Yoshua 1:1-18

  • Yehova amtia moyo Yoshua (1-9)

    • Soma Sheria kwa sauti ya chini (8)

  • Matayarisho ya kuvuka Yordani (10-18)

1  Baada ya kifo cha Musa mtumishi wa Yehova, Yehova akamwambia Yoshua*+ mwana wa Nuni, mhudumu+ wa Musa:  “Musa mtumishi wangu amekufa.+ Sasa jitayarishe, vuka Mto Yordani pamoja na watu hawa wote, mwingie katika nchi ambayo ninawapa Waisraeli.+  Nitawapa kila mahali mtakapokanyaga, kama nilivyomwahidi Musa.+  Eneo lenu litaanzia nyikani mpaka kwenye Mlima Lebanoni hadi ule mto mkubwa, Efrati, yaani, nchi yote ya Wahiti,+ mpaka kwenye Bahari Kuu,* upande wa magharibi.*+  Hakuna yeyote atakayekushinda sikuzote za maisha yako.+ Nitakuwa pamoja nawe kama nilivyokuwa pamoja na Musa.+ Sitakutupa wala kukuacha.+  Uwe jasiri na imara,+ kwa sababu ni wewe utakayewaongoza watu hawa kuirithi nchi niliyowaapia mababu zao kwamba nitawapa.+  “Ila tu uwe jasiri na imara kabisa, na ufuate kwa uangalifu Sheria yote kama Musa mtumishi wangu alivyokuamuru. Usiende kushoto wala kulia,+ ili utende kwa hekima mahali popote utakapoenda.+  Kitabu hiki cha Sheria kisiondoke kinywani mwako,+ ni lazima ukisome kwa sauti ya chini* mchana na usiku ili ufuate kwa uangalifu mambo yote yaliyoandikwa humo;+ ndipo utakapofanikisha njia yako na kutenda kwa hekima.+  Je, si mimi niliyekuamuru uwe jasiri na imara? Basi uwe jasiri na imara. Usitetemeke wala kuogopa, kwa maana mimi Yehova Mungu wako nipo pamoja nawe mahali popote utakapoenda.”+ 10  Ndipo Yoshua akawaamuru viongozi wa watu akisema, 11  “Piteni katika kambi yote na kuwaamuru watu hivi: ‘Tayarisheni vyakula, kwa sababu baada ya siku tatu mtavuka Mto Yordani ili kuingia na kuimiliki nchi ambayo Yehova Mungu wenu anawapa.’”+ 12  Kisha Yoshua akawaambia hivi watu wa kabila la Rubeni, Gadi, na nusu ya kabila la Manase: 13  “Kumbukeni amri ambayo Musa mtumishi wa Yehova aliwapa aliposema,+ ‘Yehova Mungu wenu anawapumzisha, naye amewapa nchi hii. 14  Wake zenu, watoto wenu, na wanyama wenu wa kufugwa watakaa katika nchi ambayo Musa amewapa upande huu* wa Yordani,+ lakini ninyi nyote mashujaa hodari+ mnapaswa kuvuka na kuwatangulia ndugu zenu mkiwa mmejipanga kivita.+ Mnapaswa kuwasaidia 15  mpaka Yehova atakapowapa ndugu zenu mahali pa kupumzika, kama alivyowapa ninyi, nao pia wamiliki nchi ambayo Yehova Mungu wenu anawapa. Kisha rudini na kuimiliki nchi yenu ambayo Musa mtumishi wa Yehova aliwapa upande wa mashariki wa Yordani.’”+ 16  Wakamwambia Yoshua: “Tutafanya yote ambayo umetuamuru, na tutaenda mahali popote unapotaka twende.+ 17  Kama tulivyomtii Musa katika mambo yote, ndivyo tutakavyokutii. Yehova Mungu wako na awe pamoja nawe kama alivyokuwa pamoja na Musa.+ 18  Mtu yeyote atakayeasi agizo lako na asiyetii amri yoyote utakayotoa atauawa.+ Lakini uwe jasiri na imara.”+

Maelezo ya Chini

Au “Yehoshua,” maana yake “Yehova Ni Wokovu.”
Yaani, Mediterania.
Au “kuelekea machweo ya jua.”
Au “ukitafakari.”
Yaani, upande wa mashariki.