Yoshua 15:1-63

  • Urithi wa kabila la Yuda (1-12)

  • Binti ya Kalebu apewa eneo (13-19)

  • Majiji ya Yuda (20-63)

15  Nchi ambayo watu wa kabila la Yuda waligawiwa*+ kwa ajili ya koo zao ilifika kwenye mpaka wa Edomu,+ nyika ya Zini, hadi upande wa kusini kabisa wa Negebu.  Mpaka wao wa kusini ulianzia mwisho wa Bahari ya Chumvi,+ yaani, kuanzia mahali ambapo mto unaingia baharini upande wa kusini.  Na uliendelea upande wa kusini kwenye mwinuko wa Akrabimu,+ ukavuka hadi Zini, na kupanda kutoka kusini hadi Kadesh-barnea,+ kufika Hezroni, Adari, na kuzunguka hadi Karka.  Kisha ukaendelea hadi Asimoni+ na kufika kwenye Korongo la Misri,+ nao ukafikia mwisho kwenye Bahari.* Huo ndio uliokuwa mpaka wao wa kusini.  Mpaka wa mashariki ulianzia kwenye Bahari ya Chumvi hadi mahali ambapo Mto Yordani unaingia katika Bahari ya Chumvi, na mpaka wa kaskazini ulianzia mahali ambapo Mto Yordani unaingia katika Bahari ya Chumvi.+  Mpaka huo ulipanda hadi Beth-hogla+ na kuvuka upande wa kaskazini wa Beth-araba,+ nao uliendelea juu mpaka kwenye jiwe la Bohani+ mwana wa Rubeni.  Na mpaka huo ukapanda hadi Debiri katika Bonde la* Akori+ na kugeuka kuelekea kaskazini hadi Gilgali,+ mbele ya njia inayopanda kuelekea Adumimu, ambayo iko upande wa kusini wa bonde la mto, kisha ukaendelea hadi kwenye chemchemi ya En-shemeshi+ na kufikia mwisho kule En-rogeli.+  Na mpaka huo ukapanda hadi Bonde la Mwana wa Hinomu+ kwenye mteremko wa jiji la Wayebusi+ upande wa kusini, yaani, Yerusalemu,+ nao ukapanda hadi juu ya mlima unaotazamana na Bonde la Hinomu upande wa magharibi, yaani, mwisho kabisa wa Bonde la* Refaimu upande wa kaskazini.  Mpaka huo ulianzia juu ya mlima hadi chemchemi ya Neftoa+ mpaka kwenye majiji ya Mlima Efroni; nao ulifika Baala, yaani, Kiriath-yearimu.+ 10  Kisha ukazunguka kutoka Baala kuelekea upande wa magharibi hadi Mlima Seiri, ukaendelea hadi kwenye mteremko wa Mlima Yearimu upande wa kaskazini, yaani, Kesaloni, nao ukashuka hadi Beth-shemeshi+ na kuendelea hadi Timna.+ 11  Kisha ukaendelea hadi kwenye mteremko wa kaskazini wa Ekroni,+ hadi Shikeroni, kufika kwenye Mlima Baala na kuendelea hadi Yabneeli, nao ulifikia mwisho kwenye bahari. 12  Mpaka wa magharibi ulikuwa Bahari Kuu*+ na pwani yake. Hiyo ndiyo iliyokuwa mipaka yote ya wazao wa Yuda kulingana na koo zao. 13  Naye Yoshua akampa Kalebu+ mwana wa Yefune sehemu ya nchi kati ya wazao wa Yuda kama Yehova alivyomwagiza Yoshua, yaani, eneo la Kiriath-arba (Arba alikuwa baba ya Waanaki), yaani, Hebroni.+ 14  Basi Kalebu aliwafukuza kutoka Hebroni wana watatu wa Anaki:+ Sheshai, Ahimani, Talmai,+ yaani, wazao wa Anaki. 15  Kisha akapanda kutoka huko na kwenda kuwashambulia wakaaji wa Debiri.+ (Hapo awali Debiri liliitwa Kiriath-seferi.) 16  Ndipo Kalebu akasema: “Yeyote atakayeshambulia na kuteka jiji la Kiriath-seferi, nitampa binti yangu Aksa awe mke wake.” 17  Othnieli+ mwana wa Kenasi,+ ndugu ya Kalebu, akaliteka. Kwa hiyo akampa Aksa+ binti yake awe mke wake. 18  Mwanamke huyo alipokuwa akienda nyumbani kwake, akamsihi mume wake amwombe baba* yake shamba. Kisha mwanamke huyo akashuka kutoka juu ya punda wake.* Kalebu akamuuliza: “Unataka nini?”+ 19  Akamwambia: “Tafadhali nibariki, kwa maana umenipa shamba upande wa kusini;* nipe pia Guloth-maimu.”* Basi Kalebu akampa Gulothi ya Juu na Gulothi ya Chini. 20  Huo ndio uliokuwa urithi wa watu wa kabila la Yuda kulingana na koo zao. 21  Na majiji yaliyokuwa upande wa kusini kabisa wa kabila la Yuda kuelekea mpaka wa Edomu+ yalikuwa Kabzeeli, Ederi, Yaguri, 22  Kina, Dimona, Adada, 23  Kedeshi, Hasori, Ithnani, 24  Zifu, Telemu, Bealothi, 25  Hasor-hadata, na Kerioth-hesroni, yaani, Hasori, 26  Amamu, Shema, Molada,+ 27  Hasar-gada, Heshmoni, Beth-peleti,+ 28  Hasar-shuali, Beer-sheba,+ Biziothia, 29  Baala, Iimu, Esemu, 30  Eltoladi, Kesili, Horma,+ 31  Siklagi,+ Madmana, Sansana, 32  Lebaothi, Shilhimu, Aini, na Rimoni+—jumla ya majiji 29, pamoja na vijiji vyake. 33  Majiji yaliyokuwa Shefela+ yalikuwa Eshtaoli, Sora,+ Ashna, 34  Zanoa, En-ganimu, Tapua, Enamu, 35  Yarmuthi, Adulamu,+ Soko, Azeka,+ 36  Shaaraimu,+ Adithaimu, na Gedera, na Gederothaimu*—majiji 14 na vijiji vyake. 37  Senani, Hadasha, Migdal-gadi, 38  Dileani, Mispe, Yoktheeli, 39  Lakishi,+ Boskathi, Egloni, 40  Kaboni, Lahmamu, Kitilishi, 41  Gederothi, Beth-dagoni, Naama, na Makeda+—majiji 16 na vijiji vyake. 42  Libna,+ Etheri, Ashani,+ 43  Ifta, Ashna, Nesibu, 44  Keila, Akzibu, na Maresha⁠—majiji tisa na vijiji vyake. 45  Ekroni na miji na vijiji vyake; 46  kuanzia Ekroni kuelekea magharibi, miji yote iliyo kando ya Ashdodi na vijiji vyake. 47  Ashdodi,+ miji na vijiji vyake; Gaza,+ miji na vijiji vyake, hadi kwenye Bonde la Misri, na Bahari Kuu,* na eneo jirani.+ 48  Na katika eneo lenye milima, Shamiri, Yatiri,+ Soko, 49  Dana, Kiriath-sana, yaani, Debiri, 50  Anabu, Eshtemo,+ Animu, 51  Gosheni,+ Holoni, na Gilo+—majiji 11 na vijiji vyake. 52  Arabu, Duma, Eshani, 53  Yanimu, Beth-tapua, Afeka, 54  Humta, Kiriath-arba, yaani, Hebroni,+ na Siori—majiji tisa na vijiji vyake. 55  Maoni,+ Karmeli, Zifu,+ Yuta, 56  Yezreeli, Yokdeamu, Zanoa, 57  Kayini, Gibea, Timna+—majiji kumi na vijiji vyake. 58  Halhuli, Beth-suri, Gedori, 59  Maarathi, Beth-anothi, na Eltekoni—majiji sita na vijiji vyake. 60  Kiriath-baali, yaani, Kiriath-yearimu,+ na Raba—majiji mawili na vijiji vyake. 61  Katika nyika, Beth-araba,+ Midini, Sekaka, 62  Nibshani, Jiji la Chumvi, na En-gedi+—majiji sita na vijiji vyake. 63  Lakini watu wa kabila la Yuda hawakuwafukuza+ Wayebusi+ waliokuwa wakikaa Yerusalemu,+ basi tangu wakati huo Wayebusi wanakaa Yerusalemu pamoja na watu wa kabila la Yuda.

Maelezo ya Chini

Au “waligawiwa kwa kura.”
Yaani, Bahari Kuu, Mediterania.
Au “Nchi Tambarare ya Chini ya.”
Au “Nchi Tambarare ya Chini ya.”
Yaani, Mediterania.
Au labda, “akapiga makofi akiwa juu ya punda ili kumwita baba yake.”
Yaani, “baba ya Aksa.”
Au “eneo la Negebu.”
Yaani, “Chemchemi za Maji.”
Au labda, “Gedera na mazizi yake ya kondoo.”
Yaani, Mediterania.