniani na bado hamyaamini, mtawezaje kuamini nikiwaambia mambo ya mbinguni? 13  Isitoshe, hakuna mtu aliyepanda kwenda mbinguni+ ila yule aliyeshuka kutoka mbinguni,+ yaani, Mwana wa binadamu. 14  Kama vile Musa alivyoinua nyoka nyikani,+ ndivyo Mwana wa binadamu atakavyoinuliwa,+ 15  ili kila mtu anayemwamini apate uzima wa milele.+ 16  “Kwa maana, Mungu aliupenda ulimwengu sana hivi kwamba akamtoa Mwana wake mzaliwa pekee,+ ili kila mtu anayemwamini* asiangamizwe bali awe na uzima wa milele.+ 17  Kwa maana Mungu hakumtuma Mwanawe ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe kupitia kwake.+ 18  Yeyote anayemwamini* hatahukumiwa.+ Yeyote ambaye hamwamini amehukumiwa tayari, kwa sababu hana imani* katika jina la Mwana mzaliwa pekee wa Mungu.+ 19  Basi huu ndio msingi wa hukumu: kwamba nuru imekuja ulimwenguni,+ lakini watu wamependa giza badala ya nuru, kwa maana matendo yao yalikuwa maovu. 20  Kwa maana yeyote ambaye huzoea kutenda mambo maovu huchukia nuru na haji kwenye nuru, ili matendo yake yasikaripiwe.* 21  Lakini yeyote ambaye hufanya yaliyo ya kweli huja kwenye nuru,+ ili matendo yake yafunuliwe kwamba yamefanywa kulingana na Mungu.” 22  Baada ya mambo haya, Yesu na wanafunzi wake wakaenda katika maeneo ya mashambani ya Yudea, naye akakaa pamoja nao huko kwa muda fulani, akiwabatiza watu.+ 23  Lakini Yohana pia alikuwa akibatiza huko Ainoni karibu na Salimu, kwa sababu kulikuwa na maji mengi huko,+ na watu walikuwa wakija na kubatizwa;+ 24  kwa maana bado Yohana hakuwa amefungwa gerezani.+ 25  Wanafunzi wa Yohana walibishana na Myahudi fulani kuhusu utakaso.⁠ 26  Kwa hiyo wakaja kwa Yohana na kumwambia: “Rabi, mtu aliyekuwa pamoja nawe ng’ambo ya Yordani, ambaye ulitoa ushahidi kumhusu,+ anabatiza na watu wote wanaenda kwake.” 27  Yohana akawaambia: “Mtu hawezi kupokea kitu chochote isipokuwa awe amepewa kutoka mbinguni. 28  Ninyi wenyewe mlishuhudia kwamba nilisema, ‘Mimi si Kristo,+ bali, nimetumwa nimtangulie.’+ 29  Yule aliye na bibi harusi ndiye bwana harusi.+ Hata hivyo, rafiki ya bwana harusi, anaposimama na kumsikia, anashangilia sana kwa sababu ya sauti ya bwana harusi. Kwa hiyo shangwe yangu imekamilishwa. 30  Huyo lazima aendelee kuongezeka, lakini mimi lazima niendelee kupungua.” 31  Yule anayetoka juu+ yuko juu ya watu wote. Yule anayetoka duniani, ni wa kutoka duniani na husema kuhusu mambo ya duniani. Yule anayetoka mbinguni, yuko juu ya watu wote.+ 32  Yeye hutoa ushahidi kuhusu mambo aliyoona na kusikia,+ lakini hakuna mtu anayekubali ushahidi wake.+ 33  Yeyote ambaye ameukubali ushahidi wake ametia muhuri wake* kwamba Mungu ni wa kweli.+ 34  Yule ambaye Mungu amemtuma husema maneno ya Mungu,+ kwa maana Mungu hutoa roho yake kwa wingi.* 35  Baba anampenda Mwana+ naye amekabidhi vitu vyote mkononi mwake.+ 36  Yule anayemwamini Mwana ana uzima wa milele;+ yule asiyemtii Mwana hataona uzima,+ bali ghadhabu ya Mungu hukaa juu yake.+

Maelezo ya Chini

Au labda, “asipozaliwa kutoka juu.”
Au “anayeonyesha kwamba anamwamini.”
Au “haonyeshi imani.”
Au “anayeonyesha imani.”
Au “yasifunuliwe.”
Au “amethibitisha.”
Au “hatoi roho kwa kipimo.”