Yoshua 12:1-24

  • Wafalme wa mashariki mwa Yordani washindwa (1-6)

  • Wafalme wa magharibi mwa Yordani washindwa (7-24)

12  Basi hawa ndio wafalme ambao Waisraeli waliwashinda na kumiliki nchi yao upande wa mashariki wa Yordani, kuanzia Bonde* la Arnoni+ hadi Mlima Hermoni+ na eneo lote la Araba kuelekea upande wa mashariki:+  Mfalme Sihoni+ wa Waamori, aliyeishi Heshboni na kutawala kutoka Aroeri,+ kwenye ukingo wa Bonde* la Arnoni,+ na kutoka katikati ya bonde hilo, na nusu ya Gileadi hadi Bonde la Yaboki, kwenye mpaka wa Waamoni.  Alitawala pia Araba hadi Bahari ya Kinerethi*+ kuelekea mashariki hadi Bahari ya Araba, yaani, Bahari ya Chumvi, upande wa mashariki kuelekea Beth-yeshimothi, na kuelekea kusini chini ya miteremko ya Pisga.+  Pia, eneo la Mfalme Ogu+ wa Bashani, aliyekuwa kati ya Warefaimu+ waliosalia, ambaye aliishi Ashtarothi na Edrei  na kutawala katika eneo la Mlima Hermoni, Saleka, na Bashani yote,+ hadi mpaka wa Wageshuri na Wamaakathi,+ na nusu ya Gileadi, hadi katika eneo la Mfalme Sihoni wa Heshboni.+  Musa mtumishi wa Yehova pamoja na Waisraeli waliwashinda,+ kisha Musa mtumishi wa Yehova akawapa nchi hiyo watu wa kabila la Rubeni, Gadi, na nusu ya kabila la Manase ili waimiliki.+  Hawa ndio wafalme ambao Yoshua na Waisraeli waliwashinda upande wa magharibi wa Yordani, kuanzia Baal-gadi+ katika Bonde la Lebanoni+ hadi Mlima Halaki,+ unaopanda hadi Seiri,+ halafu Yoshua akayapa makabila ya Israeli nchi yao ili waimiliki na kugawana kulingana na makabila yao,+  katika eneo lenye milima, Shefela, Araba, kwenye miteremko, nyikani, na katika Negebu+—nchi ya Wahiti, Waamori,+ Wakanaani, Waperizi, Wahivi, na Wayebusi:+   Mfalme wa Yeriko,+ mfalme wa Ai,+ jiji lililokuwa kando ya Betheli, 10  mfalme wa Yerusalemu, mfalme wa Hebroni,+ 11  mfalme wa Yarmuthi, mfalme wa Lakishi, 12  mfalme wa Egloni, mfalme wa Gezeri,+ 13  mfalme wa Debiri,+ mfalme wa Gederi, 14  mfalme wa Horma, mfalme wa Aradi, 15  mfalme wa Libna,+ mfalme wa Adulamu, 16  mfalme wa Makeda,+ mfalme wa Betheli,+ 17  mfalme wa Tapua, mfalme wa Heferi, 18  mfalme wa Afeki, mfalme wa Lasharoni, 19  mfalme wa Madoni, mfalme wa Hasori,+ 20  mfalme wa Shimron-meroni, mfalme wa Akshafi, 21  mfalme wa Taanaki, mfalme wa Megido, 22  mfalme wa Kedeshi, mfalme wa Yokneamu+ kule Karmeli, 23  mfalme wa Dori kwenye miteremko ya Dori,+ mfalme wa Goiimu kule Gilgali, 24  na mfalme wa Tirsa; jumla ya wafalme hao ni 31.

Maelezo ya Chini

Au “Korongo.”
Au “Korongo.”
Yaani, Ziwa Genesareti, au Bahari ya Galilaya.