Zaburi 102:1-28

  • Sala ya mtu aliyekandamizwa, anapokuwa amekata tamaa

    • “Mimi ni kama ndege aliye peke yake” (7)

    • ‘Siku zangu ni kivuli kinachofifia’ (11)

    • “Yehova atalijenga upya Sayuni” (16)

    • Yehova hudumu milele (26, 27)

Sala ya mtu aliyekandamizwa, anapokuwa amekata tamaa* na kummwagia Yehova mahangaiko yake.+ 102  Ee Yehova, sikia sala yangu;+Kilio changu cha kuomba msaada na kikufikie.+   Usinifiche uso wako ninapokuwa katika taabu.+ Nitegee sikio lako;*Nijibu haraka ninapokuita.+   Kwa maana siku zangu zinatoweka kama moshi,Na mifupa yangu imeungua na kuwa myeusi kama tanuru.+   Moyo wangu umepigwa kama majani na umenyauka,+Kwa maana ninasahau kula chakula changu.   Kwa sababu ya kilio changu kikubwa cha maumivu,+Mifupa yangu inashikamana na nyama yangu.+   Mimi ni kama mwari wa nyikani;Mimi ni kama bundi mdogo katikati ya magofu.   Nikilala sipati usingizi;*Mimi ni kama ndege aliye peke yake juu ya paa.+   Mchana kutwa maadui wangu wananidhihaki.+ Wale wanaonidhihaki* wanatumia jina langu kama laana.   Kwa maana ninakula majivu kama mkate,+Na kinywaji changu kimechanganyika na machozi,+ 10  Kwa sababu ya hasira yako na ghadhabu yako,Kwa maana uliniinua juu ili unitupe tu pembeni. 11  Siku zangu zinafifia kama kivuli,*+Nami ninanyauka kama majani.+ 12  Lakini wewe unadumu milele, Ee Yehova,+Na umaarufu wako utadumu* katika vizazi vyote.+ 13  Kwa hakika utainuka na kulionyesha rehema Sayuni,+Kwa maana ni wakati wa kulionyesha kibali chako;+Wakati uliowekwa umefika.+ 14  Kwa maana watumishi wako wanayathamini mawe yake+Nao wanayapenda hata mavumbi yake.+ 15  Mataifa yataliogopa jina la Yehova,Na wafalme wote wa dunia utukufu wako.+ 16  Kwa maana Yehova atalijenga upya Sayuni;+Atatokea katika utukufu wake.+ 17  Ataisikiliza sala ya maskini;+Hataidharau sala yao.+ 18  Hili limeandikwa kwa ajili ya kizazi cha wakati ujao,+Ili watu watakaozaliwa* baadaye wamsifu Yah. 19  Kwa maana yeye hutazama chini kutoka katika makao yake matakatifu yaliyo juu,+Kutoka mbinguni Yehova huitazama dunia, 20  Ili asikie kilio cha maumivu cha mfungwa,+Ili awaweke huru wale waliohukumiwa kifo,+ 21  Ili jina la Yehova litangazwe Sayuni+Na sifa yake Yerusalemu, 22  Mataifa na falmeZinapokusanyika pamoja ili kumtumikia Yehova.+ 23  Alininyang’anya nguvu zangu kabla ya wakati;Alifupisha siku zangu. 24  Nikasema: “Ee Mungu wangu,Usiniangamize nikiwa katikati ya maisha yangu,Wewe ambaye miaka yako inadumu katika vizazi vyote.+ 25  Zamani za kale uliiweka misingi ya dunia,Na mbingu ni kazi ya mikono yako.+ 26  Zitaangamia, lakini wewe utadumu;Zote zitachakaa kama vazi. Na kama nguo utazibadili, nazo zitatokomea. 27  Lakini wewe ni yuleyule, na miaka yako haitaisha kamwe.+ 28  Watoto wa watumishi wako watakaa kwa usalama,Na uzao wao utaimarishwa kabisa mbele zako.”+

Maelezo ya Chini

Au “anapokuwa dhaifu.”
Au “Inama chini na unisikilize.”
Au labda, “Nimekonda sana.”
Au “wanaonifanya nionekane mpumbavu.”
Au “ni kama kivuli kinachorefuka.”
Au “jina lako litadumu.” Tnn., “ukumbusho wako utadumu.”
Tnn., “watakaoumbwa.”