Yoshua 21:1-45

  • Majiji ya Walawi (1-42)

    • Ya wazao wa Haruni (9-19)

    • Ya Wakohathi waliobaki (20-26)

    • Ya Wagershoni (27-33)

    • Ya Wamerari (34-40)

  • Ahadi za Yehova zatimia (43-45)

21  Viongozi wa koo* za Walawi wakaenda kwa kuhani Eleazari+ na Yoshua mwana wa Nuni na viongozi wa koo* za makabila ya Israeli,  wakawaambia hivi huko Shilo+ katika nchi ya Kanaani: “Yehova aliamuru kupitia Musa tupewe majiji ya kuishi na malisho ya mifugo yetu.”+  Basi kwa agizo la Yehova, Waisraeli wakawapa Walawi majiji hayo+ na malisho yake kutoka katika urithi wao wenyewe.+  Kura ya kwanza ilikuwa ya koo za Wakohathi,+ na Walawi waliokuwa wazao wa kuhani Haruni walipewa majiji 13 kwa kura katika maeneo ya kabila la Yuda,+ kabila la Simeoni,+ na kabila la Benjamini.+  Na Wakohathi waliobaki walipewa majiji kumi kwa kura katika maeneo ya koo za kabila la Efraimu,+ Dani, na katika eneo la nusu ya kabila la Manase.+  Na Wagershoni+ walipewa majiji 13 kwa kura katika maeneo ya koo za kabila la Isakari, Asheri, Naftali, na katika eneo la nusu ya kabila la Manase kule Bashani.+  Na Wamerari+ walipewa majiji 12 kulingana na koo zao katika maeneo ya kabila la Rubeni, Gadi, na Zabuloni.+  Hivyo Waisraeli wakawapa Walawi majiji hayo na malisho yake kwa kura kama Yehova alivyokuwa ameamuru kupitia Musa.+  Yafuatayo ni majina ya majiji+ katika maeneo ya kabila la Yuda na kabila la Simeoni ambayo waliwapa 10  wana wa Haruni wa koo za Walawi Wakohathi, kwa kuwa kura ya kwanza ilikuwa yao. 11  Waliwapa Kiriath-arba+ (Arba alikuwa baba ya Waanaki), yaani, jiji la Hebroni,+ katika eneo lenye milima la Yuda, na malisho yake yote. 12  Lakini walikuwa wamempa Kalebu mwana wa Yefune mashamba ya jiji hilo na vijiji vyake kuwa urithi wake.+ 13  Nao wakawapa wana wa kuhani Haruni jiji la makimbilio kwa ajili ya muuaji,+ yaani, jiji la Hebroni,+ na malisho yake, pia Libna+ na malisho yake, 14  Yatiri+ na malisho yake, Eshtemoa+ na malisho yake, 15  Holoni+ na malisho yake, Debiri+ na malisho yake, 16  Aini+ na malisho yake, Yuta+ na malisho yake, na Beth-shemeshi na malisho yake—majiji tisa katika maeneo ya makabila hayo mawili. 17  Na katika eneo la kabila la Benjamini: Gibeoni+ na malisho yake, Geba na malisho yake,+ 18  Anathothi+ na malisho yake, na Almoni na malisho yake—majiji manne. 19  Wazao wa Haruni, makuhani, walipewa jumla ya majiji 13 na malisho yake.+ 20  Na Walawi waliobaki wa koo za Wakohathi walipewa majiji kwa kura katika eneo la kabila la Efraimu. 21  Waliwapa jiji la makimbilio kwa ajili ya muuaji,+ yaani, jiji la Shekemu+ na malisho yake katika eneo lenye milima la Efraimu, Gezeri+ na malisho yake, 22  Kibsaimu na malisho yake, na Beth-horoni+ na malisho yake—majiji manne. 23  Na katika eneo la kabila la Dani: Elteke na malisho yake, Gibethoni na malisho yake, 24  Aiyaloni+ na malisho yake, Gath-rimoni na malisho yake—majiji manne. 25  Na katika eneo la nusu ya kabila la Manase: Taanaki+ na malisho yake na Gath-rimoni na malisho yake—majiji mawili. 26  Koo zilizobaki za Wakohathi zilipewa jumla ya majiji kumi na malisho yake. 27  Na Wagershoni+ wa koo za Walawi walipewa jiji la makimbilio kwa ajili ya muuaji katika eneo la nusu ya kabila la Manase, yaani, jiji la Golani+ kule Bashani pamoja na malisho yake, na Beeshtera na malisho yake—majiji mawili. 28  Na katika eneo la kabila la Isakari:+ Kishioni na malisho yake, Daberathi+ na malisho yake, 29  Yarmuthi na malisho yake, na En-ganimu na malisho yake—majiji manne. 30  Na katika eneo la kabila la Asheri:+ Mishali na malisho yake, Abdoni na malisho yake, 31  Helkathi+ na malisho yake, na Rehobu+ na malisho yake—majiji manne. 32  Na katika eneo la kabila la Naftali: jiji la makimbilio+ kwa ajili ya muuaji, yaani, jiji la Kedeshi+ kule Galilaya na malisho yake, Hamoth-dori na malisho yake, na Kartani na malisho yake—majiji matatu. 33  Wagershoni walipewa jumla ya majiji 13 na malisho yake kulingana na koo zao. 34  Na koo za Wamerari,+ yaani, Walawi waliobaki, walipewa Yokneamu+ na malisho yake, Karta na malisho yake, katika eneo la kabila la Zabuloni,+ 35  Dimna na malisho yake, na Nahalali+ na malisho yake—majiji manne. 36  Na katika eneo la kabila la Rubeni: Beseri+ na malisho yake, Yahazi na malisho yake,+ 37  Kedemothi na malisho yake, na Mefaathi na malisho yake—majiji manne. 38  Na katika eneo la kabila la Gadi:+ jiji la makimbilio kwa ajili ya muuaji, yaani, jiji la Ramothi kule Gileadi+ na malisho yake, Mahanaimu+ na malisho yake, 39  Heshboni+ na malisho yake, Yazeri+ na malisho yake—jumla ya majiji manne. 40  Majiji yote ambayo Wamerari walipewa kwa kura kulingana na koo zao, yaani, koo zilizobaki za Walawi, yalikuwa majiji 12. 41  Majiji yote ambayo Walawi walipewa katika maeneo ya Waisraeli yalikuwa majiji 48 pamoja na malisho yake.+ 42  Kila moja la majiji hayo lilizungukwa na malisho—hivyo ndivyo ilivyokuwa katika majiji hayo yote. 43  Basi Yehova akawapa Waisraeli nchi yote ambayo aliapa kwamba angewapa mababu zao,+ wakaimiliki na kuishi humo.+ 44  Yehova akawapa pia amani katika nchi yote, kama alivyowaapia mababu zao,+ na hakuna adui hata mmoja kati ya maadui wao wote aliyeweza kuwashinda.+ Yehova aliwatia maadui wao wote mikononi mwao.+ 45  Hakuna ahadi hata moja iliyokosa kutimia kati ya ahadi zote nzuri ambazo Yehova aliwaahidi Waisraeli; zote zilitimia.+

Maelezo ya Chini

Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.