Yoshua 23:1-16

  • Maneno ya mwisho ya Yoshua kwa viongozi wa Waisraeli (1-16)

    • Hakuna ahadi yoyote ya Yehova iliyokosa kutimia (14)

23  Siku nyingi baada ya Yehova kuwapa Waisraeli amani+ kwa kuwaokoa kutoka kwa maadui wote waliowazunguka, Yoshua alipokuwa amezeeka na umri wake kusonga sana,+  Yoshua aliwaita Waisraeli wote,+ wazee wao, viongozi wao, waamuzi wao, na wakuu wao,+ akawaambia hivi: “Nimezeeka na umri wangu umesonga sana.  Ninyi wenyewe mmeona mambo yote ambayo Yehova Mungu wenu aliyatendea mataifa haya yote kwa ajili yenu, kwa sababu Yehova Mungu wenu ndiye aliyekuwa akiwapigania.+  Tazameni, niliwagawia kwa kura+ nchi ya mataifa yanayobaki na pia nchi ya mataifa yote ambayo niliyaangamiza+ ili iwe urithi wa makabila yenu,+ kuanzia Yordani mpaka Bahari Kuu* upande wa magharibi.  Na Yehova Mungu wenu ndiye aliyekuwa akiwafukuza kutoka mbele yenu,+ naye akawaondoa* kwa ajili yenu, nanyi mkamiliki nchi yao, kama Yehova Mungu wenu alivyowaahidi.+  “Basi iweni jasiri sana mshike na kutekeleza mambo yote yaliyoandikwa katika kitabu cha Sheria+ ya Musa, msiiache kamwe na kwenda kulia wala kushoto,+  na msishirikiane kamwe na mataifa haya+ yaliyobaki kati yenu. Hampaswi hata kutaja majina ya miungu yao+ wala kuapa kwa majina hayo, na hampaswi kamwe kuiabudu au kuiinamia.+  Bali mnapaswa kushikamana na Yehova Mungu wenu,+ kama vile ambavyo mmekuwa mkifanya mpaka sasa.  Yehova atafukuza mataifa makubwa na yenye nguvu kutoka mbele yenu,+ kwa kuwa mpaka sasa hakuna mtu yeyote ambaye amewashinda ninyi.+ 10  Mtu mmoja tu kati yenu atawakimbiza watu elfu,+ kwa sababu Yehova Mungu wenu anawapigania,+ kama alivyowaahidi.+ 11  Basi jilindeni daima*+ kwa kumpenda Yehova Mungu wenu.+ 12  “Lakini mkimwacha na kushikamana na watu wa mataifa haya yaliyobaki+ na kuoana nao+ na kushirikiana nao, 13  mjue kwa hakika kwamba Yehova Mungu wenu hataendelea kuyafukuza* mataifa haya kwa ajili yenu.+ Yatakuwa mtego wa kuwanasa, nayo yatakuwa mjeledi wa kuwachapa mbavuni+ na miiba machoni mwenu mpaka mtakapoangamia kutoka katika nchi hii nzuri ambayo Yehova Mungu wenu amewapa. 14  “Basi sasa nakaribia kufa,* nanyi mnajua vizuri kwa mioyo yenu yote na kwa nafsi* zenu zote kwamba halikukosa kutimia hata neno moja kati ya ahadi zote nzuri ambazo Yehova Mungu wenu aliwaahidi. Zote zimetimia kwenu. Halikukosa kutimia hata neno moja aliloahidi.+ 15  Lakini kama zilivyotimia ahadi zote nzuri alizowaahidi Yehova Mungu wenu,+ vivyo hivyo Yehova atawaletea misiba yote aliyoahidi* na kuwaangamiza kutoka katika nchi hii nzuri ambayo Yehova Mungu wenu amewapa.+ 16  Mkivunja agano la Yehova Mungu wenu alilowaamuru mshike na mkienda kuabudu miungu mingine na kuiinamia, hasira ya Yehova itawaka dhidi yenu+ nanyi mtaangamia haraka kutoka katika nchi nzuri ambayo amewapa.”+

Maelezo ya Chini

Yaani, Mediterania.
Au “akachukua nchi yao.”
Au “lindeni nafsi zenu kwa uangalifu.”
Au “kuchukua nchi ya.”
Tnn., “Leo ninafuata njia ya dunia yote.”
Angalia Kamusi.
Au “mabaya yote.”