Yoshua 6:1-27

  • Kuta za Yeriko zaanguka (1-21)

  • Rahabu na familia yake waokolewa (22-27)

6  Basi malango ya jiji la Yeriko yalikuwa yamefungwa kabisa kwa sababu ya Waisraeli; hakuna mtu yeyote aliyetoka wala kuingia.+  Yehova akamwambia Yoshua, “Tazama, nimetia mikononi mwako Yeriko, mfalme wake, na mashujaa wake hodari.+  Ninyi nyote wanaume wa vita mnapaswa kulizunguka jiji hili, lizungukeni mara moja kwa siku. Mtafanya hivyo kwa siku sita.  Waagize makuhani saba wabebe pembe saba za kondoo dume na kulitangulia Sanduku. Lakini siku ya saba, mnapaswa kulizunguka jiji mara saba na makuhani watapiga pembe hizo.+  Pembe za kondoo dume zitakapopigwa, na mara tu mtakaposikia mlio wake,* watu wote watapiga kelele kubwa za vita. Kisha ukuta wa jiji utaanguka chini,+ na kila mtu ataingia jijini moja kwa moja.”  Basi Yoshua mwana wa Nuni akawaita makuhani na kuwaambia: “Bebeni sanduku la agano, na makuhani saba wabebe pembe saba za kondoo dume na kulitangulia Sanduku la Yehova.”+  Kisha akawaambia watu, “Nendeni mzunguke jiji, na wanajeshi wenye silaha+ walitangulie Sanduku la Yehova.”  Watu wakafanya kama Yoshua alivyowaambia, makuhani saba waliobeba pembe saba za kondoo dume mbele za Yehova, wakatangulia na kupiga pembe hizo, na sanduku la agano la Yehova lilikuwa likiwafuata.  Na wanajeshi wenye silaha waliwatangulia makuhani waliokuwa wakizipiga pembe, na walinzi wa nyuma walilifuata Sanduku huku pembe zikipigwa mfululizo. 10  Yoshua alikuwa amewaamuru hivi watu: “Msipige kelele wala kupaza sauti. Msiseme neno lolote mpaka siku nitakapowaambia, ‘Pazeni sauti!’ Ndipo mtakapopaza sauti.” 11  Akaagiza Sanduku la Yehova lipelekwe kuzunguka jiji mara moja, kisha wakarudi kambini na kulala humo usiku. 12  Asubuhi iliyofuata, Yoshua akaamka mapema, na makuhani wakalibeba Sanduku+ la Yehova, 13  makuhani saba waliobeba pembe saba za kondoo dume walilitangulia Sanduku la Yehova wakipiga pembe hizo mfululizo. Nao wanajeshi wenye silaha walitembea mbele yao na walinzi wa nyuma walilifuata Sanduku la Yehova huku pembe zikipigwa mfululizo. 14  Siku ya pili, walilizunguka jiji mara moja, kisha wakarudi kambini. Walifanya hivyo kwa siku sita.+ 15  Siku ya saba wakaamka asubuhi na mapema, wakalizunguka jiji kama kawaida. Ni siku hiyo peke yake ambayo walilizunguka jiji mara saba.+ 16  Na mara ya saba, makuhani walipiga pembe na Yoshua akawaambia watu: “Pazeni sauti,+ kwa kuwa Yehova amewapa jiji hili! 17  Jiji na vitu vyote vilivyomo vinapaswa kuharibiwa;+ vyote ni vya Yehova. Ila msimwangamize Rahabu+ yule kahaba na wote walio pamoja naye nyumbani mwake, kwa sababu aliwaficha wajumbe tuliowatuma.+ 18  Lakini mjiepushe na kitu chochote kinachopaswa kuharibiwa,+ ili msikitamani kitu kinachopaswa kuharibiwa na kukichukua,+ msije mkaleta msiba* kwenye kambi ya Waisraeli.+ 19  Lakini fedha yote na dhahabu na vitu vya shaba na chuma ni vitakatifu kwa Yehova.+ Vinapaswa kupelekwa katika hazina ya Yehova.”+ 20  Basi watu wakapaza sauti pembe zilipopigwa.+ Na mara tu watu waliposikia sauti za pembe na kupiga kelele kubwa za vita, ukuta ukaanguka chini.+ Kisha kila mtu akaingia jijini moja kwa moja, nao wakaliteka. 21  Wakaangamiza kwa upanga kila kiumbe kilichokuwa jijini, wanaume na wanawake, vijana na wazee, ng’ombe dume, kondoo, na punda.+ 22  Yoshua akawaambia wale wanaume wawili waliokuwa wameipeleleza nchi: “Nendeni katika nyumba ya yule mwanamke kahaba, mkamtoe nje pamoja na watu wake wote, kama mlivyomwapia.”+ 23  Basi wale vijana wapelelezi wakaenda kumtoa Rahabu, baba yake, mama yake, ndugu zake, na watu wote wa nyumba yake; naam, wakaitoa nje familia yake yote,+ na kuileta salama salimini nje ya kambi ya Waisraeli. 24  Kisha wakaliteketeza jiji pamoja na kila kitu kilichokuwemo. Lakini fedha, dhahabu, na vitu vya shaba na chuma, wakaviweka katika hazina ya nyumba ya Yehova.+ 25  Yoshua hakumwangamiza Rahabu yule kahaba, watu wa nyumba ya baba yake, na familia yake yote;+ Rahabu anakaa katika Israeli mpaka leo,+ kwa sababu aliwaficha wajumbe waliotumwa na Yoshua kupeleleza Yeriko.+ 26  Wakati huo Yoshua alitangaza kiapo* hiki: “Na alaaniwe mbele za Yehova mtu atakayejaribu kulijenga tena jiji hili la Yeriko. Atakapojenga msingi wake, mzaliwa wake wa kwanza atakufa, na atakapoweka malango yake, mwana wake wa mwisho atakufa.”+ 27  Basi Yehova alikuwa pamoja na Yoshua,+ na umaarufu wake ukaenea duniani pote.+

Maelezo ya Chini

Au “pembe zikipigwa kwa muda mrefu.”
Au “shida; laana.”
Au labda, “aliwaapisha watu kiapo.”