Yoshua 3:1-17

  • Waisraeli wavuka Yordani (1-17)

3  Ndipo Yoshua na Waisraeli wote* wakaamka asubuhi na mapema na kusafiri kutoka Shitimu+ mpaka Yordani. Wakalala hapo usiku kabla ya kuvuka.  Baada ya siku tatu, viongozi+ walipita kambini  na kuwaamuru watu, “Mara tu mtakapoliona sanduku la agano la Yehova Mungu wenu likiwa limebebwa na makuhani Walawi,+ mwondoke na kulifuata,  ili mjue njia ya kupita kwa kuwa hamjawahi kupita njia hiyo, lakini muwe umbali wa mikono 2,000* hivi kutoka kwenye sanduku hilo; msilikaribie zaidi.”  Kisha Yoshua akawaambia watu: “Jitakaseni,+ kwa maana kesho Yehova atafanya mambo yanayostaajabisha kati yenu.”+  Halafu Yoshua akawaambia makuhani: “Bebeni sanduku la agano+ na muwatangulie watu.” Basi wakabeba sanduku la agano na kuwatangulia watu.  Ndipo Yehova akamwambia Yoshua: “Leo nitaanza kukukweza machoni pa Waisraeli wote,+ ili wajue kwamba nitakuwa pamoja nawe+ kama nilivyokuwa pamoja na Musa.+  Waamuru hivi makuhani wanaobeba sanduku la agano: ‘Mtakapofika kwenye ukingo wa maji ya Yordani, ingieni na kusimama tuli ndani ya maji ya Yordani.’”+  Yoshua akawaambia Waisraeli: “Njooni hapa msikilize maneno ya Yehova Mungu wenu.” 10  Kisha Yoshua akasema: “Kwa njia hii mtajua kwamba Mungu aliye hai yumo miongoni mwenu,+ na bila shaka atawafukuza mbele yenu Wakanaani, Wahiti, Wahivi, Waperizi, Wagirgashi, Waamori, na Wayebusi.+ 11  Tazameni! Sanduku la agano la Bwana wa dunia nzima linawatangulia kuingia ndani ya Yordani. 12  Sasa chagueni wanaume 12 kutoka katika makabila ya Israeli, yaani, kila kabila mtu mmoja,+ 13  na mara tu nyayo za makuhani wanaobeba Sanduku la Yehova, Bwana wa dunia nzima, zitakapogusa maji ya Yordani, maji ya Yordani yanayotoka upande wa juu yatasimamishwa, yatakuwa tuli kama bwawa.”*+ 14  Basi watu walipotoka ndani ya mahema yao kabla tu ya kuvuka Yordani, makuhani waliobeba sanduku la agano+ wakawatangulia watu. 15  Mara tu makuhani waliobeba lile Sanduku walipofika Yordani na kutumbukiza miguu yao ukingoni mwa mto huo (kwa maana maji ya Yordani hufurika kwenye kingo zake+ sikuzote za mavuno), 16  maji yanayotoka upande wa juu yakaacha kutiririka. Yakasimama tuli kama bwawa* mbali sana huko Adamu, jiji lililo karibu na Sarethani, na yale yanayoshuka kwenye Bahari ya Araba, yaani, Bahari ya Chumvi, yakakauka. Yalisimamishwa, na watu wakavuka kuelekea Yeriko. 17  Makuhani waliobeba sanduku la agano la Yehova wakaendelea kusimama tuli kwenye nchi kavu+ katikati ya Yordani, huku Waisraeli wote wakivuka kwenye nchi kavu+ mpaka taifa lote lilipovuka Yordani.

Maelezo ya Chini

Tnn., “wana wote wa Israeli.”
Karibu mita 890 (futi 2,920). Angalia Nyongeza B14.
Au “ukuta.”
Au “ukuta.”