Yoshua 24:1-33

  • Yoshua awakumbusha Waisraeli historia yao (1-13)

  • Awahimiza wamtumikie Yehova (14-24)

    • “Mimi na familia yangu, tutamtumikia Yehova” (15)

  • Yoshua afanya agano na Waisraeli (25-28)

  • Yoshua afa na kuzikwa (29-31)

  • Mifupa ya Yosefu yazikwa Shekemu (32)

  • Eleazari afa na kuzikwa (33)

24  Kisha Yoshua akayakusanya makabila yote ya Israeli huko Shekemu, akawaita wazee wote wa Israeli, viongozi wao, waamuzi wao, na wakuu wao,+ nao wakasimama mbele za Mungu wa kweli.  Yoshua akawaambia watu wote, “Hivi ndivyo anavyosema Yehova Mungu wa Israeli, ‘Zamani za kale+ mababu zenu,+ kutia ndani Tera baba ya Abrahamu na baba ya Nahori, waliishi ng’ambo ya Mto,* nao walikuwa wakiabudu miungu mingine.+  “‘Baada ya muda nilimtoa babu yenu Abrahamu+ ng’ambo ya Mto* na kumtembeza katika nchi yote ya Kanaani na kuzidisha uzao wake.*+ Nikampa Isaka;+  naye Isaka nikampa Yakobo na Esau.+ Baadaye nikampa Esau Mlima Seiri ili aumiliki;+ na Yakobo na wanawe wakashuka Misri.+  Baadaye niliwatuma Musa na Haruni,+ nikailetea Misri mapigo,+ kisha nikawatoa ninyi.  Nilipokuwa nikiwatoa mababu zenu Misri,+ mlifika baharini, Wamisri waliwafuatia wakiwa na magari ya vita na askari wapanda farasi mpaka kwenye Bahari Nyekundu.*+  Na mababu zenu wakaanza kumlilia Yehova,+ basi akaweka giza kati yenu na Wamisri na kuileta bahari juu yao ikawafunika Wamisri,+ na mliona kwa macho yenu wenyewe mambo niliyoyafanya huko Misri.+ Kisha mkaishi nyikani kwa miaka mingi.*+  “‘Nami nikawaleta katika nchi ya Waamori waliokuwa wakiishi ng’ambo ya* Yordani, nao wakapigana nanyi.+ Lakini niliwatia mikononi mwenu ili mmiliki nchi yao, nikawaangamiza kutoka mbele yenu.+  Kisha Balaki mwana wa Sipori, mfalme wa Moabu, akaja kupigana na Israeli. Basi akamwita Balaamu mwana wa Beori ili awalaani ninyi.+ 10  Lakini sikumsikiliza Balaamu.+ Basi akawabariki ninyi tena na tena,+ nami nikawaokoa kutoka mikononi mwake.+ 11  “‘Kisha mkavuka Yordani+ na kufika Yeriko.+ Nao viongozi* wa Yeriko, Waamori, Waperizi, Wakanaani, Wahiti, Wagirgashi, Wahivi, na Wayebusi wakapigana nanyi, lakini nikawatia mikononi mwenu.+ 12  Basi nikawafanya wavunjike moyo* kabla ya ninyi kufika, nao wakakimbia+—wafalme wawili wa Waamori. Hamkuwashinda kwa sababu ya upanga wenu wala upinde wenu.+ 13  Kwa hiyo niliwapa nchi ambayo hamkuipata kwa jasho lenu na majiji ambayo hamkujenga,+ nanyi mkakaa humo. Mnakula matunda ya mizabibu na ya mizeituni ambayo hamkupanda.’+ 14  “Kwa hiyo, mwogopeni Yehova na kumtumikia kwa utimilifu* na uaminifu,*+ ondoeni miungu ambayo mababu zenu waliabudu ng’ambo ya Mto* na nchini Misri,+ nanyi mtumikieni Yehova. 15  Sasa ikiwa mnaona ni vibaya kumtumikia Yehova, chagueni leo yule mtakayemtumikia,+ iwe ni miungu ambayo mababu zenu waliabudu ng’ambo ya Mto*+ au miungu ya Waamori mnaoishi katika nchi yao.+ Lakini mimi na familia* yangu, tutamtumikia Yehova.” 16  Ndipo watu wakajibu hivi: “Hatuwezi kamwe kuwazia kumwacha Yehova na kuabudu miungu mingine. 17  Yehova Mungu wetu ndiye aliyetutoa sisi na mababu zetu katika nchi ya Misri,+ katika nyumba ya utumwa,+ na kufanya miujiza mikubwa mbele ya macho yetu+ na kutulinda katika safari yetu yote na miongoni mwa watu wote ambao tulipita katikati yao.+ 18  Yehova aliyafukuza mataifa yote, kutia ndani Waamori, walioishi katika nchi hii kabla yetu. Kwa hiyo, sisi pia tutamtumikia Yehova, kwa sababu yeye ni Mungu wetu.” 19  Kisha Yoshua akawaambia watu, “Hamwezi kumtumikia Yehova, kwa maana yeye ni Mungu mtakatifu;+ ni Mungu anayetaka watu wamwabudu yeye peke yake.+ Hatawasamehe uasi wenu na dhambi zenu.+ 20  Mkimwacha Yehova na kuabudu miungu ya kigeni, yeye pia atawaacha na kuwaangamiza hata ingawa amewatendea mema.”+ 21  Lakini watu wakamwambia hivi Yoshua: “Hapana, tutamtumikia Yehova!”+ 22  Basi Yoshua akawaambia, “Ninyi ni mashahidi dhidi yenu wenyewe kwamba mmechagua kwa hiari yenu kumtumikia Yehova.”+ Nao wakajibu, “Sisi ni mashahidi.” 23  “Basi, ondoeni miungu ya kigeni iliyo kati yenu, mwelekeze mioyo yenu kwa Yehova Mungu wa Israeli.” 24  Watu wakamwambia Yoshua, “Tutamtumikia Yehova Mungu wetu, nasi tutaitii sauti yake!” 25  Kwa hiyo Yoshua akafanya agano na Waisraeli siku hiyo, akawapa maagizo na sheria huko Shekemu. 26  Kisha Yoshua akaandika maneno hayo katika kitabu cha Sheria+ ya Mungu, akachukua jiwe kubwa+ na kuliweka chini ya mti mkubwa kando ya mahali patakatifu pa Yehova. 27  Ndipo Yoshua akawaambia watu wote, “Tazameni! Jiwe hili litakuwa ushahidi dhidi yetu,+ kwa sababu limesikia maneno yote ambayo Yehova ametuambia, nalo litakuwa ushahidi dhidi yenu, ili msimkane Mungu wenu.” 28  Basi Yoshua akawaruhusu watu waende zao, nao wakaenda kila mtu kwenye urithi wake.+ 29  Baada ya mambo hayo, Yoshua mwana wa Nuni, mtumishi wa Yehova, akafa akiwa na umri wa miaka 110.+ 30  Basi wakamzika kwenye eneo lake la urithi kule Timnath-sera,+ katika eneo lenye milima la Efraimu, upande wa kaskazini wa Mlima Gaashi. 31  Waisraeli waliendelea kumtumikia Yehova siku zote za Yoshua na sikuzote za wazee walioendelea kuishi baada ya Yoshua kufa ambao walikuwa wameona mambo yote makuu ambayo Yehova aliwatendea Waisraeli.+ 32  Na mifupa ya Yosefu,+ ambayo Waisraeli walikuwa wameleta kutoka Misri, wakaizika huko Shekemu katika shamba ambalo Yakobo alinunua kwa vipande 100 vya fedha+ kutoka kwa wana wa Hamori,+ baba ya Shekemu; nalo likawa urithi wa wana wa Yosefu.+ 33  Pia, Eleazari mwana wa Haruni akafa.+ Wakamzika katika Kilima cha Finehasi mwanawe,+ alichopewa katika eneo lenye milima la Efraimu.

Maelezo ya Chini

Yaani, Mto Efrati.
Yaani, Mto Efrati.
Tnn., “mbegu yake.”
Au “Bahari ya Shamu.”
Tnn., “siku nyingi.”
Yaani, upande wa mashariki wa.
Au labda, “wamiliki wa mashamba.”
Au labda, “waogope; watishike.”
Au “bila lawama.”
Au “ukweli.”
Yaani, Mto Efrati.
Au “nyumba.”
Yaani, Mto Efrati.