Yoshua 13:1-33

  • Maeneo ambayo hayajatekwa (1-7)

  • Kugawanywa kwa maeneo mashariki mwa Yordani (8-14)

  • Urithi wa kabila la Rubeni (15-23)

  • Urithi wa kabila la Gadi (24-28)

  • Urithi wa kabila la Manase upande wa mashariki (29-32)

  • Yehova ni urithi wa Walawi (33)

13  Basi Yoshua alikuwa amezeeka na umri wake ulikuwa umesonga sana.+ Kwa hiyo Yehova akamwambia, “Umezeeka na umri wako umesonga sana; na bado hamjamiliki* sehemu kubwa ya nchi.  Hii ndiyo nchi ambayo imebaki:+ maeneo yote ya Wafilisti na ya Wageshuri+  (kuanzia kijito cha Mto Nile* kilicho upande wa mashariki wa* Misri hadi kwenye mpaka wa Ekroni upande wa kaskazini, eneo lililoonwa kuwa sehemu ya Wakanaani)+ kutia ndani eneo la watawala watano wa Wafilisti+—Wagaza, Waashdodi,+ Waashkeloni,+ Wagathi,+ Waekroni;+ eneo la Waavimu+  upande wa kusini; nchi yote ya Wakanaani; Meara, ambayo ni ya Wasidoni,+ hadi Afeki, kwenye mpaka wa Waamori;  nchi ya Wagebali+ na nchi yote ya Lebanoni kuelekea mashariki, kuanzia Baal-gadi chini ya Mlima Hermoni hadi Lebo-hamathi;*+  wakaaji wote wa eneo lenye milima kuanzia Lebanoni+ hadi Misrefoth-maimu;+ na Wasidoni wote.+ Nitawafukuza* mbele ya Waisraeli.+ Utaigawanya nchi hiyo na kuwapa Waisraeli kuwa urithi wao, kama nilivyokuamuru.+  Na sasa yagawie makabila tisa pamoja na nusu ya kabila la Manase nchi hii kuwa urithi wao.”+  Nusu iliyobaki ya kabila la Manase, pamoja na watu wa kabila la Rubeni na Gadi walichukua urithi wao waliopewa na Musa upande wa mashariki wa Yordani, kama tu Musa mtumishi wa Yehova alivyowapa:+  kuanzia Aroeri,+ kwenye ukingo wa Bonde* la Arnoni,+ na jiji lililo katikati ya bonde hilo, na uwanda wote wa juu wa Medeba hadi Diboni; 10  na majiji yote ya Mfalme Sihoni wa Waamori, aliyetawala Heshboni, hadi kwenye mpaka wa Waamoni;+ 11  pia Gileadi na eneo la Wageshuri na Wamaakathi+ na eneo lote la Mlima Hermoni na Bashani+ hadi Saleka;+ 12  ufalme wote wa Ogu kule Bashani, aliyetawala Ashtarothi na Edrei. (Alikuwa kati ya Warefaimu waliobaki.)+ Musa aliwashinda na kuwafukuza.*+ 13  Lakini Waisraeli hawakuwafukuza*+ Wageshuri na Wamaakathi, kwa kuwa Wageshuri na Wamaakathi wanaishi miongoni mwa Waisraeli mpaka leo. 14  Musa hakuwapa watu wa kabila la Lawi urithi.+ Urithi wao ni dhabihu zinazochomwa kwa moto zinazotolewa kwa Yehova Mungu wa Israeli,+ kama alivyowaahidi.+ 15  Ndipo Musa akawapa urithi watu wa kabila la Rubeni kulingana na koo zao, 16  na eneo lao lilianzia Aroeri, kwenye ukingo wa Bonde* la Arnoni, na jiji lililo katikati ya bonde hilo, na uwanda wote wa juu wa Medeba; 17  Heshboni na miji yake yote+ iliyo kwenye uwanda wa juu, Diboni, Bamoth-baali, Beth-baal-meoni,+ 18  Yahazi,+ Kedemothi,+ Mefaathi,+ 19  Kiriathaimu, Sibma,+ na Sereth-shahari kwenye mlima wa bondeni,* 20  Beth-peori, miteremko ya Pisga,+ Beth-yeshimothi,+ 21  majiji yote kwenye uwanda wa juu, na eneo lote la Mfalme Sihoni wa Waamori, aliyetawala Heshboni.+ Musa alimshinda yeye+ pamoja na wakuu wa Midiani, yaani, Evi, Rekemu, Suri, Huru, na Reba,+ watawala vibaraka* wa Sihoni waliokaa nchini humo. 22  Waisraeli walimuua kwa upanga Balaamu+ mwana wa Beori, yule mbashiri,*+ pamoja na watu wengine. 23  Na mpaka wa kabila la Rubeni ulikuwa Yordani; na eneo hilo lilikuwa urithi wa kabila la Rubeni kulingana na koo zao, pamoja na miji na vijiji vyake. 24  Pia, Musa akawapa urithi watu wa kabila la Gadi, kulingana na koo zao, 25  na eneo lao lilitia ndani Yazeri+ na majiji yote ya Gileadi na nusu ya nchi ya Waamoni+ hadi Aroeri, mbele ya Raba;+ 26  na kutoka Heshboni+ hadi Ramath-mispe na Betonimu, na kutoka Mahanaimu+ hadi mpaka wa Debiri; 27  na bondeni,* Beth-haramu, Beth-nimra,+ Sukothi,+ na Safoni, eneo lililobaki la Mfalme Sihoni wa Heshboni,+ na Mto Yordani ulikuwa mpaka ulioanzia upande wa chini wa Bahari ya Kinerethi,*+ upande wa mashariki wa Yordani. 28  Huo ndio uliokuwa urithi wa kabila la Gadi kulingana na koo zao, pamoja na miji na vijiji vyake. 29  Pia, Musa akawapa urithi nusu ya watu wa kabila la Manase, ukawa urithi wao kulingana na koo zao.+ 30  Na eneo lao lilianzia Mahanaimu+ na eneo lote la Bashani, eneo lote la Mfalme Ogu wa Bashani, na vijiji vyote vya mahema vya Yairi+ kule Bashani, miji 60. 31  Na nusu ya eneo la Gileadi, na Ashtarothi na Edrei,+ majiji ya ufalme wa Ogu kule Bashani, yalichukuliwa na wana wa Makiri+ mwana wa Manase, yaani, nusu ya wana wa Makiri kulingana na koo zao. 32  Huo ndio urithi ambao Musa aliwapa katika maeneo tambarare ya jangwani ya Moabu ng’ambo ya Yordani, upande wa mashariki wa Yeriko.+ 33  Lakini Musa hakuwapa urithi watu wa kabila la Lawi.+ Yehova Mungu wa Israeli ndiye urithi wao, kama alivyowaahidi.+

Maelezo ya Chini

Au “hamjateka.”
Au “mbele ya.”
Au “kijito cha Shihori.”
Au “njia ya kuingia Hamathi.”
Au “Nitachukua nchi yao.”
Au “Korongo.”
Au “kuchukua nchi yao.”
Au “hawakuchukua nchi ya.”
Au “Korongo.”
Au “nchi tambarare ya chini.”
Yaani, wafalme waliokuwa chini ya Sihoni.
Au “mwaguzi.”
Yaani, Ziwa Genesareti, au Bahari ya Galilaya.
Au “nchi tambarare ya chini.”