Zaburi 10:1-18

  • Yehova ni msaidizi wa wasio na uwezo

    • Mwovu hujigamba: “Hakuna Mungu” (4)

    • Wasio na uwezo humgeukia Yehova (14)

    • “Yehova ni Mfalme milele” (16)

ל [Lamed] 10  Ee Yehova, kwa nini unasimama mbali? Kwa nini unajificha nyakati za taabu?+   Mwovu humfuatia kwa kiburi mtu asiye na uwezo,+Lakini atanaswa katika njama anazopanga.+   Kwa maana mwovu hujigamba kuhusu tamaa zake za kichoyo*+Naye humbariki mwenye pupa;*נ [Nun] Humkosea heshima Yehova.   Kwa sababu ya kiburi chake, mwovu hafanyi uchunguzi wowote;Mawazo yake yote ni: “Hakuna Mungu.”+   Njia zake huendelea kufanikiwa,+Lakini hukumu zako zimepita uelewaji wake;+Huwadhihaki* maadui wake wote.   Anasema moyoni mwake: “Sitatikiswa kamwe;*Kizazi baada ya kizaziSitaona msiba kamwe.”+ פ [Pe]   Kinywa chake kimejaa laana, uwongo, na vitisho;+Chini ya ulimi wake kuna taabu na madhara.+   Huvizia karibu na makao;Kutoka mahali anapojificha humuua mtu asiye na hatia.+ ע [Ayin] Macho yake yanamtafuta mtu asiye na kosa.+   Hungojea mahali alipojificha kama simba katika pango* lake.+ Hungojea ili amkamate asiye na uwezo. Humkamata asiye na uwezo anapouvuta wavu wake na kuufunga.+ 10  Mtu huyo hupondwa na kuangushwa chini;Watu wasio na kosa huanguka mikononi mwake.* 11  Yeye husema moyoni mwake: “Mungu amesahau.+ Ameugeuzia mbali uso wake. Haoni kamwe.”+ ק [Qoph] 12  Inuka, Ee Yehova.+ Ee Mungu, inua mkono wako.+ Usiwasahau wasio na uwezo.+ 13  Kwa nini mwovu amemkosea Mungu heshima? Husema moyoni mwake: “Hutanifanya niwajibike.” ר [Resh] 14  Lakini unaona mateso na taabu. Wewe huendelea kutazama na kuchukua hatua.+ Mtu huyo asiye na kosa hukugeukia wewe;+Wewe ndiye msaidizi wa yatima.+ ש [Shin] 15  Uvunje mkono wa mtu mwovu na mbaya,+Ili utakapoutafuta uovu wake,Hutaupata tena. 16  Yehova ni Mfalme milele na milele.+ Mataifa yameangamia kutoka duniani.+ ת [Taw] 17  Lakini utasikia ombi la wapole, Ee Yehova.+ Utaiimarisha mioyo yao+ na kuwasikiliza kwa makini.+ 18  Utawatendea haki mayatima na wale wanaopondwa,+Ili mwanadamu anayeweza kufa ambaye ni mavumbi asiwaogopeshe tena.+

Maelezo ya Chini

Au “tamaa ya nafsi yake.”
Au labda, “Mwenye pupa hujibariki mwenyewe.”
Au “Hujitutumua kwa.”
Au “Sitapepesuka (Sitayumbayumba) kamwe.”
Au “pori.”
Au “katika makucha yake.”