Zaburi 101:1-8

  • Mtawala anayetenda kwa utimilifu

    • ‘Sitavumilia kiburi’ (5)

    • “Nitawatazama waaminifu” (6)

Muziki wa Daudi. 101  Nitaimba kuhusu upendo mshikamanifu na haki. Nitakuimbia sifa,* Ee Yehova.   Nitatenda kwa busara na bila lawama.* Utanijia lini? Nitatembea kwa utimilifu wa moyo+ ndani ya nyumba yangu.   Sitaweka kitu chochote kisichofaa* mbele ya macho yangu. Ninachukia matendo ya wale wanaokengeuka kutoka kwa jambo lililo sawa;+Sitashirikiana nao kamwe.*   Moyo uliopotoka uko mbali nami;Sitakubali* jambo lililo ovu.   Yeyote anayemchongea jirani yake kwa siri,+Nitamnyamazisha.* Yeyote aliye na macho ya kiburi na moyo wenye majivuno,Sitamvumilia.   Nitawatazama waaminifu wa dunia,Ili wakae nami. Yule anayetembea bila lawama* atanihudumia.   Hakuna mtu yeyote mdanganyifu atakayekaa katika nyumba yangu,Na hakuna mwongo atakayesimama mbele yangu.*   Kila asubuhi nitawanyamazisha* waovu wote wa dunia,Nitawaangamiza waovu wote kutoka katika jiji la Yehova.+

Maelezo ya Chini

Au “Nitakupigia muziki.”
Au “utimilifu.”
Au “cha ubatili.”
Au “Matendo yao hayashikamani nami.”
Tnn., “Sitajua.”
Au “Nitamwangamiza.”
Au “kwa utimilifu.”
Tnn., “mbele ya macho yangu.”
Au “nitawaangamiza.”